hospitali ya kcmc kunani?

Injinia

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
849
26
Jamani, kama ninakosea nirekebishwe, lakini, hivi udaktari si kati ya fani za kuheshimika na hivyo ktk nchi nyingi madaktari ni watu ambao huwa na maslahi bora? Sasa iweje jamaa zangu madaktari kcmc wachoke hivyo? Nilitembelea Ms nikakuta wanaishi maisha yasiyoweza fananishwa na ya wenzao wa Muhimbili au Bugando ambako nako ni hospitali ya shirika la dini? Wanahemea mshahara mdogo ktk ngazi zote, ni aibu kutaja.. Ukiongea nao wamejawa malalamiko, hasa juu ya jinsi palivyogeuka sehemu ya miradi ya utafiti wa kimataifa wanayodai hainufaishi wafanyakazi bali uongozi wa juu!
 
1. KCMK sii iko chini ya Kanisa KKKT? Misingi ya Kanisa inahitaji mtu kutumika tu bila kuwa mlalamishi.. na Mungu hulipa rehema baadae!

2. Nadhani kuna matatizo ya Uongozi- na KKKT wamepata Askofu Mkuu Mpya na Prof. Shao yupo tu kwa mkataba..na mda wa kustaafu ulishapiat. Nadhani baada ya siku sii nyinyi huenda mambo yapabadilika!

3. Hivi ile sakati ya kuhamiswa wale madktari na ile kesi iliyofunguliwa mahakamani je haya yameishia wapi?
 
1. Prof Shayo (Shao?) inasemekana kaongezewa mkataba wa miaka 5, kwa uVice Chancellor wa Chuo, kaongezewa na askofu mpya, nasikia bodi itatangaza ijumaa km kaongezewa na upande wa hospitali.
2. Nadhani kuna viRichmond vidogo vinaendelea, na somebody should alert leadership ya kkkt
3. Kesi bado inaendelea ila jamaa alifanikiwa kugeuza kesi iwe vs. Shirika la Msamaria Mwema!
 
Ile Hosp. hata muonekano wake siyo kcmc tuliyoijua,
kwa kweli hata jengo limechakaa, vifaa kwa kuonekana tu vimechoka,
sembuse wafanyakazi wa humo ndani hali itakuwaje?
siyo ile kcmc ya Askofu Mkuu wa KKKT Mh. Stephano Ruben Moshi (R.I.P) katu.
 
Ile Hosp. hata muonekano wake siyo kcmc tuliyoijua,
kwa kweli hata jengo limechakaa, vifaa kwa kuonekana tu vimechoka,
sembuse wafanyakazi wa humo ndani hali itakuwaje?
siyo ile kcmc ya Askofu Mkuu wa KKKT Mh. Stephano Ruben Moshi (R.I.P) katu.

Haina mvuto kama ilivyokuaga ada yake ambayo hata mgonjwa unawezapelekwa na kutokana na uzuri wa mazingira na hata majengo hakika unapona

Nyakati hii ya uongozi mwingine yani choka mbaya kbs!
 
Haina mvuto kama ilivyokuaga ada yake ambayo hata mgonjwa unawezapelekwa na kutokana na uzuri wa mazingira na hata majengo hakika unapona

Nyakati hii ya uongozi mwingine yani choka mbaya kbs!

Ninikifanyike ili kuinusuru ??????

Je Tuhuma za Kiongozi aliyepita :-

Miaka 30 na iliyopita mtumishi wa Mungu Askofu Stephano Moshi wa KKKT alipata maono...Kilimanjaro Christian Medical Centre kwa kushirikiana na wengine akiwemo Prof Otto Walter hospitali hii mashuhuri na aina yake ikajengwa...ikakua.
Leo hii KCMC imekuwa makao ya mapepo na wachawi wenye uchu wa madaraka , mafisadi. Prof John Shao anainajisi KCMC ili kulinda cheo chake. Waganga wapiga ramli wanacheza na kuweka tunguli, kisa cheo!


Prof Shao amekuwa kiongozi hapa kwa zaidi ya miaka 10. Mwanzoni alifanya mema sasa hivi amenogewa hataki kuondoka...patamu pesa, wanawake, madaraka.
KCMC imekuwa danguro....viongozi kuzaa na watumishi...hakuna maadili tena. Waliokuwa wakisali kutwa kwa ajili KCMC wameondoka , wamestaafu...msarakambo
1. Prof Shao mwaka 2006 alifukuza kundi la madaktari bingwa waliohoji ukomo wa uongozi wake. Watu hawa wakiwemo Dr Ole, Prof Mlay...walijitolea muda kufundisha chuo cha madaktari na kuiweka KCMC ilipo.
kosa lao ..walihoji uongozi wa Shao kila mmoja ...alisambaratishwa..Mbeya rufaa mradi mabingwa walijikuta wakiwa njiani..

2. Kwa kushirikiana na watiifu wachache amekuwa akijipatia 10% toka kila mradi wa research.

3. TAKUKURU mwaka 2009 walifanya utafiti na kukuta uozo mkubwa katika ulaji wa mishahara ya serikali na forgery ya majina ya watumishi wanaolipwa na serikali. kwa mfano Dr Anna Mushi aliyeondoka siku nyingi KCMC eti hadi 2009 yuko kwenye payroll wengine hata marehemu.

4. Viongozi wa Wizara wanapolalamikiwa wakifika KCMC huzibwa midomo kwa pesa..

5. Viongozi wa kanisa nao wametumbukia kwenye mkumbo hupewa fedha nao hukaa kimya.

6. Wastaafu watumishi wa KCMC karibu wote wanalia na kusaga meno hakuna mfumo wa pensheni zao zimepotea.
7. Mwanae asiyejua kukamilisha sentensi ya kiingereza anapewa cheo cha u head wa IT, jamani muogopeni Mungu.

Prof Shao ni mungu mtu hakuna wa kumgusa si Ask Malasusa wala nani anaendesha KCMC anavyotaka.

Ndugu zangu tuiombee KCMC

Sasa baada ya kashfa ya TAKUKURU 2009...amefukuza madakatari wengine bingwa akiwa na wasiwasi nao...

Hii ndio KCMC ya vitisho, mambo ya giza, ubadhirifu wa pensehni n.k
 
Back
Top Bottom