The Priest
JF-Expert Member
- Dec 8, 2010
- 1,029
- 258
Shida kama uko maeneo ya kimara baruti unataka kurudi mbezi ni lazima uende hadi ubungo ndio upate njia ya kurudi
Ngoja tuone na ile ya mchina banana to chamazi
Naomba kujuzwa, barabara za DART zitakuwa na hizi daladala za kawaida tena?
Nauliza hivi coz nilikuwa na argument na rafiki yangu, tulipita njia hiyo lakini sikuona bus stops za kawaida, aside zile za mabasi ya mwendo kasi, ndio maana nauliza, daladala za "kimara-k.koo, kimara-posta, kimara-mwenge'' zitatumia njia hiyo?
Itakapokamilika, njia hiyo haitakuwa na daladala, ni mabasi ya mradi tu.
Kweli mkuu barabara zimepunguzwa upana sana kiasi kwamba malori mawili kwenda sambamba kama ilivyokuwa zamani ni shida. Zamani ilikuwa magari makubwa na madogo yanaweza kwenda sambamba na kisha nafsi kubaki hata ya mwendesha baiskeli,pikipiki mtembea kwa miguu kupita lakini sasa ni shida. Labda kuwe na mpango wa kupunguza upana wa magari makubwa kama malori na mabasi
Foleni itakuwa pale pale kwani naona barabara bado ni finyu mno. Anyways kujuwa ubora wake ngoja tusubiri mvua zetu hizi tuone kama ni lami kweli au ni disel imepakwa kwenye moram. Bongo hii kwa usanii nafikiri tunaongoza duniani tukifuatiwa na wachina.
Miradi mingi inayo fanywa na serikali ya ccm ni ya kukurupukia haina ubunifu wowote hovyo kabisa hawa watu.
Project hii inaanza lini mkuu!?
Project hii inaanza lini mkuu!?
Wamepunguza sana upana wa barabara kama kiasi kwamba tutapigana pasi sana na tukijitahidi kukwepana tutakuwa tunazitandika zile nguzo za taa barabarani na si dhani kama zitasalimika zile. Boda boda wajiandae kwa kiama zaidi hasa inapotokea wanakatiza katikati ya magari kwani nafasi haitoshi hivyo wataishia mivunguni mwa magari kwa haraka zao maana wao wanataka kupita sehemu yoyote na wakati wowote. Hata hizo barabara za katikati za mabasi ni finyu sana kama dereva ni mtu wa kupepesa macho pembeni atajikuta ameparamia pavement blocks na kuhamia upande wa barabara za raia ambako nako ni kufinyu. Solution ni kuamua kuwa barabara hizi zitumike na vigari vidogo tu mwisho size ya coaster na canter. Milori na mibasi iishie nje ya mji kwani kwa ukubwa wao moja tu linatosha barabara yote na usiombe liwe na trailer ndio balaa! Na likiharibika barabarani ndio shida kubwa!Hii barabara ni rafiki kwa mabasi ya mwendo kasi tu lakini kwa watumiaji wengine ni shida! Ajali nje nje kwa wanaovuka popote isipokuwa vituoni tu, na kupigana pasi za hapa na pale.
Mimi kinachoniuma ni kitendo cha sisi wenyewe kutokuwa wastaarabu afu tunasingizia ubora si mzuri. Jamani watu wanatupa taka hovyo magari yanavyo overtake ni shida yaani mtu hatumiii hata akili ya kawaida tu kwamba hii barabara imekuwa nyembamba kwa hiyo hata uendeshaji inabidi uwe makini ili usiharibu miundo mbinu na chombo chako niko against na serikali kwa mambo mengi lakini kuna mengine tunawaonea tu. nimekuwa nikifatilia hata stand ya hapa mbezi asubuhi huwa inafagiwa ukipita hadi unafurahia subiri baada ya masaa 3. Na vyombo vya kuhifadhia taka pale vipo kabisa lakini utakuta uchafu hadi inasikitisha. Kuna mambo tuache kulalamika kabisa mtu akikutengenezea kitu wewe ukaki haribu kwa matumizi ya hovyo hata kingekuwa kitu imara au chenye ubora wa vipi kitaharibika tu kabla ya wakati wake tunapaswa kubadilika
Barabara ni nyembamba sana. Haifai kabisa. Kupigana pasi hapo kawaida.
Huo wembamba ni tatizo, na ndio hapo inatakiwa madereva wabadilike vichwani mwao. Tumezoea kuendesha kibabe sana ndiyo maana hata kabla watu kupigana pasi ilikuwa kawaida. Madereva wakiwa wastaarabu ninao uhakika kabisa hakuna atakayepiga wala kupigwa pasi. Wasiwasi wangu ni je, huo ustaarabu utapatikana kweli? Maana kila mtu ni mjanja, lazima aendeshe kwa kasi, mbwembwe na maringo ili aonekane anafahamu. Katikati ya mji unataka kuendesha kama uko highway. Kwenye zebra crossing unapita tu bila kupunguza hata mwendo uangalie kama kuna watu wanataka kuvuka, kwanza ndio unapiga honi kubwa hadi wenye matatizo ya moyo wanataka kuanguka wakati pale ni haki yao kuvuka, kama wapo inatakiwa uwasubiri.
Mimi naona hapa tusilaumu sana wembamba wa barabara, ni sisi wenyewe madereva aidha kwa sababu ya haraka zetu zisizokuwa na sababu ya msingi, au kwa kuwa wengine hata kuendesha kwenyewe hatujui. Kifupi matatizo zaidi yatatokana na kukosa ustaarabu kuliko wembamba/ufinyu wa barabara kwa vile tu tutataka kuendesha kama tunaenda Mbeya!
Tujipange kubadilika.