Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 13,226
- 26,048
Nianze kwa kukupa pongezi kwa ushindi wako. Umeliwakilisha vyema taifa. Hongera sana
Nimeangalia ulivyojinadi. Kusema kweli umeonesha uwezo wako kama mwanamke mahiri.
Ujumbe wangu kwako Dkt Tulia- Jijenge vizuri kimataifa, jijenge vizuri kuijua Dunia na Siasa zake. Jipe muda kujifunza sana na kwa kila unalojifunza jifunze pia namna ya kulifanyia utekelezaji.
Ujumbe wangu kwa Rais Samia- Naona umemuona Tulia. Najua hata faili lake unaweza kulipata na kulipitia. Kusema kweli mwanamke mwenzako anaweza. Mjenge vizuri, mpe exposure, mjenge aendeleze haya mazuri yote unayoyafanya sana hasa katika kujenga uchumi imara kupitia sekta binafsi pale utakapomaliza uongozi wako. Mpe exposure apate kujifunza vizuri geopolitics. Na mwisho ikikupendeza chama chako kimpe kijiti akapeperushe bendera ya chama 2030.
Kwa CCM- Najua coming 2030 kuna Mwigulu na Makamba. Najua wamejijenga sana na wanajijenga sana. Ila muangalieni vizuri Dkt. Tulia. Mjengeni kichama na kimataifa. Aijue Dunia na siasa zake ili ajifunze kipi tunatakiwa kukifanya kuendana na kasi dunia inayoenda. Msimfundishe udiktekta bali kutumia akili, busara na maarifa kama anavyofanya Rais Samia. Nchi inahitaji consistence ili ipate maendeleo ya kweli.
Mjengeni Tulia afanye haya mazuri anayoyafanya Samia ili kuwe na consistence na mwisho tuwe nchi ya maziwa na asali. Tusirudi tena nyuma.
Kwa wana Mbeya- Mmemuona Tulia. Anaweza na kweli anaweza. Kikubwa mleeni awe kiongozi bora. Mpeni ushirikiano na jifunzeni kulingia watu wenu wenye mafanikio kwa kuwa mafanikio ya watu wenu ni mafanikio yenu. Mbeya ni jiji lenye hali nzuri ya hewa nadhani kuliko mikoa yote hapa Tanzania ila mnahitaji viongozi wazuri muijenge vizuri mbeya yenu. Mmepata Tulia mtumieni vizuri.
Asanteni
Lord Denning
Kigali
Nimeangalia ulivyojinadi. Kusema kweli umeonesha uwezo wako kama mwanamke mahiri.
Ujumbe wangu kwako Dkt Tulia- Jijenge vizuri kimataifa, jijenge vizuri kuijua Dunia na Siasa zake. Jipe muda kujifunza sana na kwa kila unalojifunza jifunze pia namna ya kulifanyia utekelezaji.
Ujumbe wangu kwa Rais Samia- Naona umemuona Tulia. Najua hata faili lake unaweza kulipata na kulipitia. Kusema kweli mwanamke mwenzako anaweza. Mjenge vizuri, mpe exposure, mjenge aendeleze haya mazuri yote unayoyafanya sana hasa katika kujenga uchumi imara kupitia sekta binafsi pale utakapomaliza uongozi wako. Mpe exposure apate kujifunza vizuri geopolitics. Na mwisho ikikupendeza chama chako kimpe kijiti akapeperushe bendera ya chama 2030.
Kwa CCM- Najua coming 2030 kuna Mwigulu na Makamba. Najua wamejijenga sana na wanajijenga sana. Ila muangalieni vizuri Dkt. Tulia. Mjengeni kichama na kimataifa. Aijue Dunia na siasa zake ili ajifunze kipi tunatakiwa kukifanya kuendana na kasi dunia inayoenda. Msimfundishe udiktekta bali kutumia akili, busara na maarifa kama anavyofanya Rais Samia. Nchi inahitaji consistence ili ipate maendeleo ya kweli.
Mjengeni Tulia afanye haya mazuri anayoyafanya Samia ili kuwe na consistence na mwisho tuwe nchi ya maziwa na asali. Tusirudi tena nyuma.
Kwa wana Mbeya- Mmemuona Tulia. Anaweza na kweli anaweza. Kikubwa mleeni awe kiongozi bora. Mpeni ushirikiano na jifunzeni kulingia watu wenu wenye mafanikio kwa kuwa mafanikio ya watu wenu ni mafanikio yenu. Mbeya ni jiji lenye hali nzuri ya hewa nadhani kuliko mikoa yote hapa Tanzania ila mnahitaji viongozi wazuri muijenge vizuri mbeya yenu. Mmepata Tulia mtumieni vizuri.
Asanteni
Lord Denning
Kigali