Hizi ni kura za Lowassa

Hizi ni kura za Lowassa

Naomba mchanganuo KAMA CHARITY BEGINS AT HOME nielezwe kwa miaka 25 EL akiwa mbunge wa monduli kuna upungufu wa umaskini kiasi gani au maendeleo kiasi gani ukilinganisha majimbo mengine?

Swali zuri mkuu, niliwauliza siku moja baadhi ya wamasai wa kule mbona hamkubali upinzani huku ? wakajibu sisi tunashida gani, baba etu imetupa kila kitu, maji imejaa kule, ngombe haipati tabu, hakuna nshaa (njaa) ya kutisha ..sasa upinsani utaleta nn tena..labda ilete gari kwa kila mtu !!!
 
Naomba mchanganuo KAMA CHARITY BEGINS AT HOME nielezwe kwa miaka 25 EL akiwa mbunge wa monduli kuna upungufu wa umaskini kiasi gani au maendeleo kiasi gani ukilinganisha majimbo mengine?

Mimi sijazaliwa monduli ila nimekulia Monduli nimeishi pale kwa miaka 15.
1. Monduli barabara ni nzuri, monduli mpaka arush mjini ni mkeka mtupu... barabara za lami katikati ya wilay na nje ya wilaya. barabara nyingi zinapitika.

2. Maji. Miaka ya 90 monduli kulikuwa kuna shida kubwa ya maji. mm kipindi hicho kulikuwa na mabomba ya vijiji... yaan ilikuwa inabidi mtu atembee umbali mkubwa kwenda kuchota maji kwenye mabomba ya vijiji ambayo yalikuwa machache na kuhesabika...

Ila sasa hivi dakika hii EL amesaidia visima vya maji vimechimbwa vile vile amesaidia kapeleka maji kayatoa Meru, Meru ni mbali sana. maji hayo yanasaidia mpka maeneo ambayo yapo nje ya jimbo. sasa watu wengi wana maji mpaka majumban kwao hakuna tena matesao ya kutembea umbal mrefu.

3. Elimu. EL amekuwa mlezi mzuri wa chuo cha ualimu monduli, waliosoma pale mashahidi.
EL amewalipia ada za shule watoto wengi wasiojiweza.
EL alisaidia kuanzisha Chuo cha ufundi monduli FDC,
EL alisaidia sasa hivi kuna chuo cha CDTI
kwenye jimbo la EL kuna shule nyingi za msingi na sekondari kiasi cha kutosha kushinda majimbo mengi tu
na mengine mengi

4. umeme.. umeme sasa sio shida maeneo yote muhimu na mengi yenye makazi ya watu kuna umeme.

5. Afya. Monduli hospital zipo zahanati pia zipo za kutosha... majuzi tu hosp ya wilaya ya monduli imepandishwa hadhi na kuwa hospt ya rufaa kama KAMA SIKOSEI.. Ila nina uhakika imepandishwa hadhi.

6. Ufugaji..Monduli ni moja ya maeneo machache niliyoona maafisa mifugo wapo active kwa kiwango kikubwa.
EL amesaidia ujenzi wa mabwawa na majosho wamasai wa monduli haswa lashaine ni mashaihid wengi wamenufaika na moja ya mabwawa lililojengwa jiran na sehem nliyokua nikiishi.

mkuu kama una swali uliza ntakujibu kulingana na xperirnce yangu ya monduli chini ya uongoz wa mh. EL
 
Mi baba mwenye nyumba hapa amekunywa maji ya bendera. Kila siku asubuhi lazima amtukane lowasa. Lakini hamna shida maana hii kura yake moja ntaifidia mimi.
 
Mimi nina uwezo wa kuvishawishi vitongoji viwili vyenye wapiga kura zaidi ya 250.
 
Mkuu usijali ccm tunaitoa madarakani misa ya kwanza asubuhi tu ccm imechokwa na kila mtu safari hii adi vijijini
 
H20

Hongera ndugu tuko pamoja sana.kama ilivyo kawaida sasa hiwe zaidi kampeni ya mtu kwa mtu .ccm out 2015 nilazima
 
Last edited by a moderator:
Sie tuna group la ukoo whatsap.Tumejihamasisha Watu kama 40 wanapiga kura kwa Lowassa& ukawa.Hapo ukiondoa wafanyakazi wao na majirani!
 
Nilifurahi Sana Jana jamaa Mmoja aliposema kuwa Mzee Lowassa amemaliza kuzungumza kesho turuhusiwe kupiga kura ukizingatia kuwa tumechoshwa na magamba! Nikamuuliza na wewe unafahamu gamba? Akasema ndiyo, akaendelea kusema hawa hawasumbui kwani alfajiri October 25, 2015 tutawapigia kura ya hapana. Shauku yake kubwa ni kuona msingi imara kwenye mfuma imara wa kuaminika unajengwa. Na hakika Lowassa ndiye jiwe juu la pembeni ambalo washi waliukata ambapo msingi imara wa haki, uwajibikaji na utawala wa sheria utanjengwa na baada ya hapo nchi hii itarudi kwenye msitari wa haki aliouwacha Mwalimu.
 
mi mwanzo nilijua watu humu ni great thinker kumbe ni mijitu mishabiki tu isiojua kuchuja mambo yapelekwa na ulevi wa siasa na pesa sasa mjifariji na ndio mwisho wa chadema yenye nguvu mwaka huu because of money mmewabetry waliokua na mapenzi ya dhat ya chama mmewaleta wataka madaraka mkishindwa mtajuta tuone nani atakijenga chama kisichoaminika
 
Me nawaimbisha nikianza na wazazi wangu...wakizingua kujifanya CCM naficha kadi zao za kura wasipige kabisa

Mkuu mkuu hahahaha asantee.... Bonge la technique... Hapo lzm wasandeee!!!
 
Ni kweli, ingawa sheria haimkatazi mtu yeyote kuisema hiyo siri yake, as long as ni kwa mapenzi yake mwenyewe bila kulazimishwa na mtu yeyote.

Usemelo ni sawa kabisa. Mi ninachosema ni kuwA mtu anaweza akakwambiaa hivo ila kwenye chumba cha kupigia kura huko ndo yanaweza yakatokea mabadiliko.
 
Vizuri ila inatakiwa kama umewaelimisha watu 12 na hao kama wataweza kila mmoja akawailimishe watu kumi na mbili 12×12=144 natena hao 144 wakahaelimishe kila mmoja watu 12 kila mtu mpenda mabadiliko kama atajitole kutoka moyoni kuwaelimisha watu wote wenye mioyo migumu wakaelewa itafikia wakati kila mtu atakuwa anaelewa ccm ni ugonjwa hatari sana zaidi ya ebola kwahiyo kwa kupitia hilo nchi yetu lazima tuikombe
 
Kulikuwa na vitongoji 63000 (sensa ya 2012) Kwa sasa kuna mitaa na vitongoji vilivyoongeza takwimu sijaipata. Ikiwa sisi wa UKAWA tutahakikisha kwa kila kitongoji tunapata watu 30, na kila mtu ashawishi watu 15 ambao kwa ushawishi wake 80% watapigia UKAWA kura, basi, ushindi ni LAZIMA. Tufanye kazi hiyo tuuondoe huu mfumo uliochoka.
 
Back
Top Bottom