Hotuba ya Rais Kikwete kuliaga Bunge - 09, Julai 2015

CCM bila Lowassa ni sawa na kwenda shamba bila jembe!! - Kawakamata na wamekamatika.

Wakithubutu tu - basi wana-RIP.
 
Akihutubia bunge jana, rais Jakaya Kikwete pamoja na mambo mengine alisema katika kipindi cha miaka kumi ya utawala wake, vyama vya siasa vimekuwa na uhuru zaidi wa kufanya shughuli zao kama mikutano na maandamano. Lakini cha ajabu ni kuwa rais "alisahau" kusema kuwa ni katika shughuli hizo hizo ndipo vyombo vya dola vimekuwa vikipiga raia wasiokuwa na hatia, kuwajeruhi kwa virungu na mabomu, kuwaua na kuwaweka ndani kisha kuwafungulia mashitaka. Mifano hai ni mingi wala hangekuwa na haja ya kutoa mifano kwani inajulikana kitaifa na kimataifa.
 
Kuna watu bado mnatilia maanani anayosema huyo jamaa, poleni. Wengi tunampuuza.
 
kikwete huwa ni kauzu zaidi ya dagaa,wewe imagine "guts" za kusema maisha bora ni pamoja na foleni za magari,watu kupanda ndege na kununua bajaji kwa ajili ya wagonjwa mahututi kupelekwa hospitali!!!!this coastal indigenous has got balls.
 
kikwete huwa ni kauzu zaidi ya dagaa,wewe imagine "guts" za kusema maisha bora ni pamoja na foleni za magari,watu kupanda ndege na kununua bajaji kwa ajili ya wagonjwa mahututi kupelekwa hospitali!!!!this coastal indigenous has got balls.

Aisee nilisikitika sana ila nilikasirika zaidi pamoja na kauli hizi dhaifu kabisa alikuwa akipigiwa makofi na mengi na Wabunge wa CCM..

Haya tunayoyaona ni matokeo ya uongozi dhaifu ndio unaoweza kuwa kuwa kipimo cha uchumi wa nchi ni foleni kuwa Kali/watu kupanda ndege /Nyumba zilizoezekwa kwa mabati nk....
 
alisahau katika utawala wake diamond platinum alinyakua tuzo 3 za channel 'O' kitu ambacho nyuma hakikutokea....makofii jamaaaaan
 
Wana jamii nimeuliza hili swali kutokana na sehemu ya hotuba ya rais kufunga bunge niliyoisikiliza jana.
Rais katoa takwimu mbalimbali, katika mambo mbalimbali kudhihirisha kuwa kuna maendeleo yanaonekana ukilinganisha mihula yake ya uongozi na mingine iliyopita.
Nimebaki na maswali kwenye hayo maeneo mawili zaidi japokuwa pia hatuwezi kuhakiki sana usahihi wa hizo takwimu zilizotolewa katika nyanja tofauti tofauti. Alisema kuwa siku hizi familia zina gari la baba, mama na mtoto/watoto, je ni familia zipi hizo anazosemea? Isikute sana sana zote zenye uwezo huo ni hizo zenye wanachama wa chama chake maana sababu ndio wanaowezeshwa kwa kupatiwa kazi na nafasi zenye ulaji (ufisadi au rushwa), na zile za wanasiasa (hasa wa chama tawala) ambao wao moja kwa moja zinajulikana uadilifu wao.
Wa kawaida sio rahisi sana labda akijipinda sana apate kavitz na hapo deni utakuta kapitia saccos au against salary, hapo ataweza kumnunulia mke na mtoto?
Kuhusu kupanda ndege rais ametumia neno kama ka kejeli, nanukuu ''watanzania nao siku hizi wanapanda ndege'' ni maendeleo haya jamani. Inawezekana anaona airport kunafurika na akajua uwezo wa mtanzania umeongezeka anapanda ndege. Lakini wanaweza kuwa wanapanda kujiepusha na ajali za kila leo kwa kujikusuru tu, hawana sana lakini uzima tu ni muhimu zaidi kuliko kubania halafu hufiki salama, ukifika salama utapambana na ya kesho.na wengine wanalipiwa na ofisi, kwa uwezo wao wasingeweza.
Na zaidi ya hapo audience iliyokuwa inamshangilia ni wale wenye huo uwezo uliotajwa, sidhaani kama wale wanaogawiwa kofia, kanga na pilau na wakagawa kura walikuwepo kwenye hao washangiliaji
 
Nimesikiliza hotuba ya majigambo ya Kikwete jana na nilisikiliza watia nia wa CCM ngazi ya urais walivyokuwa wakiiponda kiaina serikali hii kuwa haijafanya chochote walipokuwa wanatangaza nia zao na walipokuwa wakipita mikoani kutafuta wadhamini, huku wakituaminisha wao ndio wanaweza kutusaidia kwa matumaini.

Je mkweli ni nani ikiwa hawa hawa ndio walimpigia makofi huyu mwenyekiti wao jana?

Je niamini wote ni wasanii wale wale wanaocheza na akili za watanzania?

