PostGE2025 HOJA: Tumefikaje Haisaidii, Tunatokaje Ndio Jambo la Msingi Je, wanaokataa maridhiano na mazungumzo wanahitaji nini hasa?

PostGE2025 HOJA: Tumefikaje Haisaidii, Tunatokaje Ndio Jambo la Msingi Je, wanaokataa maridhiano na mazungumzo wanahitaji nini hasa?

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Home tutor Dar

Senior Member
Joined
Feb 23, 2025
Posts
114
Reaction score
139
Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba 2025 uliibua hisia tofauti kwa Watanzania. Wapo waliouona kama hatua ya kidemokrasia, lakini pia wapo waliobaki na maswali kuhusu mwenendo wake. Pamoja na hayo yote mambo haya yanahitaji mazungumzo, maridhiano, na dira ya pamoja.

Tumefikaje hapa? Jibu linaweza kuwa na pande nyingi, lakini jambo muhimu sasa ni kuuliza: Tutatokaje hapa kwa pamoja kama Taifa?

Changamoto Zilizojitokeza:
1. Imani ya wananchi kwa taasisi za uchaguzi ilitetereka, hali iliyozua sintofahamu na mjadala mkubwa.
2. Matumizi ya nguvu katika maeneo kadhaa yaliathiri hali ya utulivu na amani ambayo nchi yetu imejivunia kwa miaka mingi.
3. Mazungumzo na maridhiano kabla na baada ya uchaguzi hayakupewa nafasi ya kutosha, jambo lililosababisha manung’uniko miongoni mwa makundi tofauti.

Wimbi la majeruhi na familia zilizoguswa na matukio ya kisiasa ni jambo linalohitaji huruma, uelewa, na hatua za uponyaji.

Hotuba ya Rais Samia – Ufunguzi wa Bunge la 13:
Rais alitoa wito wa maridhiano, mshikamano, na umoja wa kitaifa. Alisisitiza umuhimu wa kuangalia mbele kama taifa na kuepuka Migogoro isiyojenga ,Alitaka tuchukue hatua ya pamoja ya kujenga nchi yetu bila kushikilia chuki au tofauti za kisiasa.

“Tufanye kazi, tukosoe kwa kujenga, tukosolewe kwa kuelewa, na tuweke mbele maslahi ya Taifa.” – Rais Samia

Hii ni sauti ya busara na matumaini – na inahitaji kuungwa mkono kwa vitendo na kila upande wa jamii.

Tufanye Nini? (Tutatokaje?)
1. Kujenga maridhiano ya kweli – Vyama, viongozi wa dini, vijana, wanawake na mashirika ya kiraia washirikiane katika jukwaa la kitaifa la maelewano.
2. Kuimarisha imani kwa taasisi – Tume ya uchaguzi, mahakama, vyombo vya usalama viendelee kujenga taswira ya kutenda haki bila upendeleo.
3. Kusikiliza walioumizwa na matukio ya kisiasa – kwa pamoja kwa nia ya kujifunza, kuponya na kujenga taifa jumuishi.
4. Kutoa fursa kwa kila Mtanzania kujieleza bila hofu, kwa mujibu wa katiba na sheria.

Swali la Tafakari:
Je, wale wanaokataa maridhiano na mazungumzo wanahitaji nini hasa?
 
Aisee umeshindwa kuchemsha kicha hata dk moja tu ufanyanye mariziano bila kuwawajibisha waliowaua ndugu zetu au kisa familia yako haikuguswa
 
Wewe ukiiba kuku wangu na kumchinja ili tupate suluhu si lazima kwanza unirudishie kuku wangu? Na uende kutumikia kifungo cha wizi jela.

Basi muingie leba mtuletee watanzania wote mliowaua kisha tufanye maridhiano.
Kisha sheria ifate mkondo wake ndo maridhiano hayo.
 
Wewe ukiiba kuku wangu na kumchinja ili tupate suluhu si lazima kwanza unirudishie kuku wangu? Na uende kutumikia kifungo cha wizi jela.

