Housegirl kanichanganya sana!

Housegirl kanichanganya sana!

Ukiwa mchafu utavuna uchafu....

Inaelekea wewe uko na pepo mbaya na huyo pepo anawatafuneni na kuwavuruga.NA BADO!
 
Tukiongea kiume ningeshauri huyo h/g umpandishe cheo na kumfanya small hausi na kumpangia mbali na home lakini kwakuwa kakiri kutembea na mlinzi huyo atakuwa ugawaji fukuza wote.
Kweli kabisa mkuu!!nashukuru kwa ushauri!
 
Mhh Ibilisi kweli ulitupwa duniani,kwanza kabisa anza na hg kabla hajaanza kuonesha dharau kwa mkeo na kuharibu kabisa mpango wako wa kumfukuza hata mlinzi kwani huwa wana viburi hwa pale wanapokuwa wamevuliwa c***i na baba mwenye nyumba.
then fanya utaratibu tafuta mlinzi mwingine akashatia timu hapo mwambie kabisa tunashukuru kwa kukaa na wewe muda woote japo ulionekana mwenye udhaifu wako ni huu,kama upo tayari kujadili la mlinzi alimchakachua mkeo basi uwe tayari kujadili mbele ya mkeo kuwa umemchakachua hg lakini kama hutaki hayo timua wote kwa pamoja kama nilivyoeleza hapo awali then mkae chini na mkeo MKAPIME AFYA ZENU MAANA MNA UHAKIKA GANI NA MLIOFANYA NAO MAPENZI NI WAZIMA.
Endeleeni kuomba toba kwa Mungu pia kama ni wakristo Neno la Mungu linasema ijapokuwa dhambi zenu ni nyekundu kama bendera atazifanya nyeupe kama theluji,ili muitunze familia yenu kwa uaminifu.
Utamu wa mke hukolezwa na wewe hakuna kiungo chakununua dukani
Kila la kheri
Mkuu nashukun sana umenipa ushauri mzuri sana, mungu akubariki!!
 
isijekuwa ni ndoto aliota ucku then akasahau akajua ni real story. Nataman aje tena a2ambie samahan wanajamvi hii ilkuwa ni ndoto niliyoota ucku. Yan nngefurahi kupita maelezo cz ameniumiza utadhan mm ndo my wife wake.
Mkuu hii ni habari ya kweli kabisa na wala si ndoto!!
 
hapo..imekulaa kwako,na mlinzi ndo mjanjaa kachakachuaa zoteee,wee cha muhimu endeleaa na house gal na mkeo aendelee na mlinzi,hiyo ndoa ivunjwee
Nashukuru sana kwa ushauri wako!!
 
Umenikumbusha story ya rafiki yangu juzjuzi tu. Baada ya kuona maisha yamekuwa magumu, alimwita mkewe na kumwambia ajifunze kupika ili wamfukuze housegirl. Mke kwa unyenyekevu akajibu, 'sawa mume wangu, na wewe jifunze kuto*** ili tumfukuze mlinzi'
Duh!hii kali kweli kweli!
 
Mimi kuna kitu kinaniumiza katika hili, Mnaposema sema fukuza huyo house girl as if yeye ndio mwanzo wa matatizo wakati hao wanandoa ndo wana matatizo wenyewe. HOUSE GIRL mmemfanya kama sio mwanadamu mwenye haki wala sioni thamani yoyote mnayompa (FUKUZA HOUSE GIRL). Kumchakachua umemchakachua, kumfukuza kazi unamfukuza halafu kinafuata nini?? Unamfukuza kwa kosa gani, hataa mbwa akifukuzwa anakuwa amekosea kitu.

Unasema umetubu labda kwa Mungu na kwa watu pia, kama kweli umetubu kwa kumaanisha, unaposema umfukeze house girl au mlizi unataka waende wapi?? Maskini wa Mungu walikuwa wanajipatia mkate wao wa kila siku kwa kukufanyia kazi wewe. Lakini kwa tamaa zenu mnawanyima furaha, hasa huyo binti maskini kakosa nini??

