How to Handle Your Monster-in-Law

How to Handle Your Monster-in-Law

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
58,636
Reaction score
220,353
Yvonne K. Fulbright Ph.D.
Yvonne_Fulbright.jpg


https://www.google.co.uk/url?sa=t&rct=j&q=&esrc=s&source=web&cd=1&cad=rja&uact=8&ved=0ahUKEwiqiO_9guPOAhUpIsAKHfZJCdYQFggcMAA&url=https://www.psychologytoday.com/blog/mate-relate-and-communicate/201311/how-handle-your-monster-in-law&usg=AFQjCNGli_WZiIQTnATtCOGQ6Ttdzzuowg&sig2=q4878lp7-AYFeUugKpO2SA



Nimekutana na hii habari katika pita pita zangu za leo, imeandikwa na Yvonne Fulbright, mwanamama mwenye PhD. ya pschology. Tatizo la kuishi na mama mkwe mkorofi liko karibu katika kila jamii. Mara nyingi anaona kwa malezi bora aliyompa mwanae ni kama wewe hustahili kuwa mke, mama wengine wanasahau kuwa na wewe mwenyewe unajitahidi uwezavyo kuwa sehemu ya familia yao na kuwa huko ulikotoka, malezi na makuzi yako yalikuwa tofauti kabisa. Fulbright anaeleza kuwa pia ni vizuri kuangalia tatizo liko wapi, angalia uhusiano wa mama na mtoto wake kabla ya kuja kwako wewe, inawezekana mama anaona umechukua mapenzi yote ya mwanae na yeye ameachwa mpweke.

Fulbright anausia kuwa, hata iweje, usipoteze uhalisia wako, kuwa wewe na ujaribu kumuonyesha kuwa una misimamo yako, pamoja na heshima yote utakayompa. Pia ni vizuri kuwa na "muda wa mimi". Muda huu utakusaidia kutafakari au kusahau kwa muda unayopita.

Jambo la mwisho ni vizuri kama mwenza wako atakusaidia kutojiingiza sana kwenye maswala ya familia, siyo kila linalotokea ndani anakwenda kumhadithia mama yake, na upande wako pia. Ndugu wakifahamu machache kuhusu ndoa yenu ni kheri. Pia uelewe si kila utakalo lifanya litapendwa na wakwe zako, ukiwaonyesha misimamo yako, tangia mwanzoni, wataelewa kuwa unamaamuzi yako ambayo hayawashirikishi wao.
 
Mbona Wahindi wanaishi hata na gmil sambamba na mil lakini maisha ni bien
Culture, ndoa nyingi za kihindi wanaoana kwa kujuana, mtoto wako wewe anaoa mtoto wa best friend wako ambae mlisoma wote au ni business partner wako. Hii mara nyingi ni kuhakikisha mali haiendi mbali, binti kama huyo atakuchukulia wewe na mkeo kama wazazi wake.
 
Yataka moyo sana, especially mama wakwe zetu na pia mazingira yetu ya kinyumbani ambapo culture can play a big role.
 
Yataka moyo sana, especially mama wakwe zetu na pia mazingira yetu ya kinyumbani ambapo culture can play a big role.
Ninadhani ukijiweka kuwa ipo siku na wewe pia utakuwa mama mkwe, jaribu kumwelewa na kumheshimu. Lakini asikubadilishe.
 
Hii hekima, lakini kuna wengine inakuwa ngumu.
Ukisha fahamu kiini cha matatizo inakuwa rahisi kuyatatua, matatizo mengi yakuwa ni class, anafikiria wewe si wa class yao, wewe hufanyi vitu vile anavyotaka yeye. Ukijaribu kubadilika itakusumbua sana.
 
