Namaanisha mahusiano katika ndoto kati mtu aliye hai na aliyekufaa, sio mahusiano bora kwa ustawi wa aliye hai kama aliye hai anataka kuishi kwa misingi ya KIMUNGU, lakini kama anataka kuishi kwa misingi mingine sina neno.
Kama wewe ni mwamini na unamkiri kristo kuwa kiongozi wako katika maisha, huo ni uhusiano mbaya na haukusaidii kwani utapunguza nguvu yako kumtumaini MUNGU.
Lakini pia jambo hili halitakiwi kukutisha hata kidogo, ila ni sehemu tu ya kukupa ufahamu nawewe uanze kutafuta ukweli huu ambao kama utafanya bidii baada ya muda utajua hiki nilicho kiandika.
Kimsingi hutuishi mwilini tu, tunaishi rohoni kwanza then mwilini, hivyo mahusiano ya rohoni ambayo yanaweza kuwa yanaongozwa na MUNGU au shetani kupitia wajumbe wake ndiyo huamua maisha ya mtu ya mwilini yaonekanaje, ndoto ni sehemu ya taarifa tu kuonyesha unavyo ishi rohoni.
Kwanini nimesema sio jambo la kuogopa! kwasababu watu wote tunaishi rohoni kwa msaada wa hizi nguvu mbili either Mungu au Shetani hivyo nijambo ambalo lipo tuu penda usipende, sasa mtu akiamua kuishi KIMUNGU ndoto kama hizo sio mahali pakee kwani MUNGU anazo njia zakukuletea taarifa unahisi inakufaa kuliko kutumia wafu.
Ndiyo maana nikasema ni jambo la maamuzi kidogo na sio la lazima kwani linahitaji utashi wa mtu mwenyewe ili ujiweke kwenye nafasi ya kukataa hizo ndoto, yawezekana unajisikia faraja kuota hivyo, na kwa kiasi furani moyo unafarijika ukihisi umeongea na mtu uliyekuwa unampenda tena sana, hivyo sio rahisi leo mtu anakwambia kemea ni uhusiano mmbaya, unahitaji tafakari na kuona huo ubaya ninao usema. Ukitaka kuwa upande wa MUNGU tafuta maarifa utajifunza vitu vingi kupitia ndoto, vipo vitabu vinauzwa mitaani vya kidini lakini, pia ukipita kwenye mitandao kuna elimu nyingi ya ndoto na utajifunza sana.
Ukipata maarifa ni rahisi kushinda kila kitu, na ni rahisi kuamua uwe upande upi