Hotuba ya Rais Kikwete 30.6.2012

Hotuba ya Rais Kikwete 30.6.2012

Kwa uchumi niliosoma unaniaminisha mfanyakazi akilipwa mupesa nyingi hataweza kufanya kazi.....


Lakini wanapokea hela nyingiii, jamani????

Sasa nasubiri kugombea ubunge ili niwapite mshahara!!!!!!!
 
yani kikwete ana shida sana sana,ni muongo hakuna mfano ila ndo mtindo naona serikali imeamua "kujisafisha"mbele ya umaa,ilhali wao wanaenda kutibiwa india kwa fedha ya jasho letu!!
kweli hii ni vita kati ya serikali na wafanyakazi serikalini
 
2015 SIO MBALI

change will certainly come -
Uchunguzi ufanywe na watu waliofanya uhalifu - this is a joke - ama kweli HAKI INATOKA KWA MUNGU TU ......... duniani dhiki tupu!!!
 
Jamani hivi ni kwanini Serikali haitaki kusema kuwa "MADAKTARI WANADAI MAZINGIRA BORA YA KAZI NA SIO MISHAHARA NA POSHO" NIFEDHEHA KWA MKUU WA NCHI KUONGEA UONGO. Hii ni kupandikisha chuki kwa Wananchi dhidi ya Madaktari kuwa hawawajali wanajijali wenyewe hili jambo ni baya sana ukiliiangalia kwa undani ama kwa kina madhara yake ni makubwa.

JK na Serikali yako "DHAIFU" muache mara moja kupotosha UMMA kuhusu suala la MGOMO WA MADAKTARI

wewe ni punga.waajiri wewe ili uwalipe milioni saba na laki saba
 
yani kikwete ana shida sana sana,ni muongo hakuna mfano ila ndo mtindo naona serikali imeamua "kujisafisha"mbele ya umaa,ilhali wao wanaenda kutibiwa india kwa fedha ya jasho letu!!
kweli hii ni vita kati ya serikali na wafanyakazi serikalini

kama unaona serikali haikulipi unavotaka wewe anzisha NGO au mwambie baba yako akuajiri
 
katiba hii ya nchi rais ni dikteta ana mamlaka kubwa sana
 
[h=6]Kama una mgonjwa hosp na anateseka na kufa kipindi hiki basi huwezi kusaport huu mgomo wa madokta,isikie kwa mwenzio jmn,wagonjwa wanateseka(MUNGU IBARIKI TANZANIA,MUNGU IBARIKI AFRICA[/h]
 
Suala la madaktari naona Mkuu ameendeleza propanganda zilezile za kwamba kulikuwa na makubaliano. Makubaliano gani wakati mazungumzo yalikuwa hayajakamilika, hebu tuwekeeni haya makubaliano yakiwa na sahihi za pande zote mbili tuone.

Na JK ameendelea kuudanganya umma na kuufitinisha na madaktari kwa kuonyesha kuwa madaktari tatizo kubwa waling'ang'ania mshahari wa mil 3.5 wakati walikuwa wanajadiliana na kabla ya makubaliano serikali ikatangaza hizo 15% na labda sasa wanafikiri kuongeza mpaka 20% maana hii haikuwepo mwanzo. JK bila aibu anautangazia umma nyongeza ya posho ya kuchunguza maiti, dai ambalo halikuwepo kati ya yale waliyokuwa wanajadili.

JK acha kutishia nyau, hamuwezi kufukuza madaktari wote walioko kwenye mgomo, mnajidanganya, wasikilizeni madaktari na mfikie muafaka warudi kazini, kuendeleza vitisho na kuwakamata na kutesa viongozi wao haitawasidia.

Huduma gani zimeboreshwa kwenye hospitali za mikoa eti na sasa wanageukia wilayani, hii sio era ya kusema uongo na ukafikiri utapata watu. Ukifika mahospitalini sasa hivi hakuna dawa, hakuna vifaa tiba, hakuna watumishi. Hospitali eti zimepandishwa hadhi ya kuwa za rufaa zikiwa hazina madaktari bingwa, sasa nashangaa kama rufaa inatoka kwa MD inakwenda Kwa MD sijui itakuwa rufaa ya namna gani hiyo. Hospitali kuzitaja kwa uchache ni mfano hospitali ya mkoa wa rukwa ambayo ina bingwa mmoja tu ambaye ni surgeon nae yuko kwenye administration. JK usitupige changa la macho hakuna maboresho yoyote yalofanywe. Nchi imekushinda step down.

mkuu sio kwamba utashindwa kwenda Jamaica kubembea.Mnafiki Mkubwa dhaifu, TISS na mwanao ndio ulowatuma kumfanyia unyama Ulimboka, utalipa hapahapa duniani.