Basi muingie leba mtuletee watanzania wote mliowaua kisha tufanye maridhiano.
Kisha sheria ifate mkondo wake ndo maridhiano hayo.
Hakika, unastahiri cheo katika Taifa jipya lijalo.
 
Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba 2025 uliibua hisia tofauti kwa Watanzania. Wapo waliouona kama hatua ya kidemokrasia, lakini pia wapo waliobaki na maswali kuhusu mwenendo wake. Pamoja na hayo yote mambo haya yanahitaji mazungumzo, maridhiano, na dira ya pamoja.

Tumefikaje hapa? Jibu linaweza kuwa na pande nyingi, lakini jambo muhimu sasa ni kuuliza: Tutatokaje hapa kwa pamoja kama Taifa?

Changamoto Zilizojitokeza:
1. Imani ya wananchi kwa taasisi za uchaguzi ilitetereka, hali iliyozua sintofahamu na mjadala mkubwa.
2. Matumizi ya nguvu katika maeneo kadhaa yaliathiri hali ya utulivu na amani ambayo nchi yetu imejivunia kwa miaka mingi.
3. Mazungumzo na maridhiano kabla na baada ya uchaguzi hayakupewa nafasi ya kutosha, jambo lililosababisha manung’uniko miongoni mwa makundi tofauti.

Wimbi la majeruhi na familia zilizoguswa na matukio ya kisiasa ni jambo linalohitaji huruma, uelewa, na hatua za uponyaji.

Hotuba ya Rais Samia – Ufunguzi wa Bunge la 13:
Rais alitoa wito wa maridhiano, mshikamano, na umoja wa kitaifa. Alisisitiza umuhimu wa kuangalia mbele kama taifa na kuepuka Migogoro isiyojenga ,Alitaka tuchukue hatua ya pamoja ya kujenga nchi yetu bila kushikilia chuki au tofauti za kisiasa.



Hii ni sauti ya busara na matumaini – na inahitaji kuungwa mkono kwa vitendo na kila upande wa jamii.

Tufanye Nini? (Tutatokaje?)
1. Kujenga maridhiano ya kweli – Vyama, viongozi wa dini, vijana, wanawake na mashirika ya kiraia washirikiane katika jukwaa la kitaifa la maelewano.
2. Kuimarisha imani kwa taasisi – Tume ya uchaguzi, mahakama, vyombo vya usalama viendelee kujenga taswira ya kutenda haki bila upendeleo.
3. Kusikiliza walioumizwa na matukio ya kisiasa – kwa pamoja kwa nia ya kujifunza, kuponya na kujenga taifa jumuishi.
4. Kutoa fursa kwa kila Mtanzania kujieleza bila hofu, kwa mujibu wa katiba na sheria.

Swali la Tafakari:
Je, wale wanaokataa maridhiano na mazungumzo wanahitaji nini hasa?
Mara nyingine ni muhimu kujua tumefikaje hapa ili kujua tunatokaje hapa.
 
Hizi mada za maridhiano pigeni chini bhana.Wajibikeni kwa upande wenu.

Hivi wale watoto yatima waliofiwa na mama yao mlangoni akipigwa risasi hayo maridhiano yana msaada gani kwao?

Watu waliofiwa na watoto wao kwa kupigwa risasi maridhiano yatarejesha watoto wao?(in OT(Old Testament) it is written eye for eye and tooth for tooth)

Kufika amani ya kweli kwa sasa,kwanza;kubali kwamba kiongozi mkuu ambaye ni rais akubali alihusika na vifo vya watanzania hawa.

