mshana jr kuna ndoto hizi,
1. Nikiota nimekutana na Nyoka hasa akikatiza mbele yangu au akinipitia miguuni basi kesho yake huwa napata Pesa.
2. Kuna siku nililala chali ghafla nikaota mtu nisiyemuona sura yake anataka kunifyeka na panga (nikiwa nimelala vile vile chali), ilelinakaribia tu kutua shingoni nikalikwepa, sasa ule uelekeo niliokwepea ndo ukutani, nikajibamiza pale na nikatoka jeraha kubwa kiasi (huyo mtu nimemuota kwenye ndoto,lakini tukio la kukwepa panga liliambatana na kufumbua macho na kujibamiza ukutani). Kesho yake kwenda hospital nikatunga uwongo wa kujieleza.
NB; Hii ilikuwa kijijini kwetu Msowero, Kilosa, Morogoro
Pia niliwahi kusikia tetesi kwamba watu wananiogopa wakidai mimi mchawi wakati sijawahi kufanya tukio lolote la kichawi, Binafsi naona wananiheshimu tu, ila kuna mzee alishawahi kunionyesha kitendo cha kichawi lakini nikamwangalia tu bila uoga wala kubabaika na sikumwambia kitu nikaondoka kimya kimya na mpaka leo nikienda huyo mzee akikutana na mimi njiani lazima anisalimie.
Pia kuna hizi ndoto za kuchafua shuka nataka niziepuke maana nimejaribu kufuata taratibu za LUCID DREAMING lakini mimi nalala masaa matano tu