- Thread starter
- #21
"The healthy and strong individual is the one who asks for help when he needs it. Whether he's got an abscess on his knee or in his soul."Rona.
Kiongozi Nape, kuna watu hapa ambao huwa tu wasomaji zaidi, wachambuzi na wapimaji wa mambo kabla ya kuandika neno.
Mimi nikiwa mwana CCM damu nakupa feedback yangu na natoa ushauri wangu waziwazi bila kumungúnya maneno kama ifuatavyo:
1. Nilishangilia na kupiga moyo konde na kuanza kupangusa vumbi ya kadi yangu ya CCM juu ya Kuchaguliwa kwako katika nafasi ya Ukuu wa Idara Taifani. Ilinitia moyo sana kama kijana mwenye mawazo mapya na pia kama mtu niliyekuchukulia kuwa na msimamo usiopindika katika kutetea maslahi ya umma (rejea skata la jengo la UVCCM n.k).
2. Nilifarijika sana ulipoanza kuongea pasipo kumungúnya maneno juu ya maazimio lya vikao vya juu vya chama likiwemo MAFISADI KUPIMA WENYEWE NA KUJIONDOA VINGINEVYO BAADA YA SIKU 90 CHAMA KITAWAWAJIBISHA!
3. Nilishutushwa na kutetemeka kukusikia mbele ya Luninga ukikana suala la deadline kwa Mafisadi kupewa siku 90. Na ukaanza kudefine dhana ya kuvua gamba in a very philosophical & theoretical manner kama vile: 'tumetawala miaka mingi sasa tumezeeka na hivyo inabidi tutoke ki upya' wakati kila mtu hata mtoto anajua kuwa hiyo dhana ya kujivua gamba ilianza kwa msisitizo wa kuondoa (gamba baya) wale wambao wametuchafulia chama ikiwa ni sehemu ya kujisahihisha na kurejesha heshima na matumani kwa mamilioni ya Watanzania.
4. Hili lisemwalo la wewe kuwa miongoni mwa waanzilishi wa CCJ ni jambo nyeti sana na hivyo linatakiwa kuli handle kwa uangalifu mkubwa.
Sikiliza, kama kweli kutoka moyoni unajua kuwa ulishiriki kwa namna moja au nyingine kutokana na ama kutoridhishwa kwako na mambo yalivyokuwa (kitu ambacho si ajabu ndio maana hata Chama chenyewe kufikia kuona kivue magamba!) au pia kama uliingizwa kimtego bila kujua kibinadamu, ni vyema useme wazi kuwa ni KWELI na kwamba sasa uko CCM na si CCJ kutokana na kile unachokiona kuwa CCM inaelekea kujirekebisha na kurejesha imani kwa Wananchi katika kusimamia masilahi yao kama mwanzo. Na useme waziwazi kuwa, kama kuna mtu anataka kukuadhibu kwa hatua uliyokuwa umeidhamiria basi uko tayari kupokea adhabu hiyo endapo itaamuliwa na vikao husika vilivyowekwa kihalali na CCM.
Mbona kuna wengi walikuwa Upinzani na leo wako CCM (wengine wamepewa uongozi) na hawasemwi? Siri ni kuwa walikuwa wazi! Kujiunga au kuondoka katika chama cha siasa ni kutokana na kile unachoamini na kwamba lazima ukione kinatekelezwa!
5. Kama utaendelea kukana kuwa hukuhusika na CCJ wakati ni kweli ulihusika (nasema kama ndivyo ilivyo, maana Mungu wetu, wewe mwenyewe na mashahidi wa kweli mnajua ukweli) hilo sasa ndilo KOSA KUBWA KULIKO YOTE na hakuna hatakayekuamini tena. Kumbuka, sema kweli nayo itakuweka huru au sema uongo na uendelee kuwa mtumwa na kukosa heshima na kutokubalika milele!
6. Kama kweli hukuhusika, basi shikilia msimamo wako wa kukataa, lakini suala la kupambana na Mafisadi waziwazi kwa kushirikiana na Katibu MKuu na wengine wote kwa kuwataja majina yao hadharani, kuwapa deadline na kulisimamia lazima lilejewe bila kusuasua. Matendo kama hayo ndiyo yanaweza kufyonza propadanda zote za U-CCJ, Ubaba n.k mara moja. Maana huwezi kuwafanya Watz wajinga kujadili mtu kujiunga na chama cha siasa ambapo ni uhuru wake wa kikatiba akaacha kujadili na kumsifu mtu anayeamua kwa ujasiri kumshughulikia fisadi pasi kumwangalia usoni ambaye anaathiri vibaya mlo, makazi, nishati, biashara, elimu, miundombinu yetu, rasilimali zetu na utu wetu.
Vinginevyo bado mtaonekana mnapwaya sana (hamna afya wala nguvu) katika hizo nafasi na kama ni hivyo nasema, Tanzania ni kubwa sana mtutafute sisi tuwasaidie tupasue majipu na kutumbua usaha ili tupone!
Kamwe sikubaliani na kuendelea kupaka mafuta jibu na kubadilisha mikao na mitembeotukifikiri kuwa siku moja jipu linazama lenyewe!
Ndugu yangu Kibunago,
Kwanza kwa heshima kubwa nikushukuru sana kwa ushauri na mawazo mazuri. Niseme kuwa hakuna shaka kila atakayeamua kuwa mkweli juu ya kauli ya Porokwa anajua kwanini kasema hivyo hasa ikizingatiwa mahusiano yake na monduli na msimamo wangu juu ya Monduli..
Binafsi sioni tabu ya mtu kuanzisha chama kingine cha siasa kwa mujibu wa sheria za nchi yetu sio dhambi wala jinai....Lakini kubwa kwa chama kama CCJ kilichovuma hapa nchini japo kwa muda mfupi nikihusishwa nacho kwa haki sina shida kabisa.... Tatizo hapa labda niamue kuwafurahisha mafisadi wachache MIE NAWAJUA KWA MAJINA NA ROLE ZAO WALIOANZISHA CCJ, NAJUA KWANINI ILIKUFA HAWA WANAODANDIA LEO HAKIKA NI VIBARAKA TU.....
NINGEKUWA NIMEHUSIKA HATA KWA HARUFU SIONI HAYA KUSEMA KISU KIITWE KISU NA UMMA UITWE UMMA.
JUU YA WATUHUMIWA WA UFISADI SIJUI HOJA YA KUWA HATUCHUKUI HATUA INAANZIA WAPI, TULICHOAMUA KWENYE KIKAO NA AMBACHO NIMEKISIMAMIA NA NITAENDELEA KUKISIMAMIA NI KUWA WACHUKUE HATUA WENYEWE BAADA YA HAPO WASIPOCHUKUA HATUA KIKAO KIJACHO CHA NEC TUNAWAFUKUZA. SASA HAPA KATIKATI HATUA GANI ZICHUKULIWE ILI IONEKANE TUNACHUKUA HATUA?
HIKI NI KIPINDI CHA KUSUBIRI NEC IJAYO MUONE KAMA HAWAJATOKA NDIPO NIULIZWE.....MENGINE YALE 24 YANAENDELEA KUCHUKULIWA HATUA NA MOJA NI LA KUVUNJA KITENGO CHA PROPAGANDA NA KUANZISHA KITENGO CHA MAWASILIANO KWA UMMA NA NASHUURU NI WAZO LILOJADILIWA HUMU PIA KWA MUDA MREFU