Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Kama ni kweli kikundi cha majambazi/wezi kiliweza kuingia kwenye hoteli yenye hadhi kubwa kama Nashera na kuweza kumuibia Naibu Waziri maswali mengi yameachwa juu ya hoteli hiyo. Maelezo yote ambayo yametolewa hadi hivi sasa yanaionesha hoteli kwenye mwanga mbaya zaidi kuliko hata Malima. Think about it. Nadhani Hoteli itabidi ijisafishe tu kwa kueleza vya ukweli kwani watu wengine mashuhuri wanaweza kuhofia sana kwenda hapo sasa...
Lakini pia inaonekana hoteli haina SOP za kuonesha wafanyakazi wanatakiwa washughulikie vipi matatizo ya wateja. Inawezekana Malima kaenda kuripoti wizi kwenye front desk (kitu ambacho pia kinashangaza kwani ningeassume angempigia moja kwa moja meneja wa hoteli) na wale vijana wa FD walipopiga simu kwa meneja wakati huo huo waka sms marafiki zao "aisee Malima kachapwa hapa". Maana nasikia taarifa za Malima kuibiwa zilikuwa zimeenea kwa watu wengi kabla hazijaandikwa magazetini for at least 24 hours.
Je, wafanyakazi wanapotoa taarifa za ndani kama hizo yawezekana ni kwa sababu hawajali ajira zao au hata taswira ya hoteli yao? au hawana hisia kuwa ni "hoteli yao"?
Lakini pia inaonekana hoteli haina SOP za kuonesha wafanyakazi wanatakiwa washughulikie vipi matatizo ya wateja. Inawezekana Malima kaenda kuripoti wizi kwenye front desk (kitu ambacho pia kinashangaza kwani ningeassume angempigia moja kwa moja meneja wa hoteli) na wale vijana wa FD walipopiga simu kwa meneja wakati huo huo waka sms marafiki zao "aisee Malima kachapwa hapa". Maana nasikia taarifa za Malima kuibiwa zilikuwa zimeenea kwa watu wengi kabla hazijaandikwa magazetini for at least 24 hours.
Je, wafanyakazi wanapotoa taarifa za ndani kama hizo yawezekana ni kwa sababu hawajali ajira zao au hata taswira ya hoteli yao? au hawana hisia kuwa ni "hoteli yao"?