mtu anapo kimbia bafuni bila nguo kisa ameona mende ile ni hofu lakini mtu anapo kimbia simba msituni ile
ni anakimbia hatari, mtu anapo ona kisiki usiku na kuzani ni mtu ile ni hofu. Tukiweza kutofautisha kati ya hofu na hatari tunaweza kuwa realy na kuishi kwa kiwango kikubwa bila hofu.
Najaribu kutafakari asili ya hofu.
tunazaliwa nayo au tunafujifunza, je msingi mkuu wa hofu nin?? je ni ujinga kwa maana ya
kwamba kuogopa vitu ambavyo hatuvijui kama kifo.
Hofu(false expectation appearing realy = fear) nashawishika kusema ni matokeo ya uwezo mkubwa wa akili
zetu kukumbuka(memory) na imagination(mawazo).
Akili zetu zimekuwa ni silaha kubwa sana ambayo iko against us ambayo tumeitumia kwa mda mrefu kujianangamiza,
na hofu ni rafki mkubwa wa akili. Ikunbukwe akili sio sehemu ya ubongo bali ni namna ubongo unavyo generate mawazo
kila wakati yawe sahihi au lah by defaualt kila mtu anazaliwa na akili.
Asili ya hofu tunaweza kuifahamu tu kwa kuangalia asili ya akili, Akili haiwezi kutofautisha kati ya realy and imagination
ndio maana ukiwa unaota unahisi ni kweli pia hata wanaocheza magem ya hologram wanaelewa.
Tunahitaji kitu cha ziada (intellect) upeo ambao utatuwezesha kutofautisha kati ya mawazo yanayo be generated na akili
kuweza kutofautisha mawazo ambayo ni realy na vicevesa.
kwanini tuipinge hofu? kwasababu hofu inaathiri our judgement kawaida ya hofu haitoi nafasi ya kufanya maamzi kwa kuzingatia
kanuni na uhalisia bali hisia na mihemko . Tafakari bado naamini hofu ni bidhaa kunawatu wananufaika na hofu yako katika
kila nyanja ya maisha yako dini, siasa, elimu, afya.
Nikuache na swali:
msingi mkuu wa dini ni imani au hofu?
“mtu anapo ona kisiki usiku na kuzani ni mtu ile ni hofu.”
Daah umenikumbusha mbali sana kama sikufa ile siku basi mungu bado anaendelea kuupigania uhai Wangu!!
Ilikua sa 11 kasoro kijijin huko,naelekea msikitini kuwahi swala ya alfajir
Ile nakaribia umbali wa kama nusu ekari,naona kitu ambacho sikielew akilini mwangu kwani pale napita kila siku Na hamna kisiki
Nikawa nawaza haraka haraka bila majibu Na huku akili haitulii kabisa
Mara mwili ukaanza kuzizima kuanzia miguuni hadi kichwani ghafla kichwa kikawa kizito Na mwili pia ukaungana jumlajumla
Wakati haya yote nayahisi si kwamba nimesimama naendelea safari yangu kuelekea kule kisiki kilipo na ndo msikiti ulipo yani...
aisee kila hatua nnayopiga mguu mzito mno
Mara kisiki kikatikisika ....daaaah!! Nilizidi kuvurugwa kishenzi
dah nikajikuta mzima mzima yule jamaa nimemvaa na kumkaba shingo
Loooh! salaaaleh!!!!!
Kumbe ni mtu bhana af namjua,ana matatizo ya akili wakat mwingine anaweza kusimama mahali mda mrefu tena bila kutikisika
aisee....
Wakat nimemkaba vile nikawa na mwambia ndgu yangu kumbe ndo wew leo unataka kuniuwa
Hiyo sauti namna nilivyoitoa ya kuongea nae sasa
Yani nimeifos af nzito kinouma
Nikamuachia akaanguka chini
Dah nikaingia zangu msikitini,lakni kwa kweli sikua na amani yan