Hotuba ya rais Kikwete Bungeni Julai 16 - Full Text

Hotuba ya rais Kikwete Bungeni Julai 16 - Full Text

Namnukuu:

Mheshimiwa Spika,
Kwa upande wa wasanii hasa wa muziki, katika miaka mitano hii tumeshuhudia kukua na kustawi kwa muziki wa kizazi kipya na uigizaji wa filamu. Nasikitishwa sana na hali ya wasanii kutokupata malipo ya haki kwa kazi zao. Niliamua nijaribu kusaidia. Nilipokutana na baadhi ya wana muziki wa kizazi kipya wakanieleza haja ya wao kuwa na mastering studio yao ili waweze kumiliki kazi zao. Nimeshawanunulia mtambo huo uliogharimu shilingi 50 milioni. Hivi sasa tumelipia mtaalamu mshauri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam asaidie kutengeneza njia bora ya kusambaza kazi za wasanii wa muziki na filamu ili wapate malipo halali kwa jasho lao. Mafanikio ya zoezi hili yatatufundisha namna ya kuwasaidia wasanii wa fani nyingine pia.
Mheshimiwa kweli kafanya kazi kubwa sana, ni mfano wa kuigwa :smash:
 
Huyu jamaa ni muongeaji mzuri. Utekelezaji mh! Pia bunge lingekuwa linajaa hivi mwaka mzima ingekuwa kheri
 
Michezo, Burudani na Utamaduni
Mheshimiwa Spika,
Tuliahidi kuendeleza shughuli za michezo na utamaduni. Tumerudisha michezo mashuleni ili tujipe fursa ya kubaini vipaji vya watoto wetu na kuviendeleza. Nimetimiza ahadi yangu ya kumgharimia mwalimu wa mpira wa miguu wa Timu ya Taifa Stars kutoka nje. Kocha Marcio Maximo kutoka Brazil aliajiriwa na amesaidia sana kuinua kiwango cha soka hapa nchini. Tanzania imepanda kutoka nafasi ya 172 Desemba 2005 hadi nafasi ya 108 Aprili 2010. Mimi naamini kama tutaongeza juhudi tupo karibu kufanikiwa zaidi.

Tumeshapata makocha wa riadha na ngumi. Nimekubali ombi la CHANETA kumlipia kocha wa mchezo wa netiboli. Hivi karibuni nilisaidia kugharimia kambi ya mazoezi na posho za wachezaji wa Twiga Stars ili waweze kushiriki vizuri katika mashindano ya soka la wanawake Afrika. Ushindi wao ni fahari ya nchi yetu. Tutaendelea kuwasaidia ili waendelee kupeperusha Bendera yetu kwa mafanikio makubwa zaidi.
Nafurahi kwamba kupitia Taifa Stars moyo wa uzalendo umezidi kuongezeka miongoni mwa Watanzania. Tofauti na ilivyokuwa zamani, ni jambo la kawaida kuwaona Watanzania wakivaa jezi za timu yetu ya taifa au wakienda uwanjani wakiwa wanapeperusha bendera yetu ya taifa.

Mheshimiwa Spika,
Kwa upande wa wasanii hasa wa muziki, katika miaka mitano hii tumeshuhudia kukua na kustawi kwa muziki wa kizazi kipya na uigizaji wa filamu. Nasikitishwa sana na hali ya wasanii kutokupata malipo ya haki kwa kazi zao. Niliamua nijaribu kusaidia. Nilipokutana na baadhi ya wana muziki wa kizazi kipya wakanieleza haja ya wao kuwa na mastering studio Nimeshawanunulia mtambo huo uliogharimu shilingi 50 milioni. Hivi sasa tumelipia mtaalamu mshauri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam asaidie kutengeneza njia bora ya kusambaza kazi za wasanii wa muziki na filamu ili wapate malipo halali kwa jasho lao. yao ili waweze kumiliki kazi zao. Mafanikio ya zoezi hili yatatufundisha namna ya kuwasaidia wasanii wa fani nyingine pia.
 
Ahsante mhe rais kwa kuendelea kusimamia nchi yetu vizuri mpaka kuendelea kudumisha amani, utulivu na upendo wetu pamoja na kudumisha muungano wetu.

