Hizi sio ndoto za kawaida

Hizi sio ndoto za kawaida

Mkuu mshana mi niliota nakimbia ila hatua nilizokuwa napiga zilikuwa ndefu sana yaani napaa kama natembea mwezini
 
View attachment 421080Ni usiku mwingine tena tunapojiandaa kupumzika vitandani mwetu ( hata kama ni ugenini gesti house au barabarani kuna dakika chache utalala kidogo na kuota)
Ndoto njozi na kuota ni hitaji la kawaida la mwanadamu, shida ipo ni je unaona ndoto za aina gani?

-unaota ndoto za kawaida kutokana na harakati za kawaida za kimaisha kutokana na fikra mawazo matendo na maono?

-Ama la unaota ndoto taarifa au ndoto ujumbe au ndoto maono? Ndoto zenye ujumbe maalum?

- Au je unaota zile ndoto zile ambazo si ndoto bali ni matendo ya giza? Ndoto za
Kuota umelazwa kwenye jeneza
Kuota unazama/unazamishwa baharini
Kuota unakula/unalishwa nyama

Kuota unang'atwa na mdudu na unapata maumivu mpaka asubuhi
Kuota unakimbizwa au kufukuzwa
Kuota umefungiwa kwenye kiota chupa nk
Ndoto zote hizi huwa live mpaka asubuhi au unapostuka na unakumbuka kila kitu saa nyingine hata uchovu maumivu na Ladha....!

Ndoto za namna hii si ndoto za kawaida na huambatana na mambo yako mengi kuharibika! Hizi ni ndoto za kufanyiwa mambo mabaya na watu wabaya
Ukiweza jitahidi kuchunguza ndoto zako leo na siku zijazo utagundua kitu View attachment 421088

Mimi jaman nikiota ndoto hua inatokea kweli niliahawah kuota mtt wa dada yangu amefarik kwel baada ya cku3 akafarik...niliwah kuota mama mdogo amefarik kwel baada ya mwez akafarik..Wa mwsho nilishawah kuota mama yangu amefarik nikalia mpaka nmezimia na kwel akafarik nilivyoota kwny ndoto ndivyo ilivyotokea kwa kwel mpaka naogopa.
 
Mshana jr, mie tokea mama yangu alivyofariki huwa kila mara namuota tena ndoto za Enzi nilivyokuwa mdogo, na weza kuongea naye kama vile yupo na hata kumueleza yanayonisibu au hata furaha yangu yaani ANAKUWA KAMA VILE YUPO TU

Sio ww peke yako hata mm tena mama yangu naongea nae akiwa amevaa mavaz meupe na anaonekana bado msichana huku anatabasamu
 
Mimi jaman nikiota ndoto hua inatokea kweli niliahawah kuota mtt wa dada yangu amefarik kwel baada ya cku3 akafarik...niliwah kuota mama mdogo amefarik kwel baada ya mwez akafarik..Wa mwsho nilishawah kuota mama yangu amefarik nikalia mpaka nmezimia na kwel akafarik nilivyoota kwny ndoto ndivyo ilivyotokea kwa kwel mpaka naogopa.
Hizi ndio zile ndoto taarifa au ndoto maono! Kama ungejaribu kuwaambia ungeambulia kuambiwa una mdomo mbaya
 
Hizi ndio zile ndoto taarifa au ndoto maono! Kama ungejaribu kuwaambia ungeambulia kuambiwa una mdomo mbaya

Kabla mama yangu hajafariki alishanikataza vitu kama hvyo nisimuhadithie mtu na nikitaka kufanya jambo lolote lile langu la maendeleo nisimwambie mtu nifanye kmya kmya
 
Sio ww peke yako hata mm tena mama yangu naongea nae akiwa amevaa mavaz meupe na anaonekana bado msichana huku anatabasamu
Yaaani mimi hadi nafurahi, maana naongea naye, namweleza jambo lolote linalonisibu ananishauri, yaani tunaongea utadhani kweli yuko hai! Yaani kuna wakati huwezi kuamini hadi ananiambia hapo unakosea fanya hivi fanya hivi.
Mwee Jamani mama yangu upumzike kwa amani, alikatika kama glass ghafla eti moyo valvu ziliachia🙁🙁🙁🙁
 
