Hoja 5 ambazo viongozi wa vyama vya siasa watazungumza na Rais Samia Hassan

Hoja 5 ambazo viongozi wa vyama vya siasa watazungumza na Rais Samia Hassan

tpaul

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
25,826
Reaction score
25,116
Bila kuchoshana na maneno mengi, naomba niingie kwenye mada moja kwa moja. Kwa maoni yangu, nadhani hoja zifuatazo ndizo zitakuwa ajenda kuu kipindi viongozi wa vyama vya siasa wakikutana na Rais Samia Hassan ikulu ya Chamwino jijini Dodoma, kama Rais mwenyewe alivyoahidi kukutana na wanasiasa hao ili kuzika tofauti na chuki za kisiasa zilizoshamiri nchini kwa kipindi cha miaka 6 ya utawala wa hayati Dr Magufuli:

1. Katiba mpya
Hoja ya Katiba mpya imekuwa mwiba mkali sana kwa siku za hivi karibuni, hasa baada ya kufariki kwa Dr Magufuli. Katiba mpya ndilo litakuwa suluhisho la kudumu kwa matatizo mengi yanayolikumba taifa hili. Kwa kuwa mama Samia Hassan alikuwa makamu mwenyekiti wa bunge la katiba, nina imani kuwa atawapatia watanzania katiba mpya kuanzia pale mchakato ulipoishiwa endapo atashauriana vizuri na viongozi wa vyama vya siasa pindi watakapokutana naye Ikulu ya Chamwino. Nakumbuka mbunge wa Makambako, Deo Sanga, alidemka bungeni kisawasawa ile siku ambayo katiba ya wananchi ilipigwa chini rasmi baada ya kundi la UKAWA kujitoa na kuwaacha wachumiatumbo bungeni peke yao. Mama SSH ndiye tumaini pekee la watanzania kuwarejeshea katiba yao (Katiba ya Wananchi).

2. Kikokotoo
Bila shaka hiki kikokotoo kilianzishwa na Rais Magufuli, hasa baada ya kuifilisi mifuko ya hifadhi ya jamii. Mifuko hii ilifilisiwa na serikali ya Magufuli kwa namna mbili: Mosi, serikali inapaswa kupeleka michango yake kwenye mifuko kila mwezi lakini, kwa makusudi mazima, haipeleki michango yoyote. Pili, pamoja na kuwa serikali haichangii chochote, serikali ya Magufuli ilichota pesa nyingi sana kutoka kwenye mifuko hii kwa sababu mbalimbali kama vile ujenzi wa SGR, Stiglier’s Gorge, Uchaguzi Mkuu, barabara, nk. Haya ni matumizi mabaya ya mifuko kwa kuwa haikuanzishwa kwa makusudi ya kutoa fedha za kujengea miradi bubu ya serikali.


3. Tume Huru ya Uchaguzi
Sote ni mashahidi jinsi uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 ulivyochezewa na serikali ya Magufuli. Uliofanyika sio uchaguzi bali ni uchafuzi. Kukiwa na Tume Huru ya Uchaguzi yenye misingi imara isiyoweza kuchezewa na mtawala yeyote, haki na uwazi itatawala katika chaguzi na hakutakuwa na uingiliaji wa kinajisi wa wanasiasa wachumiatumbo kama ilivyotokea katika uchaguzi uliopita.

4. Covid 19 wa JPM (na Ndugai)
Kule mjengoni kuna wabunge 19 ambao hawatokani na chama chochote cha siasa na hata wao wenyewe wameishajikana lakini Job Ndugai na JPM waliamua kuwachomeka mle kwa lengo wanalolijua wao wenyewe. Mpaka sasa fedha kibao za wananchi zimeishatumika kuwalipa “wabunge” hawa. Tunaomba wanasiasa wamshauri vizuri mama Samia awafukuze bungeni hawa covid-19 ili kuokoa fedha za umma zinazopotea bila sababu na pesa walizokwishalipwa hadi sasa wazirejeshe mara moja.


5. Mitihani ya ku-BET
Elimu ya wanafunzi wetu imeharibiwa kwa kiasi kikubwa sana kipindi cha utawala wa hayati JPM. Ni katika kipindi hiki tumeshuhudia mitihani ya ku-BET iliyopelekea wanafunzi kujiunga sekondari wakiwa hawajui kusoma, kuandika au kuhesabu. Hii hoja ni nyeti sana kwa sababu watoto wanaolemazwa na hizi siasa uchwara za JPM ni wale wa “wanyonge” wanaosoma shule za Kata huku watoto wa vigogo wakisomeshwa shule za Academies. Nina imani mama Samia akishauriwa vizuri ataifuta mitihani yak u-BET na hata kumfuta kazi waziri wa elimu aliyekubali uwepo wa hii mitihani haramu.


Kwa mtazamo wangu, hizi ndizo hoja kuu 5 ambazo viongozi wa vyama vya siasa watakaokutana na mama Samia hawatakosa kuzizungumzia. Nawe mchangiaji unaweza ukaongezea hoja yoyote ambayo unadhani ni muhimu kupenyezwa kwa Rais SSH kupitia kwa viongozi wa siasa.