Pili,afanye toba ya kweli(akubali na kujutia) na kuomba msamaha wa dhati kwa watanzania wote(sana waliopata misiba,majeraha na kupoteza mali)

Tatu,waliohusika wachukuliwe hatua kali(rais unaliweza hili hata ukilifanya kinafiki itakusaidia)

Mwisho akubali kutenda haki katika kila jambo(huu ndio utakuwa wimbo mpaka siku yanamshinda au anafanikiwa)
 
Huyu dogo angekuwa ni ndugu yako au mwanao ungetaka maridhiano bila watu kuwajibika na kuwajibishwa? Ili iweje? Machawa nyie mnaandika tu hata bila kutambua maumivu ambayo Watanzania wenzenu wanapitia. Wapeni muda angalau waomboleze japo wengine wengi hata miili ya wapendwa wao wanaishia kuiona tu kwenye video na picha. Pumbavu!

20251116_150612.png
20251116_150551.png
20251116_150631.png
 
Hujui chanzo unawezaje kuzungumzia suluhisho la kudumu?

Unaridhiana nini ikiwa upande mmoja bado haukubali uharibifu walioufanya?

Walioharibu mali wamepatikana,je walioua watu holela wapo wapi?
 
T
Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba 2025 uliibua hisia tofauti kwa Watanzania. Wapo waliouona kama hatua ya kidemokrasia, lakini pia wapo waliobaki na maswali kuhusu mwenendo wake. Pamoja na hayo yote mambo haya yanahitaji mazungumzo, maridhiano, na dira ya pamoja.

Tumefikaje hapa? Jibu linaweza kuwa na pande nyingi, lakini jambo muhimu sasa ni kuuliza: Tutatokaje hapa kwa pamoja kama Taifa?

Changamoto Zilizojitokeza:
1. Imani ya wananchi kwa taasisi za uchaguzi ilitetereka, hali iliyozua sintofahamu na mjadala mkubwa.
2. Matumizi ya nguvu katika maeneo kadhaa yaliathiri hali ya utulivu na amani ambayo nchi yetu imejivunia kwa miaka mingi.
3. Mazungumzo na maridhiano kabla na baada ya uchaguzi hayakupewa nafasi ya kutosha, jambo lililosababisha manung’uniko miongoni mwa makundi tofauti.

Wimbi la majeruhi na familia zilizoguswa na matukio ya kisiasa ni jambo linalohitaji huruma, uelewa, na hatua za uponyaji.

Hotuba ya Rais Samia – Ufunguzi wa Bunge la 13:
Rais alitoa wito wa maridhiano, mshikamano, na umoja wa kitaifa. Alisisitiza umuhimu wa kuangalia mbele kama taifa na kuepuka Migogoro isiyojenga ,Alitaka tuchukue hatua ya pamoja ya kujenga nchi yetu bila kushikilia chuki au tofauti za kisiasa.



Hii ni sauti ya busara na matumaini – na inahitaji kuungwa mkono kwa vitendo na kila upande wa jamii.

Tufanye Nini? (Tutatokaje?)
1. Kujenga maridhiano ya kweli – Vyama, viongozi wa dini, vijana, wanawake na mashirika ya kiraia washirikiane katika jukwaa la kitaifa la maelewano.
2. Kuimarisha imani kwa taasisi – Tume ya uchaguzi, mahakama, vyombo vya usalama viendelee kujenga taswira ya kutenda haki bila upendeleo.
3. Kusikiliza walioumizwa na matukio ya kisiasa – kwa pamoja kwa nia ya kujifunza, kuponya na kujenga taifa jumuishi.
4. Kutoa fursa kwa kila Mtanzania kujieleza bila hofu, kwa mujibu wa katiba na sheria.

Swali la Tafakari:
Je, wale wanaokataa maridhiano na mazungumzo wanahitaji nini hasa?
Haufahamu hila za CCM wewe dogo kaa kimya. Maridhiano tunayotaka sizi wananchi jambo la kwanza ni kuunda serikali ya mseto ili kuunda tume huru ya uchaguzi na uchaguzi na uchaguzi uludiwe ili wananchi wapate fulsa ya kuchagua viongozi wanaowataka

KAMA CCM HAWALITAKI HILO NA SISI WANANCHI HATUTAKI MARIDHIANO YAO YA KISENGE
 
Wakati mnateka na kuuwa watu mlikuwa hamuoni umuhimu wa maridhiano?
 
Back
Top Bottom