Peter Stephano 809
Senior Member
- Feb 29, 2020
- 120
- 162
Aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kupitia mtandao wa Instagram amechapisha akilalamika kuwa kuna makundi 5 ya watu wanaopanga kumuangamiza.
Makonda amesema makundi hayo yanataka kuhakikisha anapata kesi ya uhujumu uchumi au auwawe kabisa kwa manufaa yao binafsi.
"Nafahamu pia juu ya mbinu zinazoandaliwa ili kuniuwa kwa faida a familia zao pamoja na kutengeneza mashaidi wa uongo ili mnipe kesi ya uhujumu uchumi" Makonda ameandika.
Aidha makonda amebainisha makundi hayo yanaundwa na wauza madawa ya kulevya, mashoga, mafisadi, wanufaika na madawa ya kulevya na kundi la mwisho ambalo hakuliweka wazi. Ameandika kuwa licha ya kazi nzuri aliyoifanya wakati akiwa ofisini lakini bado kuna watu wanataka kumpoteza.
Hakika ukiwa mtumishi mwaminifu unaetetea haki za wanyonge tena ukitokea kwenye familia masikini haya ndivo malipo yake?, mtu aliejenga hospital , aliejenga ofisi za CCM, magari ya police ofisi za walimu, vituo vya polisi, shule za secondari na msingi, kutibu wagonjwa mpaka meli kuja Tanzania, kuhudumia makundi mbalimbali mpaka kuiunganisha serikali na viongozi wa dini leo hii naonekana eti natakiwa kunyongwa?" amehoji.
Sio mara ya kwanza Makonda kulalamika ingawaje hapo awali alisema kuwa kuna watu wana muhujumu kutaka kupora mali zake kwa maksudi.
Malalamiko haya ya Makonda yanaibua hisia na maswali mengi ambayo mtu anaweza kujiuliza ni nini kinamsibu Makonda?
Alipo sema kuwa wanataka kumnyang'anya mali ikaonekana ni jambo dogo lakini kufika kuhofia uhai wake ni jambo kubwa linalohitaji kujulikana.
Kama kweli kuna watu wanataka kumdhuru makonda ni akina nani hao na kwanini wasichukuliwe hatua?
Makonda anadai hayo makundi 5 ya watu wanootaka kumpoteza yanajulikana kwanini asipeleke malalamiko kwenye vyombo vya dora Mahakama na polisi kwa hatua za kisheria zaidi?
Tuseme kwamba Makonda haviamini vyombo vya dora hadi anakimbilia mitandaoni kulalamika ili apate huruma ya raia wa kawaida?
Hatuwezi kufikiria kuwa Makonda aliyetatua migogoro lukuki akiwa mkuu wa Mkoa hajui taratibu za kufuata ili kuripoti matukio kama haya?
Hapana kabisa bado kuna maswali mengi tunapaswa kujiuliza ili tupate kujua makonda ana hofu gani inayomtafuna na kumfanya alalamike kila kukicha.
Hatuwezi kujua ukubwa wa madaraka ya watu hao alio wataja katika makundi matano pengine ni wakubwa kimamlaka anohofia hawezi kupata haki, lakini mahakama na polisi ni vyombo huru anaogopa nini?
Bila shaka serikali ina miongozo yake katika kuwasaidia viongozi wake wastaafu kwanini Makonda hajatumia nafasi hiyo kulalamika?
Malalamiko ya Makonda Mitandaoni yanafikirisha na yanahitaji majibu.
Peter Mwaihola
Makonda amesema makundi hayo yanataka kuhakikisha anapata kesi ya uhujumu uchumi au auwawe kabisa kwa manufaa yao binafsi.
"Nafahamu pia juu ya mbinu zinazoandaliwa ili kuniuwa kwa faida a familia zao pamoja na kutengeneza mashaidi wa uongo ili mnipe kesi ya uhujumu uchumi" Makonda ameandika.
Aidha makonda amebainisha makundi hayo yanaundwa na wauza madawa ya kulevya, mashoga, mafisadi, wanufaika na madawa ya kulevya na kundi la mwisho ambalo hakuliweka wazi. Ameandika kuwa licha ya kazi nzuri aliyoifanya wakati akiwa ofisini lakini bado kuna watu wanataka kumpoteza.
Hakika ukiwa mtumishi mwaminifu unaetetea haki za wanyonge tena ukitokea kwenye familia masikini haya ndivo malipo yake?, mtu aliejenga hospital , aliejenga ofisi za CCM, magari ya police ofisi za walimu, vituo vya polisi, shule za secondari na msingi, kutibu wagonjwa mpaka meli kuja Tanzania, kuhudumia makundi mbalimbali mpaka kuiunganisha serikali na viongozi wa dini leo hii naonekana eti natakiwa kunyongwa?" amehoji.
Sio mara ya kwanza Makonda kulalamika ingawaje hapo awali alisema kuwa kuna watu wana muhujumu kutaka kupora mali zake kwa maksudi.
Malalamiko haya ya Makonda yanaibua hisia na maswali mengi ambayo mtu anaweza kujiuliza ni nini kinamsibu Makonda?
Alipo sema kuwa wanataka kumnyang'anya mali ikaonekana ni jambo dogo lakini kufika kuhofia uhai wake ni jambo kubwa linalohitaji kujulikana.
Kama kweli kuna watu wanataka kumdhuru makonda ni akina nani hao na kwanini wasichukuliwe hatua?
Makonda anadai hayo makundi 5 ya watu wanootaka kumpoteza yanajulikana kwanini asipeleke malalamiko kwenye vyombo vya dora Mahakama na polisi kwa hatua za kisheria zaidi?
Tuseme kwamba Makonda haviamini vyombo vya dora hadi anakimbilia mitandaoni kulalamika ili apate huruma ya raia wa kawaida?
Hatuwezi kufikiria kuwa Makonda aliyetatua migogoro lukuki akiwa mkuu wa Mkoa hajui taratibu za kufuata ili kuripoti matukio kama haya?
Hapana kabisa bado kuna maswali mengi tunapaswa kujiuliza ili tupate kujua makonda ana hofu gani inayomtafuna na kumfanya alalamike kila kukicha.
Hatuwezi kujua ukubwa wa madaraka ya watu hao alio wataja katika makundi matano pengine ni wakubwa kimamlaka anohofia hawezi kupata haki, lakini mahakama na polisi ni vyombo huru anaogopa nini?
Bila shaka serikali ina miongozo yake katika kuwasaidia viongozi wake wastaafu kwanini Makonda hajatumia nafasi hiyo kulalamika?
Malalamiko ya Makonda Mitandaoni yanafikirisha na yanahitaji majibu.
Peter Mwaihola