Yaaani mimi hadi nafurahi, maana naongea naye, namweleza jambo lolote linalonisibu ananishauri, yaani tunaongea utadhani kweli yuko hai! Yaani kuna wakati huwezi kuamini hadi ananiambia hapo unakosea fanya hivi fanya hivi.
Mwee Jamani mama yangu upumzike kwa amani, alikatika kama glass ghafla eti moyo valvu ziliachia🙁🙁🙁🙁

Nilijua nipo peke yangu mm naongea nae vizur na ananiambia mwanangu usijali mm bado naishi nikamwambia basi bora tubomoe lile kabur kumbe bado ww n mzma akaniambia wala usijal wacha watu wajue nmefarik lkn mm bado mzma mwsho akalishika tumbo langu akasema nipo karibu yako
 
Mkuu mtani nilikua nasoma hadithi usiku inayohusu joka chatu afu usiku huo nikaota amenigonga maeneo ya mgongoni na nilipata maumivu sana akaniachia sumu nyingi niliposhtuka nilikua nimechoka sana sasa nashindwa kuelewa je ni mawazo ya ile hadithi au nini nisaidie hapo mtani mshana
 
Mkuu mtani nilikua nasoma hadithi usiku inayohusu joka chatu afu usiku huo nikaota amenigonga maeneo ya mgongoni na nilipata maumivu sana akaniachia sumu nyingi niliposhtuka nilikua nimechoka sana sasa nashindwa kuelewa je ni mawazo ya ile hadithi au nini nisaidie hapo mtani mshana
Ni fikra zilitengeneza uhalisia halafu zikawa ndoto
 
View attachment 421080Ni usiku mwingine tena tunapojiandaa kupumzika vitandani mwetu ( hata kama ni ugenini gesti house au barabarani kuna dakika chache utalala kidogo na kuota)
Ndoto njozi na kuota ni hitaji la kawaida la mwanadamu, shida ipo ni je unaona ndoto za aina gani?

-unaota ndoto za kawaida kutokana na harakati za kawaida za kimaisha kutokana na fikra mawazo matendo na maono?

-Ama la unaota ndoto taarifa au ndoto ujumbe au ndoto maono? Ndoto zenye ujumbe maalum?

- Au je unaota zile ndoto zile ambazo si ndoto bali ni matendo ya giza? Ndoto za
Kuota umelazwa kwenye jeneza
Kuota unazama/unazamishwa baharini
Kuota unakula/unalishwa nyama

Kuota unang'atwa na mdudu na unapata maumivu mpaka asubuhi
Kuota unakimbizwa au kufukuzwa
Kuota umefungiwa kwenye kiota chupa nk
Ndoto zote hizi huwa live mpaka asubuhi au unapostuka na unakumbuka kila kitu saa nyingine hata uchovu maumivu na Ladha....!

Ndoto za namna hii si ndoto za kawaida na huambatana na mambo yako mengi kuharibika! Hizi ni ndoto za kufanyiwa mambo mabaya na watu wabaya
Ukiweza jitahidi kuchunguza ndoto zako leo na siku zijazo utagundua kitu View attachment 421088
Habari,ni Mara ya kwanza kukuona nimefurahi kwakuwa ktk watu wanaoongoza kwa kuota nahisi naongoza duniani:Nina maswali Mengi ambayo sijawahi kupata ufumbuzi:kwa Leo naomba nisaodie kutafsiri hii ndoto:kuna siku niliota nipo shule ya msingi ambayo nilisoma miaka mingi sana,nipo kwenye uwanja Fulani hv sasa ghafla nikamuona Simba dume nikaogopa sana,nikajitengenezea fensi zile za seng'enge haraka nikawa ndani ya fensi Simba nje,ghafla àkaja Mdogo wangu wa kiume ameshikilia bahasha ya kaki mkononi akaruka fensi akaingia ndani,nikashangaa amepitaje huko nje wkt kuna Simba?
Wkt nashangaa Mara nikamuona yule Simba nae kaingia ndani ya fensi bila kujua kapitia wapi,basi akaanza kutukimbiza tulikimbia sana huku namwambia Mdogo wangu akazane ni heri Simba anile Mimi lkn asimle yeye.nikashtuka ghafla.kuangalia saa ilikuwa SAA 8 usiku.je maana Yake nini hyo ndoto?
 