Nawasilisha.
 
Tume ya uchunguzi
Mikutano ya hadhara
Katiba
Covid19 happy no sehem ya ubovu wa tume
 
Ingekuwa vema kama wangetoa hoja moja ya namna gani na wao wawe sehemu ya utawala.
Kwa mfano wanaweza kubadili kipengele kinachosema "chama kinachoshinda uchaguzi ndicho kiunde Serikali " badala yake iwe "yeyote yule asiye na chama au mwenye chama anaweza kuteuliwa katika wadhifa wowote ndani ya Serikali.
Lakini pia wanaweza kuongeza hoja ya wagombea binafsi hasa ngazi ya Mitaa /vitongoji na udiwani.
 
Ingekuwa vema kama wangetoa hoja moja ya namna gani na wao wawe sehemu ya utawala.
Kwa mfano wanaweza kubadili kipengele kinachosema "chama kinachoshinda uchaguzi ndicho kiunde Serikali " badala yake iwe "yeyote yule asiye na chama au mwenye chama anaweza kuteuliwa katika wadhifa wowote ndani ya Serikali.
Lakini pia wanaweza kuongeza hoja ya wagombea binafsi hasa ngazi ya Mitaa /vitongoji na udiwani.
Kwahiyo wakaongee na rais kutafuta madaraka na posho badala ya muafaka wa kitaifa ?
 
Kwahiyo wakaongee na rais kutafuta madaraka na posho badala ya muafaka wa kitaifa ?
Sio habari ya posho wala madaraka.
Bali ni namna gani vyama vyao vitachangia katika usimamizi wa rasilimali za nchi, hata hivyo si vibaya na wengine wasio na vyama kuwa sehemu ya uwakilishi/utumishi WA Wananchi.
Ushirikishwaji wao ndani ya Serikali ndio njia sahihi na wao kujifunza ili hapo baadae waje kushika dola na kubadilisha vile wanavyoona havikuwa sawa.
Haiwezekani kuchukua agenda nzito nzito ili zitekelezwe kwa haraka, waanze na vitu rahisi rahisi vya kawaida kwanza.
 
Sio habari ya posho wala madaraka.
Bali ni namna gani vyama vyao vitachangia katika usimamizi wa rasilimali za nchi, hata hivyo si vibaya na wengine wasio na vyama kuwa sehemu ya uwakilishi/utumishi WA Wananchi.
Ushirikishwaji wao ndani ya Serikali ndio njia sahihi na wao kujifunza ili hapo baadae waje kushika dola na kubadilisha vile wanavyoona havikuwa sawa.
Haiwezekani kuchukua agenda nzito nzito ili zitekelezwe kwa haraka, waanze na vitu rahisi rahisi vya kawaida kwanza.
Hilo ni jambo ambalo haliwezekani kwani linahitaji mabadiliko ya katiba kwanini wasipeleke ajenda ya katiba mpya tu badala ya kuanza kulilia vyeo ?
 
Hilo ni jambo ambalo haliwezekani kwani linahitaji mabadiliko ya katiba kwanini wasipeleke ajenda ya katiba mpya tu badala ya kuanza kulilia vyeo ?
Ni kweli katiba mpya ni nzuri sana, lakini katika kipindi waanze kwanza na marekebisho madogo madogo ambayo pengine yanaweza kupelekea takwa zito la katiba mpya kwa mfano.

Tume huru ya uchaguzi.

Vipaumbele vya kitaifa na
Mgawanyo wa vipaumbele kulingana na idadi ya watu, Jiographia na vigezo vya kiusalama.

Ushiriki wa Wananchi katika kuchangia pato la Taifa bila kuathiri shughuli za kuzalisha mali /uwekezaji/utalii/makazi ya wanyama /vivutio vya uwekezaji na miundombinu ya kimkakati.

Namna gani ukuaji wa uchumi unaenda sambamba na hali halisi ya maisha ya watu.
 
Wahanga wa kesi za kubambikizwa za uhujumu uchumi utakatishaji fedha wote watolewe , kesi za uchaguzi , za kisiasa , viongozi wa dini waliokizuizini bila kufungwa wote waachiwe .
 
Bila kuchoshana na maneno mengi, naomba niingie kwenye mada moja kwa moja. Kwa maoni yangu, nadhani hoja zifuatazo ndizo zitakuwa ajenda kuu kipindi viongozi wa vyama vya siasa wakikutana na Rais Samia Hassan ikulu ya Chamwino jijini Dodoma, kama Rais mwenyewe alivyoahidi kukutana na wanasiasa hao ili kuzika tofauti na chuki za kisiasa zilizoshamiri nchini kwa kipindi cha miaka 6 ya utawala wa hayati Dr Magufuli:

1. Katiba mpya
Hoja ya Katiba mpya imekuwa mwiba mkali sana kwa siku za hivi karibuni, hasa baada ya kufariki kwa Dr Magufuli. Katiba mpya ndilo litakuwa suluhisho la kudumu kwa matatizo mengi yanayolikumba taifa hili. Kwa kuwa mama Samia Hassan alikuwa makamu mwenyekiti wa bunge la katiba, nina imani kuwa atawapatia watanzania katiba mpya kuanzia pale mchakato ulipoishiwa endapo atashauriana vizuri na viongozi wa vyama vya siasa pindi watakapokutana naye Ikulu ya Chamwino. Nakumbuka mbunge wa Makambako, Deo Sanga, alidemka bungeni kisawasawa ile siku ambayo katiba ya wananchi ilipigwa chini rasmi baada ya kundi la UKAWA kujitoa na kuwaacha wachumiatumbo bungeni peke yao. Mama SSH ndiye tumaini pekee la watanzania kuwarejeshea katiba yao (Katiba ya Wananchi).

2. Kikokotoo
Bila shaka hiki kikokotoo kilianzishwa na Rais Magufuli, hasa baada ya kuifilisi mifuko ya hifadhi ya jamii. Mifuko hii ilifilisiwa na serikali ya Magufuli kwa namna mbili: Mosi, serikali inapaswa kupeleka michango yake kwenye mifuko kila mwezi lakini, kwa makusudi mazima, haipeleki michango yoyote. Pili, pamoja na kuwa serikali haichangii chochote, serikali ya Magufuli ilichota pesa nyingi sana kutoka kwenye mifuko hii kwa sababu mbalimbali kama vile ujenzi wa SGR, Stiglier’s Gorge, Uchaguzi Mkuu, barabara, nk. Haya ni matumizi mabaya ya mifuko kwa kuwa haikuanzishwa kwa makusudi ya kutoa fedha za kujengea miradi bubu ya serikali.


3. Tume Huru ya Uchaguzi
Sote ni mashahidi jinsi uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 ulivyochezewa na serikali ya Magufuli. Uliofanyika sio uchaguzi bali ni uchafuzi. Kukiwa na Tume Huru ya Uchaguzi yenye misingi imara isiyoweza kuchezewa na mtawala yeyote, haki na uwazi itatawala katika chaguzi na hakutakuwa na uingiliaji wa kinajisi wa wanasiasa wachumiatumbo kama ilivyotokea katika uchaguzi uliopita.

4. Covid 19 wa JPM (na Ndugai)
Kule mjengoni kuna wabunge 19 ambao hawatokani na chama chochote cha siasa na hata wao wenyewe wameishajikana lakini Job Ndugai na JPM waliamua kuwachomeka mle kwa lengo wanalolijua wao wenyewe. Mpaka sasa fedha kibao za wananchi zimeishatumika kuwalipa “wabunge” hawa. Tunaomba wanasiasa wamshauri vizuri mama Samia awafukuze bungeni hawa covid-19 ili kuokoa fedha za umma zinazopotea bila sababu na pesa walizokwishalipwa hadi sasa wazirejeshe mara moja.


5. Mitihani ya ku-BET
Elimu ya wanafunzi wetu imeharibiwa kwa kiasi kikubwa sana kipindi cha utawala wa hayati JPM. Ni katika kipindi hiki tumeshuhudia mitihani ya ku-BET iliyopelekea wanafunzi kujiunga sekondari wakiwa hawajui kusoma, kuandika au kuhesabu. Hii hoja ni nyeti sana kwa sababu watoto wanaolemazwa na hizi siasa uchwara za JPM ni wale wa “wanyonge” wanaosoma shule za Kata huku watoto wa vigogo wakisomeshwa shule za Academies. Nina imani mama Samia akishauriwa vizuri ataifuta mitihani yak u-BET na hata kumfuta kazi waziri wa elimu aliyekubali uwepo wa hii mitihani haramu.


Kwa mtazamo wangu, hizi ndizo hoja kuu 5 ambazo viongozi wa vyama vya siasa watakaokutana na mama Samia hawatakosa kuzizungumzia. Nawe mchangiaji unaweza ukaongezea hoja yoyote ambayo unadhani ni muhimu kupenyezwa kwa Rais SSH kupitia kwa viongozi wa siasa.

Nawasilisha.
Uhuru wa vyombo vya habari na Mishahara ya wapunge kuanza kukatwa kodi
 
Uhuru wa vyombo vya habari na Mishahara ya wapunge kuanza kukatwa kodi
Mkuu, wabunge wanachukuliwa kuwa sio watumishi wa umma bali wachumiatumbo. Ndio maana mishahara na posho zao huwa hazikatwi kodi.
 
Kwahiyo wakaongee na rais kutafuta madaraka na posho badala ya muafaka wa kitaifa ?
Mkuu, nia na malengo ya mwanasiasa yeyote ni kushika madaraka. Hilo lisikupe shida. Tunachotaka sasa hivi ni siasa safi zinazoendeshwa kwa misingi ya kistaarabu pasipo kulazimika kuondoa uhai wa watu ili uingie au ubakie madarakani.
 
.katiba mpya
.katiba mpya
.katiba mpya
.katiba mpya

ikipatikanwa hiki vingine vyote vitakuwa humu ndani
 
Back
Top Bottom