Mshashindwa mtabakia kutukana tu msimamo wa serikali ndo huo. Mimi nilikuwa nasupport madaktari lakini baada ya maelezo ya jana ya JK, nimewashusha thamani wote mlioanzisha upuuzi wa mgomo wa mara ya 3!
Jitihada zote za serikali za kuwasomesha bure na nyongeza kubwa ya mshahara na posho bado mnaendelea kudeka!
Big up sana JK...
 
Vp leo wameendelea kugoma au wameenda kusign kitabu then wananyuti kusikilizia reaction?
 
Madaktari hawa hawa ndio WEZI WAKUBWA wa madawa huko mahospitalini leo wanakuja kisenele nyuma kujifanya wanadai madawa hospitalini..naunga mkono hotuba nzima ya JK.
 
JK alitoa hotuba hiyo TBC1 ilimalizikia kabla ya taarifa ya Habari ya saa 2. Mie niliona akimalizia kusema suala la Dr. Ulimboka
 
Anasema serikali haihusiki na mateso ya Ulimboka,hata kichaa anaweza kugundua kuwa wanahusika moja kwa moja.
 
Anasema serikali haihusiki na mateso ya Ulimboka,hata kichaa anaweza kugundua kuwa wanahusika moja kwa moja.
Ulitegemea aseme pale kua Serikali yangu inahusika?
 
[h=6]NI UKWELI MTUPU.

JK hatuwezi kutoa ahadi za kuwalipa 7.7milion kwa mwezi maana uwezo huo hatuna.acheni kupotosha kauli hii bali jadilini na kuiboresha.[/h]
 
Kikwete hajazuia kitu ,mnyonge mnyongeni ,aliposema kuna tuhuma nyingi ,ikiwemo serikali kuwa ndio imehusika na mauaji ,sasa anaposema uchunguzi ufanywe ,alimaanisha kila anaetuhumiwaa achunguzwe ,wacheni uzezeta ,CCM itupotoshe na nyinyi weengine mnakuwaa hamna tofauti na CCM ,mnatupotosha.
 
kwa sasa hatuwezi kuwaahidi kuwa tunao
uwezo wa kuwalipa mshahara wa kuanzia wa
shilingi 3,500,000 na posho zote zile. Tukifanya
hivyo malipo ya daktari anayeanza kazi yatakuwa
shilingi 7,700,000. Kwa hakika kiasi hicho
hatutakiweza
 
Mods endelea kuchomoa post lakini ukweli tutaendelea kuusema; mgomo huu una shinikizo kutoka kwa upinzani hizi ni hujuma za wazi dhidi ya serikali. Tangu Mh. Raisi atoe hotuba ni takribani masaa 24 mbona jumuiya ya madaktari haiji na kukanusha yale yaliyosemwa na mh. Raisi? Bado tunauliza wizi wa vifaa na dawa kutoka kwenye hospitali za serikali ni nani wahusika wakubwa kama sio hawa hawa madaktari ambao leo hii wameshika bango wakidai vitendea kazi duni? Inakuwaje vifaa vinavyoharibika ni hospitali za serikali tu? Tunachowaomba madaktari wajiangalie miongoni mwao wasaliti ni wengi; wananchi tunasema liwalo na liwe kama noma acha iwe noma
If you dare to talk the truth then let the truth prevail other than that you will be a coward!!!!!!!!
Chama
Gongo la mboto DSM
 
[h=6]Baada Ya Hotuba Maswali Yafuatayo Yameibuka Akilini Mwangu;
1.kwanini Madaktar Walimng'ang'ania Ulimboka Awe Kiongoz Wao Ktk Mazungumzo Na serikal Wakat Si Mhanga Kama Wao?.
2.Kwanini Nae Ulimboka Alipenda Kuingilia Mgogoro Huu?
3.kwanini Timu ya usuluhish toka serikalin ilihofia uwepo wa ulimboka na ikamkataa lakin kikwete akaruhusu awepo tu?.
4.kama Serikal Ilifikia Makubaliano Aloyataja Kwanin Madokta Hawaridhik ? Nini Bado?
5.Wanaharakat Kina Nkya Na Wenzio Hiv Wanayajua Yotehayo? Kwanin Nao Wanawasapot Madokta ?.
???.[/h]
 
Rais jakaya kikwete amesema mshahara wanaotaka kulipwa madaktari haulipiki, na amewataka wajiondoe wasisubiri kufukuzwa. Gazeti la UHURU.
 
Back
Top Bottom