Hongera Maulid Kitenge

Hongera Maulid Kitenge

Siku ya leo kumetokea tukio la kustaajabisha ktk tasnia ya siasa nchini tanzania. Tukio hilo limetokea dar es salaam wakati aliyekuwa waziri wa michezo na tamaduni Nape nauye akitaka kuongea na waandishi wa habari baada ya kuondolewa katika nafasi yake ya uwaziri. Nape ameondelewa leo hii katika nafasi yake baada ya mh rais kufanya marekebisho madogo katika wizara mbili.

Baada ya mh Nape kuwasili maeneo ya Pritoria hotel kulitokea tafrani baada ya watu walitambuliwa kuwa ni maafisa usalama kumzuia asiongee na waandishi na kumtaka arudi ndani ya gari. Wakati sakata hilo likitokea mmoja wa maafisa usalama alitoa bastola na kumtishia Mh Nape ambaye naye hakustuka . Afisa huyo aliirudisha silaha hiyo kiunoni kisha kuanza kumsukuma Mh nape kumrudisha ndani ya gari. Pasipo kutarajiwa kijana mmoja mtanashati aliyevaa koti jekundu alionekana kujongea kujua kinachoendelea baada ya kuona tafrani ikitokea.

Kijana huyo aliweza kutambuliwa kuwa ni mtangazaji maarufu Maulid Kitenge. Kijana huyoo aliweza kuingilia kati na kumtoa afisa usalama kwa nguvu eneo la tukio huku akimsukuma bila kuogopa. Hakika alifanikiwa akamuondoa eneo hilo na afisa huyo alitii bila shurti. Wengi tumeona na kustaajabu na hatuna budi kumpa hongera maulidi kitenge kwa ujasiri aliouonesha.

ILA
Nimejaribu kujiuliza kwa hali ya kawaida kuna raia wa kawaida anaweza kuwa na ujasiri wa namna hiyoo. Nikapata jibu inawezekana na yeye ni wale watu wanaovaa suti nyeusi(mashushu).mpaka sasa bado sijapata jibu sahihi .

Waungwana ninyi mnaonaje nawasilishaView attachment 485865View attachment 485866View attachment 485867View attachment 485868
 
Maulidi pokea 5 uko vizuri nendelea kutetea haki. Achana na Bashite na Pombe wanaovuruga ukweli. Pombe sijui karogwa au kiti ndo kinampeleka motoni
 
Kitenge ni Muhuni wa Alharamain Secondary School , usikute alishapasha cha Shaurimoyo kabla ya kwenda kwny press conference halafu Ana hasira sana na aliefoji vyeti na majina
Hapana wala c muhuni ila kuna watu huwa wakichoka husema liwalo na liwe kama kufa wacha na iwe ikifikia hapo ni hatari sana na ndiko tunakoelekea.
 
Me nasema iv izi bastola walivyo ziacha acha njee maana namuona na uyu mwenye shati nyeupe nae bastola inachungulia kiunoni je angetokea mtu mwenye akili ndogo akawachomolea pale nakuanza kufyatua ovyo ingekuwaje
Yaani kama hawa ni wana usalama wamefanya makosa mengi sana Leo na ni wana usalama uchwara over
 
Kama Yule Jamaa wa bastora ni usalama basi tunataizo kubwa mahari

Usalama anataka kuua mbele ya waandishi wa habari.

Aliyewatuma kawadanganya nchi inatawaliwa kijeshi?

Jamaani mnaoongoza nchi wananchi Hatutaki Madhaifu mnayotuonesha wazi.

Nape tu mnatumia bastora, akija Al shabab mtaita vifaru?

Shame kwa aliye mfunza
 
Maulidi ni wakumwangalia jicho la5 nasikia anamwambia uyu usalama wa taifa uchwara utaaribu mambo uku anamsukuma na yy kawa mdogo kweli uyu jamaaa mmmm yaweza kuwa nae ni ......
maulid ni mtoto wa mjini anajua namna ya kutuliza boli, kitenge alichofanya ni kumsukumiza jamaa hadi kwenye gari la rpc jamaa kugeuka kamwona boss ikabidi awe mpole
 
Ngoja niendelee kuunganisha dot ntamjua tuu huyu kitenge ..hili ni tukio la pili namshuhudia akiwa katika shughuli hizi za kusema utaharibu mambo..lakini kwa maneno mengine ...Ingawa kama nini majibu yangu mfukoni tayari ivi
 
Kama Yule Jamaa wa bastora ni usalama basi tunataizo kubwa mahari

Usalama anataka kuua mbele ya waandishi wa habari.

Aliyewatuma kawadanganya nchi inatawaliwa kijeshi?

Jamaani mnaoongoza nchi wananchi Hatutaki Madhaifu mnayotuonesha wazi.

Nape tu mnatumia bastora, akija Al shabab mtaita vifaru?

Shame kwa aliye mfunza
Narudia tena kuna hatua kifikia mtu amechoka kuonewa au ameona mtu anaonewa roho ya huruma humwijia na akawa tayari kukubali lolote liwalo na liwe hapo roho hujaa sumu mbaya ya kuyakubali mauti na ndipo shida huanzia hapo akili ya uoga hupotea na ndipo yanapotokeza hayo ya kina maulid kitenge na kwa ss tunakoelekea kutokana na sheria zinavyovurugwa tusubiri lkn iko siku tutatafuta aman na hatutaipa
 
Hapo Maulid nilimkubali kishenz yaan, jamaa hakuwa mwoga kabsa.

Ila mdogo wangu Harmo rapper alilula kona ni hatari. Alipata kiboko yake pale
Ha ha ha ha ha ha ha haaaah, mjomba, mbele ya bereta lazima uingie ndichi tu
 
Vijana msipongeze tu ilazingatieni mazoezi. Maulid kitenge huwa anapasha na team yake ya efm asubuhi.
 
Back
Top Bottom