Hongera Aslay: Mkurugenzi wa USAID nchini anakuzimia

Kaka Pekee

JF-Expert Member
Apr 3, 2018
336
559
Bwana mdogo wangu Aslay, ni wazi kuwa unajitahidi sana kufanya kazi nzuri kimuziki na unashika nafasi mbalimbali za music chat hapa nchini.

Tungo zako na Matumizi ya sauti yako yanaonyesha ni jinsi gani unazidi kukomaa kmuziki ingawa inabidi ufanye mazoezi ya ziada way too far kwenye live performance sababu kwenye Valentine ulizingua kwa kweli ( Kutawala Jukwaa) ubunifu zaidi unahitajika.

Katika ziara yake hapa Mkoani Mbeya Mkurugenzi mkazi wa Usaid Bw. Andy Karas (Huyu ni boss wa USAID nchini- Mmarekani aliyeishi miaka mingi Afrika) nilimuuliza ni mwanamuziki yupi anayempenda nchini...Jibu lake likawa kwa Muziki wa Kale anampenda Remmy Ongala Sura mbaya, Marijani Rajab, na wengine wakongwe wa kale.....Kwa upande wa Muziki wa sasa hakuwa na list kubwa zaidi ya kutaja jina lako “ Muziki wa sasa ninamkubali Mwanamuziki anaitwa ASLAY” basi.

Sasa mdogo wangu Hiyo ni fursa sababu USAID wana miradi mingi ya kimaendeleo nchini. Kuna mradi wa Boresha Afya, Boresha Habari, Tusome Pamoja nk. Hebu fanya kama unatembelea Ubalozi wa marekani pale Msasani Dar es Salaam Uombe kuonana na huyu Mzee wa kimarekani, huenda ukapata zali la kuwa Balozi wa USAID kwa mradi mmoja wapo ukala shavu zaidi mdogo wangu.

Hiyo ni fursa mimekupa kwa kukung’ata sikio kidogo Kazi kwako.
 
Halafu akienda anaanzaje? Lemme guess (in Aslay's voice) "Sir/Madam, I read somewhere that you love my music... thank you Sir, that's why I came to visit you!"

Ebo!

Kama umekusudia kumpa mchongo, nusa nusa hapo USAID ufahamu kwa sasa kuna project gani inahitaji public awareness ili aitungie wimbo na kwenda pale akiwa na DVD mkononi ya kuhamasisha suala husika!
 
Halafu akienda anaanzaje? Lemme guess (in Aslay's voice) "Sir/Madam, I read somewhere that you love my music... thank you Sir, that's why I came to visit you!"

Ebo!

Kama umekusudia kumpa mchongo, nusa nusa hapo USAID ufahamu kwa sasa kuna project gani inahitaji public awareness ili aitungie wimbo na kwenda pale akiwa na DVD mkononi ya kuhamasisha suala husika!
nimekupenda Bure
 
Halafu akienda anaanzaje? Lemme guess (in Aslay's voice) "Sir/Madam, I read somewhere that you love my music... thank you Sir, that's why I came to visit you!"

Ebo!

Kama umekusudia kumpa mchongo, nusa nusa hapo USAID ufahamu kwa sasa kuna project gani inahitaji public awareness ili aitungie wimbo na kwenda pale akiwa na DVD mkononi ya kuhamasisha suala husika!
Hii ndio sababu ya sisi watanzania kutoendelea...tukiwa na mawazo hasi mbele ya kila kitu, Anyway hata Kuwaandikia Email pia ni jambo jema, hii niliyotoa hapa si habari ya Kiuzushi hata kidogo. So anaweza pia kuomba yeye kuwa balozi wa Mradi mmoja wapo Mf. **** mradi wa Tusome pamoja kwa shule za msingi Nchini, Boresha Habari, Boresha Afya...Fanya research kuhusu miradi hiyo mtandaoni au kwenye tovuti yao utaielewa vizuri.

Kuna wakati inabidi kuweka pembeni umaarufu na kujishusha na kujiongeza kidogo.
Wanamuziki wapya kila siku wanakuja, so ni wakati wake ikibidi...ama la atakuja mwingine akala shavu halafu ikawa si rizki yake tena.
 
Halafu akienda anaanzaje? Lemme guess (in Aslay's voice) "Sir/Madam, I read somewhere that you love my music... thank you Sir, that's why I came to visit you!"

Ebo!

Kama umekusudia kumpa mchongo, nusa nusa hapo USAID ufahamu kwa sasa kuna project gani inahitaji public awareness ili aitungie wimbo na kwenda pale akiwa na DVD mkononi ya kuhamasisha suala husika!
...Halafu kitu kingine aisee Huyo Mkurugenzi anaongea kiswahili cha kizaramo kabisa...kwa hiyo Bwana Aslay asiwe na mashaka kabisa ya Mawasiliano akiamua kumcheki....hii ni kama tu ana kidhungu chetu cha 'Ai amu Coming zea zea, au Katelephone donti smoki my riva'. ila naamini mdogo wangu yuko vizuri kapiga hata ka English kozi mchikichini.
 
Mungu ndiye mpangaji wa Kila jambo
kabisa buji, ila tukumbuke na lile neno la ombeni nami nitawapa...Allah maanani hawezi kutuletea Ugali nyumbani, Tuutafute kwa jasho huku tukimuomba yeye kutufungulia njia na maarifa zaidi,
 
...Halafu kitu kingine aisee Huyu Mkurugenzi anaongea kiswahili cha kizaramo kabisa...kwa hiyo Bwana Aslay asiwe na mashaka kabisa ya Mawasiliano akiamua kumcheki....hii ni kama tu ana kidhungu chetu cha 'Ai amu Coming zea zea, au Katelephone donti smoki my riva'. ila naamini mdogo wangu yuko vizuri kapiga hata ka English kozi mchikichini.
Wengi wao wanaoa Wandengeleko vile viuno si mchezo, sasa mama wa Kindengeleko utaanzia wapi kumuita honey?
 
Hebu Picha/sauti Ya Huyo Balozi Mwenyewe!
Isijekuwa Jina La Kidhungu Kumbe Mwenyewe Mzaramo Wa Msanga
 
I think hayo ni mapenz yake mkurugenzi yeye binafsi na ni upande wa starehe na burudani zake ambapo sion uhusiano na kazi zake hapo USAID. Nafikiri jambo la msingi ni kumtaka Aslay a keep it up ,, aongeze bidii katika muziki wake kwan unafuatilia na watu wakubwa/ wazito.
 
Mkuu ungeweka na kavidio wakati unamuuliza make mlikuwa wawili tu sisi hatuwezi kujua zaidi alivyokujibu,maelezo ya upande mmoja hayanogeshi habari weka kavidio tu ili ikibidi bwana mdogo amtungie hata wimbo huyohuyo boss mwenyewe!,lkn pia na sisi wa Tanzania tuache kurahisisha vitu kwani hicho alichokisema ni interest binafsi sasa wewe mkuu umegeuza na kutwambia kuwa anaweza akampa mradi pale USAID,tuache upogba wa kuteuana kama ilivyo hapa tz.ni hayo tu
 
Back
Top Bottom