Daah, Nimepitia michango ya members wengine na hakika kuna mengi ya kujifunza. Ki uhalisia nimeumbwa kwa roho ya chuma na nimekutana na mengi katika maisha haya. Ki ukweli ndoto nyingi nazoota huwa zinatokea na hii huwa inani disturb sana ingawa napotezea tu. Siku moja nilikuwaa Nchi za watu (Ugenini) nikaumwa sana na kulazwa na sikuwa na ndugu/rafiki wa karibu wa kunihudumia. Usiku nikaota napata ajali mbaya ya ghali, nikashituka sana na kuamka nalia. kwa kuwa ilikuwa usiku wa manane, Mwuguzi wa zamu alinisikia na kuja kunifariji. kesho yake nikapigiwa simu na rafiki yangu ambaye ni mfanyakazi wa WFP-Tanzania kuwa ameota nimefariki.....

Mkuu mshana jr, Hii inamaanisha nini?
 
Hakuna kitu nsichopenda kama vile, unaota Ndoto nzuri wala haijaisha mara umeamshwa
 
Au unaota umo kwenye Ulimwengu wa Kugegedana.

Mara unastuka Bao lote umelimwaga kwenye Shuka na kwenye Nguo ya kulalia.

Kwa kweli ni Adha inayopitiliza kikomo
 
Mkuu Mshana Jr Heshima yako chief.

Nimeota usiku wa kuamkia majuzi (wiki hii hii),..Ni Mara ya tatu kama sio ya pili.
Nilianza kwenda na jamaa mahali (sura simfahamu) tukaelekea poroni kama vile kuna kitu tunaenda kukufuata tulikua na piki piki.Gafla likatokea basi Moja ivi likasimamishwa na wanajeshi wakasema Luna jambazi humo mpo chini ya linzi Mimi nilikua Katibu na basi hilo nikajitupia kwenye mitaro hii ya pembeni ya Barbara",.. Mmoja wa wale wanajeshi wakiwa wanatangisha basi akaniona akaanza kunilenga kwa risasi,.. nikainua mkono kuashiria sins kosa ila alizidi kunimiminia risasi hizo (nilikua sijeruhiki) hakuna aliyenitetea hata kwa kusikitika huku nafsi ikijawa na hofu na maumivu,..

Nikaona nisimame akanilenga za kichwa (bado nilikua sijeruhiki) Punde baada ya risasi hizo likatokea gari Moja likanibeba kunipeleka mbali (walionibeba hata siwafahamu) tukaenda mbali gafla wakatokea wengine wakimsaka mtu wao ila wakiniona mm wananitaka, kutokana na wale watu wakawa wananiacha,.. ivo ivo kwenye barrier zingine adi nikavuka nikaenda sehemu salama nikashuka nikiwa na furaha kwa kiasi chake.
Sijui itakua INA maana yoyote maana nimeota Mara ya tatu hivo hivo bila kubadilika kitu.
 
Mimi niliwahi kuota hivi,kuna jirani yetu alikuwa na kijana wake sasa yule kijana ile siku ikatokea akawa anampiga sana mtumishi wao wa ndani na yule mtumishi akawa anapiga kelele sana,ikanibidi nitoke kwenda kumsaidia ila nkiwa njian nkapita sehemu palikuwa na wadudu wengi sana na miongoni mwao walikuwa ni nyoka na hapo ndipo nyoka mmoja akaniuma mguuni na katika ndoto ile wala mimi sikujali nikaendelea na safari yangu ila nkiwa na kumbukumbu kwamba nyoka kaniuma!!
Mpaka nilipostuka nilikuwa bado naikumbuka ndoto hiyo japo ckuwa na maumivu yoyote,je inawezakuwa ilimaanisha nini!?@Mshana jr
Nyoka alikuwa wa rangi gani? Na hao wadudu wengine walikuwa ni wadudu wa namna gani?
 
Au unaota umo kwenye Ulimwengu wa Kugegedana.

Mara unastuka Bao lote umelimwaga kwenye Shuka na kwenye Nguo ya kulalia.

Kwa kweli ni Adha inayopitiliza kikomo
Wet dreams! [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Back
Top Bottom