Hizi sio ndoto za kawaida

Hizi sio ndoto za kawaida

Mkuu mshana mimi nimeota hivi majuzi tu, ilikua hivi,
Nikiwa kwenye kituo cha daladala, ghafla akatokea mama mmoja akanishika kidole gumba cha mkono, nikashituka na kutaka kukimbia, lakini akanituliza na kuniambia nisimwogope Kwani anataka kunitoa mdudu kwenye kidole changu, kugeuka na kumwangalia kumbe ni mama jirani yetu ninaye mfahamu, baada ya kubinya kidole changu na kweli akatoka mdudu ambaye sikumuelewa ni mdudu wa aina gani, baada ya kubinya kidole changu kikabadilika kikawa na mwonekano wa mdudu pamoja miguu kabisa, na nikaanza kuhisi maumivu, lakini Ile hali haikunitisha hata kidogo
NB: mimi huwa sina Kawaida ya kuota ndoto za kutisha, lakini hii ndio imenitatiza sana, sasa mkuu mshana sijui ina maana gani hii ndoto.
Ototo usiku una mengi yasiyo na tafsiri kwenye ulimwengu wa kawaida kuna wakati tunaota ndoto ambazo si ndoto za kawaida bali michezo ya wanga na walozi tuwapo usingizini! Nyingi ya hizi ndoto hazina madhara lakini zinaleta usumbufu
 
Baadhi ya ndoto tafsiri yake ni kinyume
Kwa kawaida mwanadamu hutembea kwenda mbele sio kinyume nyume kama kifurukobe


Nilipokuwa jeshini niliwahi kuota kuwa kuna jiwe kubwa linaniangukia usoni. Kustuka nikakuta ni tone la maji toka darini limeniangukia usoni. Mpaka leo sijaweza kuhusisha hivyo vitu viwili.
 
Nilipokuwa jeshini niliwahi kuota kuwa kuna jiwe kubwa linaniangukia usoni. Kustuka nikakuta ni tone la maji toka darini limeniangukia usoni. Mpaka leo sijaweza kuhusisha hivyo vitu viwili.
Ni sawa na zile ndoto za kuanguka kwenye kina kirefu kumbe ni udenda lakini hiyo yako jicho la tatu hufunguka uwapo usingizini na kama picha ya kitu chochote inapokaa katikati ya macho huonekana ni kitu kimoja kikubwa
 
Ni sawa na zile ndoto za kuanguka kwenye kina kirefu kumbe ni udenda lakini hiyo yako jicho la tatu hufunguka uwapo usingizini na kama picha ya kitu chochote inapokaa katikati ya macho huonekana ni kitu kimoja kikubwa

Issue ni kwamba nilikuwa usingizini na macho yamefunga sasa fahamu ilijuaje kuwa kuna tone la maji linaanguka?
 
Fahamu kupitia jicho la tatu ndio huona ndio maana tunashauriwa tusilale chali
what and sababu ya kutolala chali??!! maana mie mkinga huwa nalala chali na huku nimepandanisha miguu kwa style ya kukunja 4.. umenistua mshana
 
Fahamu kupitia jicho la tatu ndio huona ndio maana tunashauriwa tusilale chali


girl-running-away-clipart-74058338.jpg
 
Mimi huota ninakimbizwa,huwa ninastutaka usingizini ninapokaribia kukamatwa.
 
what and sababu ya kutolala chali??!! maana mie mkinga huwa nalala chali na huku nimepandanisha miguu kwa style ya kukunja 4.. umenistua mshana
1476936691754.png
Dunia ni duara na anga liko juu huku tukiishi kwenye nguvu ya uvutano, dunia ina pande kuu kumi ambazo zote zinashikiliwa kwenye mhimili wa kati
Paji la uso ndio penye njia ya jicho la tatu unapolala chali ni kama unauangalia ulimwengu kupitia mhimili wa kati kuelekea angani ambako huko angani kunapita vitu vya kila aina vinavyoonekana na visivyoonekana vizuri na vibaya
Ni katika hali hiyo ya usingizi jicho la tatu likinasa jambo zuri utaota ndoto nzuri au usiote kabisa lakini kama ni jambo baya basi ndoto zitakuwa za kutisha sana
1476936682455.jpg
lakini kwa style yako hiyo ya kukunja nne huko sio kulala chali
 
Back
Top Bottom