Mjenda Chilo
JF-Expert Member
- Jul 20, 2011
- 1,471
- 526
Membe anaonekana anaweza lakini affiliates wake je? decendant wa nani? kusave interest za nani? hapo ndo shughuli. Kama Jk akiweza kuweka mgombea basi Membe sawa, lkn je? ndani ya ccm watalikubali hilo? na wananchi watakubali tawi la JK litawale? akifaulu hapo mi sidhani.
Ukiangalia sana kati ya viongozi wengi wa CCM na walioko serrikalini Membe ndiye anayeonekana kuja kuweza kumudu kuwa mgombea wa kiti cha Urais kupitia chama hicho. Ukimlinganisha na wagombea wengine (hasa Lowassa aliyejiuzulu kwa kashfa) ni Membe tu ambaye anaonekana kulindwa na mlolongo mkubwa wa kashfa mbalimbali na japo - kama nilivyosema wiki kadhaa nyuma - hajajiandaa kuwa Rais ni wazi miaka hii miwili iliyobakia inaweza kumsaidia kujitengenezea na kuwa a true "presidential candidate"
CCM ikimsimamisha Membe kama mgombea wake inaweza kuwa na nafasi ya kushinda tena kiti cha Urais; wakimsimamisha mtu mwingine yeyote itakuwa ni mwisho wa utawala wa CCM.
Ni kweli?