Ahsante kwa kuendeleza yale mazuri yaliyoachwa na viongozi waliotangulia na kuweza kuhimili vishindo vyote kutoka kwa watu na makundi mbalimbali na ahsante tena kwa kusamehe wale wote waliokukosea kwa namna moja au nyingine katika utendaji wako

Nakuombea mazuri huko mbeleni uzidi kuwa na nguvu zaidi kama ukifanikiwa kuchaguliwa tena na wananchi wa Tanzania uweze kutuwekea viongozi mahiri, shupavu na wazalendo ambao wataweza kuwa msaada kwako na kwa taifa hili siku za mbeleni.
 
Nimerekodi sehemu kubwa ya hotuba ya Rais na utaweza kuiona kwenye channel yangu ya youtube/mwanakijiji
 
Huyu jamaa ni muongeaji mzuri. Utekelezaji mh! Pia bunge lingekuwa linajaa hivi mwaka mzima ingekuwa kheri
Jamani, kuna baadhi ambayo ameyaongea anadai yametekelezwa, na anavyosema mengine yapo njiani kutekelezwa (mpeni kura!) hivyo tuwe watu wa subira, itapendeza mtu akasoma juu ya mafanikio ya awamu ya nne kwenye attachment na kisha akachangia, naamini hapo ndipo tutakuja na hotuba mbadala ya hii ya mheshimiwa rais.

Nasubiri kwa hamu sana comments za comrade Malaria Sugu (MS)
 
Kikwete said:
Nimeshawanunulia mtambo huo uliogharimu shilingi 50 milioni.

..hapa ametoa pesa yake mfukoni kununua huo mtambo, au ni pesa ya serikali yetu?

..linganishe pesa hizo na mabilioni yaliyotumika kuileta timu ya mpira ya brazil.
 
Jamani, kuna baadhi ambayo ameyaongea anadai yametekelezwa, na anavyosema mengine yapo njiani kutekelezwa (mpeni kura!) hivyo tuwe watu wa subira, itapendeza mtu akasoma juu ya mafanikio ya awamu ya nne kwenye attachment na kisha akachangia, naamini hapo ndipo tutakuja na hotuba mbadala ya hii ya mheshimiwa rais.

Nasubiri kwa hamu sana comments za comrade Malaria Sugu (MS)

Mmh,Invisible na wewe unamkampenia Rais Kikwete,duu,kumbeee sasa nimepata nimekuelewa.
 
Hebu msikilizeni Rais anachosema kuhusu suala la TRL ... "

Nyote ni mashahidi kwamba tumehangaika sana na Reli zetu mbili za TAZARA na Reli ya Kati katika kipindi hiki cha miaka mitano. Kwa miaka kadhaa Reli reli zetu hizi zilikuwa na matatizo mengi na kusababisha huduma za uchukuzi wa abiria na mizigo kuathirika. Kiini cha tatizo ni uendeshaji usioridhisha. Kwa ajili hiyo, Serikali ya Awamu ya Tatu iliamua kutafuta kampuni ya uendeshaji wa reli ije isaidie kuendesha Reli yetu ya Kati. Hivyo ikapatikana kampuni ya RITES ya kutoka India. Wakati ule iliaminika kuwa kampuni hiyo ingesaidia kupata jawabu kwa tatizo linaloisibu reli yetu. Bahati mbaya matarajio yetu hayakuwa, ndiyo maana tumelazimika kufanya uamuzi tulioufanya wa kuanza mazungumzo na wabia hao ili Serikali ichukue tena reli hiyo na kutafuta namna nyingine iliyo bora ya kuiendesha reli yetu. "
Mheshimiwa anaposema Bahati mbaya ana maana gani ? ........Huku ni kulea uzembe tuu, watu waliohusika walitakiwa kupelekwa Jela.
 
Mheshimiwa anaposema Bahati mbaya ana maana gani ? ........Huku ni kulea uzembe tuu, watu waliohusika walitakiwa kupelekwa Jela.
Mkuu, mimi hapo niliposikia BAHATI MBAYA nikajua huyu alomwandalia amedhani kawa smart sana; na eti wabunge wakafurahi na kupiga makofi kisa kasema "Tulichukua maamuzi mazito sana kusitisha ubia na mwekezaji huyu (RITES)"
 
Mhe. anasema hivi:
Mheshimiwa Spika,
Wakati Mfuko wa Akina Mama umekopesha zaidi ya wanawake 300,000, hadi Mei 2010 Mfuko wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ulikuwa umekopesha shilingi 45.2 bilioni na wajasiriamali 67,000 wamenufaika. Halmashauri za Wilaya 128 zimekopesha vijana jumla ya shilingi 1.16 bilioni kutoka Mfuko wa Maendeleo wa Vijana.

