HOJA MBADALA: Tuhamasishe CCM imsimamishe Membe 2015?

Nakubali, Membe ndiye chaguo bora kwa CCM. Atasaidia sana 'kuleta mageuzi' ya kweli.
Thanks mkuu FJM for joining the team!. Hivi sisi Watanzania, mbona huwa hatujiulizi, sisi ndio tuna wakimbiaji mahiri since time immemorial, kina Filbert Bayi, Suleiman Nyambui, Gidamis Shanga, Nzael Kiyomo, Juma Ikaangaa etc, etc, Wakenya walikuwa nyuma yetu!. Sasa Wakenya ndio machampioni wa mbio ndefu!, Watanzania..kwishney!, Hivi kuna mnao jiuliza Wakenya wanatushindaje?!. Wakenya wanatushinda kwa ku file, runners na run mates ambao ni wasindikizaji!, wanaitwa "pace makers"!, hawa kazi yao huwa ni kukitimka mbio ili kuwachanganya na kuwachosha opponents washindwe ku-maitain constancy pace! ili the true runner wetu aweze kumaitain his pace, and win the victory!. EL could make a good "pace maker so du Membe!".
P.
 
Rais hatoki tena miji ya mwambao...safari hii ni zamu ya nyanda za juu, kaskazini na ziwa jitihada za kuumiliki u-rais mwambaoni safari hii hazita weza lbd kwa force.
 
Nimeipenda sana hii post. Kingekuwepo kitufe cha like
ningekugongea like
 
Huwa nakukubali sn ila kwa hili sikubaliani nawe hata kidogo, membe ni kiongozi asiye na subila na uwezo wake wa kiutendaji ni mdogo pia kashifa nyingi zilitakiwa zmezuiliwa na ofisi yake hasa hawa wawekezaji wanaohujum nchi toka nchi za ulaya. Huyu membe hafai kabisa kuwa rais hta ktk nafasi ya uwaziri imemshinda
 
MM naomba nichakachue thread yako kama inavyoendelea kuchakachuliwa.
Mara nyingi natatizika sana kila ninaposoma habari za fulani ni best candidate.
Hapa ndipo nakubaliana na Mkandara kuwa elimu ya uraia bado ni tatizo kubwa sana.

Wenzetu wanaojua kuchagua viongozi huangalia kigezo kimoja hadi kingine:
Maadili ya mtu, misimamo yake kisiasa, anasimamia nini, mahusiano na wenzake, mahusiano na chama chake, ushiriki katikashughuli za kijamii, maadili yake, mahusiano kati yake na wananchi, mtazamo wake kuhusu nchi, historia ya utendaji wake, maamuzi aliyowahi kuayafanya huko nyuma, uthubutu katika kusimamia anachokiamini n.k.

Tunatakiwa twende mbali zaidi ya hapa pa kusema fulani atatusaidia.
Labda nitoe mifano kidogo, ni Membe aliyetuambia kuwa tumeibiwa katika Radar, ni Membe aliyekataa kutuambia nani ni wezi. Alichotaka ni ku-score political point kuwa pesa zimerudi! Sasa huyu mtu kimaadili unamweka kundi gani?
Nina nani miongoni mwetu anayejua misimamo ya Membe kuhusu masuala ya kitaifa?

Mfano wa pili, ni Lowasa huyu aliyetuambia hakuna wizi Richmond, ni Lowasa huyu aliyejiuzulu kwa dhambi anayosema hakuitenda, ni Lowasa huyu anayesema alifanya hivyo kuilinda serikali, ni Lowasa huyo asiyetuambia nani alibofoa Richmond hadi leo tunapata hasara. Ushujaa wa kusema huyu ni best candidate unakuwa katika misingi gani?
Ni nani anayeweza kunishawishi kuhusu uadilifu wa Lowasa hadi apewe ofisi kubwa kiasi hicho?Ni nani anayeweza kutumia vigezo ilivyoweka kumpa pasi Lowasa japo 60%?

Kama ni suala la kusema tu fulani anafaa basi mimi nasema Sophia Simba anafaa kama best candidate.
Msiniulize kwa vigezo gani kwasababu lengo ni kutaja tu.
 


Ooh boy...! haya unajua kilichomo moyoni mwangu. Kadizooo
 
I wish tungekuwa na nafasi ya kupush vya kutosha, basi tungetumia nafasi hiyo kujihakikishia kuwa CDM inachukua nchi ifikapo 2015. Ni kweli Membe ni mzuri, lakini hakika Membe hana ubazu hata kidogowa kuzichanga na EL. Hakika mziki utakuwa mzito zaidi endapo EL atasimama kuliko akisimama Membe. Sijawahi kum-beza hata kidogo EL
 
Mzee Mwanakijiji hajasema kwamba Membe anafaa kuwa Rais bali anafaa kuwa Mgombea Urais kupitia CCM kuliko wenzie wote wanaotajwa. Kama kushinda au kushindwa hilo ni suala jingine kabisa linalohitaji mjadala wake!!

Brilliant mind!!! Post yangu ya awali kwa makusudi kabisa haijasema Membe anafaa kuwa Rais wa Tanzania au mgombea yeyote wa CCM kuwa anafaa kuwa Rais wa Tanzania...
 

"Nikisema nitagombea urais nitapakwa matope puani na machoni hadi nitashindwa kuchukua na hizo fomu… kuna watabiri wa ajabu na uongo ambao wamezuka kuwatabiria watu. Hata usipoomba wanapata jina lako wanakuchukulia fomu na kukupigia kura na kukwambia wewe utapata asilimia fulani… mtu anakwambia hivyo wakati hata hujatamka wala hujachukua fomu" - source Membe mwenyewe.

