Hongereni STRABAG! Dar Rapid Transit imefana mno!

Hongereni STRABAG! Dar Rapid Transit imefana mno!

Kweli mkuu barabara zimepunguzwa upana sana kiasi kwamba malori mawili kwenda sambamba kama ilivyokuwa zamani ni shida. Zamani ilikuwa magari makubwa na madogo yanaweza kwenda sambamba na kisha nafsi kubaki hata ya mwendesha baiskeli,pikipiki mtembea kwa miguu kupita lakini sasa ni shida. Labda kuwe na mpango wa kupunguza upana wa magari makubwa kama malori na mabasi

Copy and paste Mkuu, yaelekea kule ilimo patikana hii copy barabara haitymiwi na malori, kwa kuwa ni uwazi baadhi ya sehemu masemi trailer inabidi yawe yanasubiriana;mfano mzuri ni eneo kuelekea KIMARA mwisho na kupita daraja la kimara .
Kitu kingine yaonekana ilikochukuliwa copy ya barabara ni ukanda wa Tetemeko la ardhi, hebu angalia reinforcement ya vituuo vya abiria !
Huo mradi na Mkopo uliotumika kufanikisha mtazamo wangu ni uthibitishho tosha kuonyesha uzuzu wa watz ...
 
Shida kama uko maeneo ya kimara baruti unataka kurudi mbezi ni lazima uende hadi ubungo ndio upate njia ya kurudi

Tumia service road ama kwa kuingilia palepale baruti ili uje uingilie kwa Thomas au hadi Kibo...
 
Jamani wale wazazi 2etu wenye daladala na coaster wataxipeleka wapi ??? Maisha yatakuwaje ???
 
Kuna mapungufu kadhaa kwenye design ya Dar es Salaam Rapid Transit network:
(1) Barabara za lami ni nyembamba mno kiasi kwamba nafasi kati ya gari na gari ni ndogo sana (inch 18).
(2) Kuna baadhi ya sehemu njia ya gari za kawaida imeingiliana na njia ya gari za mwendo kasi (kuanzia Kibo hadi Kimara) na hii imesha sababisha ajali na vifoo kadhaa hadi sasa.
(3) Barabara zimewekewa kinga za kuzuia kuingia au kutoka hadi maeneo maalumu ya matoleo na hivyo kukitokea ajali msongamano unaotokea unakuwa ni tabu kuupunguza haraka
(4) Kule mwishoni Kimara njia ina kona balaa mfano wa herufi S na imeshasababisha ajali kadhaa hasa kwa magari makubwa kupitiliza na kuanguka
(5) na kadhalilka na kadhalilka......
nitaongezea baadaye!!
 
Kuna mapungufu kadhaa kwenye design ya Dar es Salaam Rapid Transit network:
(1) Barabara za lami ni nyembamba mno kiasi kwamba nafasi kati ya gari na gari ni ndogo sana (inch 18).
(2) Kuna baadhi ya sehemu njia ya gari za kawaida imeingiliana na njia ya gari za mwendo kasi (kuanzia Kibo hadi Kimara) na hii imesha sababisha ajali na vifoo kadhaa hadi sasa.
(3) Barabara zimewekewa kinga za kuzuia kuingia au kutoka hadi maeneo maalumu ya matoleo na hivyo kukitokea ajali msongamano unaotokea unakuwa ni tabu kuupunguza haraka
(4) Kule mwishoni Kimara njia ina kona balaa mfano wa herufi S na imeshasababisha ajali kadhaa hasa kwa magari makubwa kupitiliza na kuanguka
(5) na kadhalilka na kadhalilka......
nitaongezea baadaye!!
Ni uendeshaji mbovu wa madereva,ukiendesha bila kufuata sheria za barabarani,ajali ni lazima ikutokee.
 
Shida kama uko maeneo ya kimara baruti unataka kurudi mbezi ni lazima uende hadi ubungo ndio upate njia ya kurudi

Na ukishatoka ubungo mataa, ukashindwa ku-U- turn SHEKILANGO, safari yk inakuhusu MWEMBECHAI!
 
Umeona eeh!? Yani tuko radhi tulaumu barabara kuwa na kona kabla ya kujiuliza kama mwendo tunaoendeshaga unafaa. Kama vile tumesahau kuwa ukiendesha gari kasi na polepole pia waweza. Barabara zinachorwa kwa umakini ukiona kona inakushinda jua unendesha kasi ambayo haistahili kwenye hiyo barabara.
 
Sijaona uboreshaji wowote wa maana ni kinyumenyume tu, kwanza vituo kujengwa katikati ya barabara tena vikubwa kama maghala ya kuhifadhia mahindi, pili barabara nyembamba ambayo itawaharimu tena baada ya muda mfupi tu watasema ipanuliwe awe kama ulikua ni mpango wa makusudi ili bajeti nyengine ije itengewe tena pesa.

Hata jana tulisikia serikali imetenga bil2 kwa mpango wa kupunguza foleni ni kweli iko siku tutegemee mipango hi ya 10pacent itakwisha ili tujenge mambo ya maana kwa karne japo moja bila ya barabara kutiwa viraka au kupanuliwa?
 
Wamezifanya nyembamba ili usiendeshe kwa kasi na kusababisha ajali.
 

kadoda11 huku umeniita ila naona ni malalamiko ya Wabongo, kama nilivyosema siku fulani design ya hiyo BRT ina walakini na mapungufu. Fuatilia mjadala kwanza kabla hujaniita. Kwanza hebu leo nakupa mtihani endesha gari pita Ubungo ukielekea Kimara, angalia kama utaona U-turn.
 