Mipango ya Serikali ya uendelezaji wa sekta binafsi, uwekezaji na uwezeshaji wananchi kiuchumi imewezesha shughuli za kiuchumi kupanuka na hivyo kuchochea ongezeko la ajira nchini. Hivyo, utekelezaji wa ahadi ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM kuhusu kuzalisha ajira milioni moja umeenda vizuri, kwani hadi kufikia mwezi Juni 2010, ajira 1,313,121 zilikuwa zimezalishwa nchini kote.
Kina mama gani hao wamenufaika hivyo? Hizi ajira pia nina wasiwasi sana, huenda kuna mtu anaweza kunifungua macho wakuu?

Nahisi hapa ndipo kwenye MABILIONI YA KIKWETE! Nachoka kabisa, maanake kuna watu wamenufaika na fedha hizi lakini mamilioni ya watanzania wakiendelea kuishi katika hali mbaya sana mijini na vijijini.
 
Jamani, kuna baadhi ambayo ameyaongea anadai yametekelezwa, na anavyosema mengine yapo njiani kutekelezwa (mpeni kura!) hivyo tuwe watu wa subira, itapendeza mtu akasoma juu ya mafanikio ya awamu ya nne kwenye attachment na kisha akachangia, naamini hapo ndipo tutakuja na hotuba mbadala ya hii ya mheshimiwa rais.

Nasubiri kwa hamu sana comments za comrade Malaria Sugu (MS)
Kauli hii ni matunda ya safari ya jana bungeni?
 
Kauli hii ni matunda ya safari ya jana bungeni?
Mkuu unaweza kufikiria zaidi ya hivi; achana na hoja zilizoshafungwa kabisa... Kama huwezi kusoma between the lines basi kumradhi tu
 
Wala si waziri aliyeyatamka maneno hayo bali ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa Jakaya Kikwete ndiye aliyetamka hivyo wakati akifunga Bunge la Muungano tar 16/07/10.

Nanukuu sehemu ya hotuba
;"Katika kipindi hiki pia tumepandisha kima cha chini cha mshahara ya watumishi wa umma kutoka shilingi 65,000 mpaka shilingi 135,000 sawa na ongezeko la asilimia 107".......Mwisho wa kunukuu.

Kama kumbukumbu zangu ziko sahihi kima cha chini cha mshahara kilikuwa sh. 104,000 kwa mwaka wa fedha wa 2009/2010. Hivyo basi serikali wameongeza mshahara kwa takribani sh. 31,000 (30%). Hiki natumai ndicho kiwango ambacho serikali iliwaahidi TUCTA kuwa itakitangaza kutokana na mashauriano waliyoyafanya.

Wafanyakazi sijui wachekelee au wanune kwa kuwa kima cha chini kilichotangazwa na serikali hakijafikia kile cha TUCTA hata kwa nusu yake?
 
mbona anaongelea mambo madogo madogo, ambayo hastahili kuyataja katika hotuba. kazi kweli kweli
 
Ahsante mhe rais kwa kuendelea kusimamia nchi yetu vizuri mpaka kuendelea kudumisha amani, utulivu na upendo wetu pamoja na kudumisha muungano wetu.

Ahsante kwa kuendeleza yale mazuri yaliyoachwa na viongozi waliotangulia na kuweza kuhimili vishindo vyote kutoka kwa watu na makundi mbalimbali na ahsante tena kwa kusamehe wale wote waliokukosea kwa namna moja au nyingine katika utendaji wako
Dah,

Shy bana... Ama kweli ukipenda kitu huwezi kuona ubaya wake. Hayo mekundu mkuu ni ya kumpongeza JK seriously?
mbona anaongelea mambo madogo madogo, ambayo hastahili kuyataja katika hotuba. kazi kweli kweli
Mkuu, wapo wanaoona kuwa ni MAKUBWA SANA haya na kuona kuwa RAIS kajitahidi kama unavyomwona mkuu Shy hapo juu!
 
Back
Top Bottom