 
Wana jamii nimeuliza hili swali kutokana na sehemu ya hotuba ya rais kufunga bunge niliyoisikiliza jana.
Rais katoa takwimu mbalimbali, katika mambo mbalimbali kudhihirisha kuwa kuna maendeleo yanaonekana ukilinganisha mihula yake ya uongozi na mingine iliyopita.
Nimebaki na maswali kwenye hayo maeneo mawili zaidi japokuwa pia hatuwezi kuhakiki sana usahihi wa hizo takwimu zilizotolewa katika nyanja tofauti tofauti. Alisema kuwa siku hizi familia zina gari la baba, mama na mtoto/watoto, je ni familia zipi hizo anazosemea? Isikute sana sana zote zenye uwezo huo ni hizo zenye wanachama wa chama chake maana sababu ndio wanaowezeshwa kwa kupatiwa kazi na nafasi zenye ulaji (ufisadi au rushwa), na zile za wanasiasa (hasa wa chama tawala) ambao wao moja kwa moja zinajulikana uadilifu wao.
Wa kawaida sio rahisi sana labda akijipinda sana apate kavitz na hapo deni utakuta kapitia saccos au against salary, hapo ataweza kumnunulia mke na mtoto?
Kuhusu kupanda ndege rais ametumia neno kama ka kejeli, nanukuu ''watanzania nao siku hizi wanapanda ndege'' ni maendeleo haya jamani. Inawezekana anaona airport kunafurika na akajua uwezo wa mtanzania umeongezeka anapanda ndege. Lakini wanaweza kuwa wanapanda kujiepusha na ajali za kila leo kwa kujikusuru tu, hawana sana lakini uzima tu ni muhimu zaidi kuliko kubania halafu hufiki salama, ukifika salama utapambana na ya kesho.na wengine wanalipiwa na ofisi, kwa uwezo wao wasingeweza.
Na zaidi ya hapo audience iliyokuwa inamshangilia ni wale wenye huo uwezo uliotajwa, sidhaani kama wale wanaogawiwa kofia, kanga na pilau na wakagawa kura walikuwepo kwenye hao washangiliaji

Kuna familia inasemekana ina semi trela zaidi ya 200 labda hiyo ndiyo anayoisemea!
 
Kwa kweli chama chetu kimeshindwa kutoka usingizini hata baada ya kupigiwa king'ora, sasa alikuwa anahutubia Bunge au Mkutano wa CCM?
 
Hizo ndo mi naita sifa za kijinga jinga... Muulize serikali yake ime-subsidize kwenye bati, sementi,n.k kwa kiasi gani...??
Hajui kuwa watu wake wanakula mlo mmoja ili tu waweke akiba kuzijenga hizo nyumba na kununua hayo magari..?? Wa hovyo sana huyu! Bora liende!

Mkuu.., kula tano kwa kusoma between the lines!
Ni wachache sana wenye kuweza kuona hilo/kufikiria mbali!
Wengi wanaishia kumpigia makofi..., bila kuelewa porojo za Le Profeseri!

"If someone fools me once, shame on him........"
 
Pamoja na hayo, hatukusita wala kuchelea kuchukua hatua pale uhuru huo ulipotumiwa vibaya na kutishia kuvuruga amani, umoja na usalama wa jamii au taifa. Au, pale ambapo Sheria za nchi zimekiukwa. Huo ni wajibu wetu wa kikatiba ambao mimi na wenzangu tuliapa kuutimiza.


sasa nimeelewa kwa nini walimpeleka Mabwepande.
 
1. Mazingira ya Kisiasa visiwani Zanzibar yamekuwa bora kuliko awali kabla ya Muafaka kati ya CCM na CUF


2. Nchi yetu iko salama, mipaka iko salama. JWTZ imefanya kazi na Jeshi letu limeimarishwa nyanja zote, Jeshi letu lina utayari wa kivita kwa kiwango cha hali ya juu. Weledi umepanda kwa kiwango kikubwa


3. Demokrasia, imeimalishwa mpaka kufikia hatua wanasiasa wanaandamana, wanatoka nje ya Bunge.


4. TAKUKURU imepewa meno ya kudhibiti na kupambana na Rushwa. Ina ofisi kila Mkoa na kila Wilaya


5. Mafanikio makubwa, mapato ya Serikali yameongezeka. Bajeti ya Serikali imekuwa mara 5 ya mwaka 2005 ilivyokuwa, Tumepunguza utegemezi wa misaada katika Bajeti toka 42% hadi 8% kwa kusimamia ukusanyaji mapato, Pato la Taifa limekua kwa 7%, Tanzania ni miongoni mwa mataifa 20 Duniani yenye uchumi unaokua kwa kasi IMF wanasema Pato la Tanzania ni kubwa kuliko walivyodhania. Tumebakiza kidogo sana kuingia kwenye Nchi za Pato la Kati .


6. Taarifa za CAG zinapewa uzito mkubwa na hatua huchukuliwa. POAC/PAC imefanya kazi nzuri. Pale inapobainika kuna wizi, hatua za haraka kuwajibisha wahusika zinachukuliwa hata bila kusubiri kuwasilishwa Bungeni.

7. Hati zimeongezeka Serikalini tokana na utendaji mzuri wa Ofisi ya CAG pia imejili vijana wenye CPA zaidi ya 780 na kuwasambaza nchini.



8 Ongezeko la Majaji wa Mahakama ya Rufani toka 8 hadi 16. Majaji wanawake wameongezeka toka 8 hadi 37 majaji wakazi 1,266 na kati yao majaji wanawake ni 534 mrundikano wa kesi utakuwa historia katika muda mfupi ujao tokana na ongezeko la majaji na mahakimu.


9. Ujenzi wa Mahakama kila Mkoa unaendelea katika Mikoa 9. kutenganisha kazi ya Upelelezi na Kushtaki


10. Kila mwaka tumeongeza kima cha chini cha mshahara toka TZS 65,000/= (2006) hadi TZS 300,000/= (2015)


11. Vyuo vikuu kulikuwa na wanafunzi wa kike 10,000+ mwaka 2005 na sasa wamefikia 78,000+,Idadi ya wabunge wanawake imeongezeka toka 62 hadi 127 sasa!

Itaendelea
 
Back
Top Bottom