Nyie wote wanandoa mjue mlikuwa mnakomoana, yawezekana huyo mkeo, aliamua kutoka namlinzi baada ya kujua kwamba unatoka na house girl. Daaa mi kinauma kwa kweli, watoto wetu hawa wanaofanya kazi nyumbani kwa watu, yani nyumba nyingine sio nyumba kabisa ni mlango wa kwenda jehanamu.

Mi sijui kama nimekusamehe, mpaka nitakapojua, umechukua uamuzi gani juu ya huyo binti na huyo kaka.
Wala sioni cha kukwambia zaidi ya hili. TUBU KWA KUMAANISHA KUACHA, KAA NA HUYO MKEO MTUBIANE UOVU WENU. Mgeuke kuwa baba na mama wenye mfano wa kuigwa. MKISHAFANYA hivo kama unamfukuza huyo binti ujue anakwenda wapi kufanya nini, na maisha yake yataendelea je?? Yani ningekuwa mwamuzi wa hii kesi TUKUTUKU sijui ningekupa adhabu gani ................................basi tu,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

Na hata kama umetunga. Kuna viumbe vinafanya mchezo kama huu. Washindwe!!!
Nashukuru kwa ushauri wako mkuu!!
 
Hapo nilipopigiliamsumari ni kwmba MLINZI ALISHA TAFUNA WOTE YAANI HOUSE GIRL NA MKEO, ILA HOUSE GIRL WAKO BADO NI MTAMU.

MIMI NI MWANASAIKOLOJIA, NA HAPA NAONA KUWA WEWE ULISHAHISI MKEO SIYO MTAMU NDIO MAANA UKAKIMBILIA NJE (KWA HOUSE GIRL WAKO).

NA KWA KUWA MLINZI PIA ALISHANOGEWA NA HOUSEGIRL, BASI NADHANI HAMCHAPI TENA MKEO, ANAENDELEA KUCHAP HUYO HOUSE GIRL.

HIVYO, USIMFUKUZE MKEO, MFUKUZE HOUSEGIRL ILI KUWE NA AMANI NDANI YA NYUMBA YAKO.

BAADA YA HAPO, UKAE WEWE NA MKEO NA MLINZI MZUNGUMZE OPENLY UMWAMBIE UKWELI, INGAWA KUNA SHAKA KUWA AKIONDOKA HOUSEGIRL, PENGINE MLINZI WAKO ATAENDELEZA UTAFUNAJI WA MKEO. HAPO KAA CHONJO!

ALTERNATIVE NYINGINE NI KUFUKUZA HOUSEGIRL NA MLINZI WAKAANZE MAISHA MAPYA NA WEWE UIJENGE FAMILIA YAKO.
Nashukuru sana mkuu kwa ushauri wako mkuu!
 
Hii nimewahi sikia kijiweni kwetu ililetwa na mtu mmoja akatuuliza kama ni baba mwenye nyumba ungefanyaje? Napata kigugumizi kuamini hii imemtokea tukutuku.
Sawa mkuu naona umeamua kunitosa,cha msingi hapa ni kunipa ushauri,mwenzio nina matatizo katika ndoa yangu!!
 
MKUU POLE SANA KWA TAMAA ZAKO!PILI LABDA NIKUULIZE HUYO BEKI TATU ANA UMRI KWANZA,TATU, NI NINI KIMEKUFANYA UTEMBEE NA HUYO BEKI TATU WAKO,NI KIPI KILICHOKUVUTIA MAPAKA UKALALA NAYE?NI UMBO AU

USHAURI;
MFUKUZE KWANZA HUYO BEKI TATU
KISHA MFUKUZE NA MLINZI :usa2:
 
Likely 2b a cook story. But these things do happen. Be careful. Hujawahi sikia mume kutembea na h/g au mke na h/b au na mlinzi. Akili za kuambiwa changanya na zako.
Mimi nashangaa hao wanaobisha wakati ni real life context,this things happen!!
 