Last edited by a moderator:
Naomba kujuzwa, barabara za DART zitakuwa na hizi daladala za kawaida tena?
Nauliza hivi coz nilikuwa na argument na rafiki yangu, tulipita njia hiyo lakini sikuona bus stops za kawaida, aside zile za mabasi ya mwendo kasi, ndio maana nauliza, daladala za "kimara-k.koo, kimara-posta, kimara-mwenge'' zitatumia njia hiyo?

Swali zuri mkuu! Kwa ufupi huu mradi ukikamilika hizi bus za kawaida Kimara-Posta hazitokuwepo tena na inabidi owners wafanye mpango wa kubadilisha route zao, wazipeleke kule tu ambapo hakujafikiwa na mradi, kwa mfano toka Kimara mwisho kwenda Kibamba au Kibaha, au labda Gongolamboto/Mbagala-Kariakoo. Natumai nimejaribu kukujibu.
 
kuna makutano ya shekilango, wamepabana sana, pia magomen mapipa, magar yanayotaka kwenda mzimun au kuingia main road, ni tatizo.
 
Kuna mapungufu kadhaa kwenye design ya Dar es Salaam Rapid Transit network:
(1) Barabara za lami ni nyembamba mno kiasi kwamba nafasi kati ya gari na gari ni ndogo sana (inch 18).
(2) Kuna baadhi ya sehemu njia ya gari za kawaida imeingiliana na njia ya gari za mwendo kasi (kuanzia Kibo hadi Kimara) na hii imesha sababisha ajali na vifoo kadhaa hadi sasa.
(3) Barabara zimewekewa kinga za kuzuia kuingia au kutoka hadi maeneo maalumu ya matoleo na hivyo kukitokea ajali msongamano unaotokea unakuwa ni tabu kuupunguza haraka
(4) Kule mwishoni Kimara njia ina kona balaa mfano wa herufi S na imeshasababisha ajali kadhaa hasa kwa magari makubwa kupitiliza na kuanguka
(5) na kadhalilka na kadhalilka......
nitaongezea baadaye!!
Na. 1 Nafikiri serikali inampango wa kuzifanya barabara hizo kuwa za magari madogo tu mwisho size ya coater au canter vinginevyo hizi nguzo za taa zitapigwa chini zote kwani nazo zipo karibu sana na barabara ukizidiwa cha kwanza ni kuzitandika hizo nguzo. Mbona ile ya Sam Nu Joma Iko fresh na nguvu za taa mpaka uzifuate zilipo basi wewe unakuwa na lako jambo. Barabara pana na ni ya kujimwaga na ndio maana ni nadra sana kukuta ajali za kupigana pasi au nyingine katika barabara ile labda dereva awe wa viroba na bangi

Na 2 huwa inachanganya sana mwishowe unajikuta umpanda ile pavement ya kutenganisha na kuiweka katikati ya uvungu wa gari ambapo magari mengi nimeshuhudia yakiharibika sana uvunguni na mengine kufa kabisa kwasababu ya madhara ya tuta linalotenganisha barabara ya lami na basi

Hiyo Na. 4 hata mimi huwa inanishangaza ni kwanini waliamua kuweka kona wakati nafasi ya kufanya barabara inyooke ipo. Labda wamefanya hivyo ili kuwapa mazoezi ya kona za kitonga madereva ambao wanajiandaa kwenda Iringa Mbeya na Zambia
 
Copy and paste Mkuu, yaelekea kule ilimo patikana hii copy barabara haitymiwi na malori, kwa kuwa ni uwazi baadhi ya sehemu masemi trailer inabidi yawe yanasubiriana;mfano mzuri ni eneo kuelekea KIMARA mwisho na kupita daraja la kimara .
Kitu kingine yaonekana ilikochukuliwa copy ya barabara ni ukanda wa Tetemeko la ardhi, hebu angalia reinforcement ya vituuo vya abiria !
Huo mradi na Mkopo uliotumika kufanikisha mtazamo wangu ni uthibitishho tosha kuonyesha uzuzu wa watz ...

Kweli mkuu yale mavituo ukisema uyavunje gharama yake itakuwa kubwa kuliko ya kujenga. Nadhani yatahitaji bomu la nyukilia. Yaani reinforcement kama ile ingetumika kwenye shule za kata ingekuwa poa sana. Lakini ukipita sasa kwenye shule ya kata iliyojengwa miaka 2 iliyopita utadhani ilijengwa kabla ya vita kuu ya kwanza ya dunia. Sakafu ukiwa na kilo nyingi inatitia, kuta nyufa za kuka mijusi na nyoka, mapaa ndio yameshaoza. Lakini ukienda kwenye shule tulizotaifisha zilizojengwa na wakoloni zipo ngangali utadhani zimejengwa mwaka jana tatizo ni uchakabu wa rangi na matumizi mabaya ya miundo mbinu.
 
Na ukishatoka ubungo mataa, ukashindwa ku-U- turn SHEKILANGO, safari yk inakuhusu MWEMBECHAI!

mkuu unaweza kukatia pale soko la big brother Kuna u turn pale
 
Foleni itakuwa pale pale kwani naona barabara bado ni finyu mno. Anyways kujuwa ubora wake ngoja tusubiri mvua zetu hizi tuone kama ni lami kweli au ni disel imepakwa kwenye moram. Bongo hii kwa usanii nafikiri tunaongoza duniani tukifuatiwa na wachina.
Ukiacha ufinyu wa barabara! Shida nyingine ni pale watakaposhuka kwenye mabasi na kutaka kuvuka ili waingie pembeni mwa barabara! Magari katika barabara za kawaida yatalazimika kusimama mara kwa mara karibia kila kituo! Hapo ndo watatengeneza foleni za kufa mtu! Magari yatakuwa hayatembei kabisa!
 
Back
Top Bottom