princess13
Senior Member
- Aug 30, 2018
- 100
- 112
Safi sana,Arusha ifuate mfano sasa manake hakufai
Pongezi nyingi kwa mtukufu Rais wetu mama yetu kwa kuwaondoa wamachinga maeneo yasiyo rasmi. Hapo je?Hivi ni mkuu wa mkoa au ni boss wao ndiye wa kumpongeza?
Kwa hili nampongeza sana Mheshimiwa Makala. Jiji lazima liende na hadhi yake.Naomba niungane na wana DSM wengine kumpongeza mkuu mkoa kwakweli umeweza unastahili nishani na pongezi ilikuwa sio kazi nyepesi kurudisha jiji katika hali yake baada jiji kuwa ovyo kabisa.
Sasa Dar inawaka Manzese leo unaangusha sindano unaiona kongole kwa timu nzima ya mkoa.
Ila ushauri muwashirikishe ngazi ya chini kama wenyeviti Serikali za Mitaa ili kusimamia kila mtaa wake vibanda visirejee tena maana watanzania tuna mambo ya kujaribu jaribu ataanza mmoja tu wengine wakiona kimya wanarudi kama mwanzo.
Hongera sana RC Makalla
Wako
Mwanadar es salaam
Kaishawapa 5 bilioniTo be honest, nilimbeza Makalla, nilisema hataweza kuondoa wamachinga, smenishangaza kwani zoezi limefanyika kwa amani na upendo na jiji limependeza.
Ushauri wangu;
1. Makalla awaite aongee nao watoe madukuduku yao ili kupunguza mukari usijelipuka baadae..na awasikilize changamoto mpya.
2. Samia naye aitikie wito wao na kukaa nao kama wanawe, awatiw moyo kuvumilia makazi mapya na aahidi kuwasaidia, hapo atawaweza
Sasa, kama kweli tumedhamiria kutakatisha jiji, na wenye fremu/maduka wapigwe marufuku kusambaza vitu nje ya fremu zao. Kwanza, ni mbaya kiafya. Bidhaa zao nyingi ni zile haziendani na mwanga wa moja kwa moja wa jua (huandikwa, store in a cool dry place). Kuziweka nje ni kuhatarisha maisha ya watumiaji/wateja. Pili, kutaleta muonekano mzuri wa hizo barabara. Wengi wanateka hadi sehemi za kupita.
Kupiga marufuku, kutaonesha wazi zoezi halijalenga kuumiza kundi fulani bali mmedhamiria kurudisha hadhi ya jiji.