Culture, ndoa nyingi za kihindi wanaoana kwa kujuana, mtoto wako wewe anaoa mtoto wa best friend wako ambae mlisoma wote au ni business partner wako. Hii mara nyingi ni kuhakikisha mali haiendi mbali, binti kama huyo atakuchukulia wewe na mkeo kama wazazi wake.
Sio best friend ndugu ila mtoto wa baba mkubwa anaoa au kuolewa na mtoto wa baba mdogo kulinda mali ya familia, mara nyingi ukiibuka ugomvi ktk mahusiano haya huitwa ugomvi wa familia coz hauna pande mbili.
 
Sio best friend ndugu ila mtoto wa baba mkubwa anaoa au kuolewa na mtoto wa baba mdogo kulinda mali ya familia, mara nyingi ukiibuka ugomvi ktk mahusiano haya huitwa ugomvi wa familia coz hauna pande mbili.
Nimeshaona Wahindi ambao ni share holders kwenye biashara, waamua kuoza watoto wao, wengine ni kutokana na professinals za, unakuta lawyers walisoma pamoja, wamefungua law firm pamoja, wanawekeza kwenye elimu ya watoto kufuata mfumo wa sheria na wanakuja kuoana na kuendeleza kilichoanzishwa na wazazi wao.
 
Sio wahindi tu kwa nilichokieleza hapo juu ila hata Wapemba wengi wapo hapa ktk kulinda mali isitapanywe. Ila kiukweli wengi nia yao kubwa ni kulinda mali na fedha tu sio kitu kingine.
 
Ukisha fahamu kiini cha matatizo inakuwa rahisi kuyatatua, matatizo mengi yakuwa ni class, anafikiria wewe si wa class yao, wewe hufanyi vitu vile anavyotaka yeye. Ukijaribu kubadilika itakusumbua sana.


Haya mambo ya class kwa kweli yanakuaga magumu. Si vizuri kuingia mahali ambapo mmoja atanyanyasika.

Lakini kama ma mkwe yuko kwangu, it's not fair atake nifanye vile anataka yeye. If she's at my house she should play by my rules. Of course heshima itabaki pale pale lakini kwa mengine, she'll have to go with my flow...thory.
 
Culture, ndoa nyingi za kihindi wanaoana kwa kujuana, mtoto wako wewe anaoa mtoto wa best friend wako ambae mlisoma wote au ni business partner wako. Hii mara nyingi ni kuhakikisha mali haiendi mbali, binti kama huyo atakuchukulia wewe na mkeo kama wazazi wake.
ila hii culture ni nzuri sana hata ukisoma biblia ndo ilikuwa inatumika
leo mtu wa musoma anaoa songea huko mpaka mje msomane sio leo mshaumizana sana
 
Haya mambo ya class kwa kweli yanakuaga magumu. Si vizuri kuingia mahali ambapo mmoja atanyanyasika.

Lakini kama ma mkwe yuko kwangu, it's not fair atake nifanye vile anataka yeye. If she's at my house she should play by my rules. Of course heshima itabaki pale pale lakini kwa mengine, she'll have to go with my flow...thory.
Anakuja kusalimia anaanza kubadilisha ratiba za nyumba, watoto wanatakiwa walale saa hii, mimi sikulea wanangu hivi..Unamwambia mama hawa ni wajukuu wako lakini ni watoto wangu mimi.
 
ila hii culture ni nzuri sana hata ukisoma biblia ndo ilikuwa inatumika
leo mtu wa musoma anaoa songea huko mpaka mje msomane sio leo mshaumizana sana
Cha muhimu ufahamu utakae ishi nae ni mwanaume, kama mnadate na unampenda, ndugu msiwaruhusu waingie na kujua sana mahusiano yenu.
 
  • Thanks
Reactions: kui
Cha muhimu ufahamu utakae ishi nae ni mwanaume, kama mnadate na unampenda, ndugu msiwaruhusu waingie na kujua sana mahusiano yenu.
sio rahisi kibongobongo mamilicious
ni wachache watakaokuacha
cc bossylady na madale family
 
Back
Top Bottom