Haya bana. Naona kuna mwingine kule kaanzisha thread ya kumetetea Dr. Migiro kugombea urais kwa kuwa eti hana kashfa, si fisadi na hana doa. Na wewe hapa unasema Membe hana kashfa. Kama kigezo cha kugombea urais Tanzania ni kutokuwa fisadi, kutokuwa na doa au kashfa si hata wewe Mwanakijiji unaweza kuchukua fomu fasta na kugombea? Au una kashfa?

Siyo kweli kuwa kama Membe "hataoteshwa" kugombea urais, basi ndio itakuwa mwisho wa CCM. Tatizo sio mgombea. Tatizo ni system ya chama chenyewe na Watanzania kwa ujumla. CCM inaweza kumweka mgombea yoyote hata kama ni fisadi, ana doa au kashfa na akashinda vile vile. Sababu ni kwamba kwa sasa Watanzania wengi sana hawana mpango wowote wa ku-replace system ya sasa na system mpya.

CCM wataweka mtu yoyote na kushinda simply because most Tanzanians are sad, but not angry with what is going on in their own country. Soma posts kibao hapa JF na kule facebook nyingi zinaanza na "Ee Mungu wetu tusaidie kuondoka na hili tatizo". Ni full maombi tuu. "Usually when people are sad, they don't do anything. They just cry over their condition. But when they get angry, they bring about a change." – Malcolm X.
 

pasco mi nakuelewa sana,pamoja na kuwa chama cha kwanza kusajiliwa,pamoja na kwamba ndo kimeunda serikali,lakini kwa sasa ccm kimepoteza uhalali wa kuiongoza tanzania,na sababu ni wale waliomo ndani ya CCM,
hata kiwe kna miaka 200 kwa ukongwe,hakuna msafi tena pale CCM,ndo maana hata minyukano yao yote wana ccm imekaa kimaslah yao binafsi
 
Mkuu napendekeza ccm wamsimamishe white hair au bibi kiroboto

 

Ka akigombea Membe urahisi coz sio urais basi hata tlp watachukua nchi
 
Adui namba moja wa tanzania ni c.c.m kwa hyo hamna cha el wa nini
 

mdau nazifatilia comment zako,unafafanua vizuri sana,,,,,,membe jimbo limemshinda nchi ataiweza?????
Membe anasema tayari anamaadui,na aliahidi kuwatatja,je si kwamba ataendeleza siasa za jk za visasi????
Kwenye Color hakuna cha kuongeza,hawa wanaowapigia kelele akina membe na Lowassa ni waramba nyayo tu,,,baadae wapewe U-DC
 
Sawa wacha niseme kwamba tuna mawazo tofauti juu ya hili (ndio demokrasia yenyewe hiyo) labda hatujaelewana na tunaongelea vitu viwili tofauti! Tukubali kutofautiana!
Mkuu wangu nimekuelewa sana na nimewahi kusema wanawake jinsi wasivyopenda kumpa support mwanamke mwenzao nadhani ilikuwa mada fulani aloileta marehemu Mpiganaji na mbunge wetu wa viti maalum. Hilo lipo wazi wala halina Ubishi isipokuwa pale Umoja wa wananwake unapohusika ama kushirikishwa hasa ktk siasa zetu nimegundua kwamba wana nguvu kubwa sana ya ushawishi maana JK mwaka 2010 alikuwa ktk hali mbaya sana kisiasa. Na nachelea kusema kwamba mwaka 2010 CCM walikuwa ktk hali mbaya zaidi na uwezekano wa kushndwa vibaya ulikuwa wazi lakini mbinu zao za kutumia mgawanyiko wa wananchi ktk makundi ya kijamii ulitumika kama kawaida yao hasa pale wanapobanwa kona..Hivyo, mbegu walobakia nayo ni AshaRose maana ktk Udini na Ukabila wameshindwa kukivuruga CDM -Tujiandae kwa hilo..
 
Kwa Kanuni ya ushindi: Mshindi ni Mshindi, CCM kupata 50.1% dhidi ya Chadema 49.9%, CCM ni mshindi. Membe au mgombea mwingine yeyote atakayesimamishwa na CCM, hasa wale wote ambao tayari wapo masikioni mwa Watanzania watapita kwa urahisi sana dhidi ya Chadema chini ya kanuni hii ambayo Chadema kwa sababu tusizojua hawaonekani kuwa na jitiada zozote za kuifanyia kazi. Vinginevyo katika siasa za Tanzania kuelekea 2015 zinazotawaliwa na "innocent until proven guilty, lakini muhimu zaidi, guilty only if you dont have money to buy justice, any publicity is good publicity, iwe ya ufisadi, kukamatwa ugoni n.k;
 

Mkuu Mkandara: Tafadhali angalia hapo nilipoweka red!! Kwa kutumia hiyo kauli mbiu inaashiria ufanisi bora? Hili la kusema kuwa wanawake wakiwezeshwa wanaweza bado ni kitendawili kwa hapa Tanzania. Wanawake watendaji wamewezeshwa kielimu na kwa semina elekezi lakini mazingira ya kazi si rafiki kwao. Je wanawake walio madarakani wamewezaje kuwakomboa wananchi kutokana na mateso ya umaskini, ujinga na maradhi. Tuchukulie mfano wa wabunge, viongozi wanawake kwenye mawizara, wakuu wa mikoa na wilaya na wakurugenzi wa wilaya hivi wameonyesha utendaji uliotukuka tofauti na wanaume wenye nafasi kama hizo? Swali moja tu je, ubadhirifu wa mali ya umma haupo kwenye sehemu ambazo wanawake wanaongoza? Bila kubadilisha mfumo uliopo hata wanawake wakipewa nafasi zote za uongozi bado ni tabu na shida tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…