Mchane live mlinzi kuwa kale ka agenda kake ka kudandia ndan ya nyumba umegundua ila usimwambie kamchakachua nani na mwambie unaendelea na uchunguz mkali ukibaini ameingia ndan zaid basi ajue ama zake ama zako na kama anajua amefika ndan zaid bora atimue mapema sabb hupend kumharibia.kama ni kweli mlinz alipiga ndani atajua dil limebuma atateleza mwenyew ila ka ni fitna za hg nahc atakuwa mvumilivu na hapo itakuwa rahic kwako kumchuja mbaya wako.
Nashukuru sana mkuu kwa ushauri wako!!
 
Ili mradi mlinzi amekiri kuwa Hg ni zaidi ya mkeo. Cha kufanya achana na Hg ili mlinzi aendelee kujinafasi huko na wewe endelea na mkeo.
Nashukuru sana mkuu kwa ushauri wako!!
 
Sawa mkuu nimeshakiri kuwa nini makosa na nikaomba mnisamee!naomba ushauri wako namna ya kumfukuza mlizi!!
Huyo mlinzi unamlipa au anakulipa wewe mshahara??amka asubuhi moja just sema kuanzia sasa sitaki kukuona ktk nyumba hii,tena mtoe baruti kali,ila uhakikishe kuwa ni kweli kuwa alishatembea na hg na wife wako,then muite hg wako nae mtimue kwa sytle ileile uliyomfanyia mlinzi!hapo ndio wana jf tutauelewa msamaha wako!
baada ya hili zoezi muite wife wako na umueleze kila kitu kuhusu wewe kutembea na hg wako na yeye kutembea na mlinzi.then kubalianeni kuanza upya kwa kuwa mko ktk ndoa!na hao wote waliwakuteni nyie na maisha yenu!!afu mkuu si vyema kuchakachua ma hg huo ni udhaifu wa kutumia ignorance ya mtu!AIDS KILLS
 
Mimi nina uhusiana wa kimapenzi na housegirl wangu.Siku moja tulikuwa faragha, tukifanya mapenzi,baada ya kumaliza kufanya mapenzi nilimsifia sana na kumwambia penzi alilonipa ni tamu sana kuliko hata la mke wangu.
Baada ya kusikia hivyo alifurahi sana na kusema asante sana Baba kwa kuniambia ukweli,hii ni mara ya pili,mara ya kwanza Mlinzi aliwahi kunisifia na kuniambia penzi langu ni tamu sana kuliko la mama(Mke wangu),nilimbishia sana na kuamini alikuwa ananitania.Sasa leo nimeamini baada ya wewe pia kunisifia.
Baada ya kusikia hayo nilichanganyikiwa sana,na hasa baada ya kugundua kuwa mlinzi wangu kumbe anatembea na mke wangu wa ndoa.Baada ya kufikiri kwa kina niligundua kuwa mimi nilikuwa mkosefu sana,sistahili hata kidogo kumfukuza mke wangu,lakini ni lazima nimfukuze mlinzi ili kunusuru ndoa yangu.Kinachonitatiza ni namna ya kumfukuza huyu mlinzi wangu.Sote kama familia tunaamini ni mchapa kazi na hana mapungufu yoyote ambayo naweza kuyatumia kumfukuza kazi.Je nitumie mbinu gani ili niweze kumfukuza .
Najua nina makosa,lakini naomba wanaJF wote mnisamehe,kwa kuwa hakuna binadamu aliyekamilika,kila mtu ana mapungufu yake.Naomba ushauri wenu namna ya kumfukuza mlinzi.
Nawasilisha!!

Kwa nini unataka kumfukuza huyo mlinzi? Je ni kwa sababu amekula tunda la maspap au ni kwa sababu amekula matunda ya wote yaani mamsap and house girl? Mimi nashauri uwafukuze wote wawili yaani house girl and mlinzi halafu umuombe msamaha mke wako na pia umtake akuombe msamaha.
 
Back
Top Bottom