Hizi ni kura za Lowassa

Hizi ni kura za Lowassa

H20

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2013
Posts
341
Reaction score
170
Wadau kwa moyo wa dhati kabisa tangu Mh Edward Ngoyai Lowassa ajiunge na UKAWA nimefanikiwa kutoa ushawishi kwa watu 12 waliokuwa hawana mpango wa kupiga kura na wakakubali kuwa watapiga kura na kumchagua EL through CHADEMA na UKAWA kwani walikubaliana nami kwamba wamepigika.

Nilitumia vigezo vya uhaba wa maji, elimu duni, gharama za matibabu na issues za ufisadi wa escrow nikawatajia figures mbona wamepata hasira na chama chakavu? So in short, home kwangu kuna kura 3 ukiongeza hizo 12 nitakuwa na mtaji wa 15 (wote wamejiandikisha).

Kama kweli tunahitaji mabadiliko wako watu wasiojua umuhimu wa kura na wengi wamepigika ila hawajui kwanini kupiga kura. Hebu angalia vijana, wazee wa kijiweni, house girl wako, mafundi magari, wafanya biashara wa vigenge, wasukuma mkokoteni na wengineo hao wote waimbishe watakuelewa (Sina maana kuwa hao niliowataja hawajui ila wapo baadhi yao wako bize na mambo yao hawahangaiki na mambo ya uchaguzi).

Mimi naendelea na kazi ya kuwaimbisha waichinje CCM.Wewe je?
 
...pamoja tutashinda mkuu hongera ...
 
Sawa kura ni siri ila kumshawishi mtu akakuelewa na kubadilisha muelekeo yaonesha matumaini katika kile unachopenda afanye. Ila nimefanya jitihada kuongeza kura mkuu hata kama hao 12 watapiga kura nina uhakika wa zaidi ya 75% watapiga kule nilikowashawishi kwani hawakuwa na mpango wa kura.
 
Kwahiyo unataka kutuambia kuwa kuna watu 12 waliojiunga na kundi la hao nyumbu wasiojua wanapoelekea?
 

Attachments

  • 1438719601355.jpg
    1438719601355.jpg
    33.3 KB · Views: 1,025
H20

Kwani mwaka huu kura za urais zitahesabiwa kwa mtindo wa TV ya taifa live kila mtu akiona jinsi zinavyoongezeka au ni siri? Maana wkt wa slaa walipoona wanashindwa, walitafta sababu eti mfumo umezidiwa data toka mkoani, mpaka leo matokeo ya urais sijayaona. Ngoja nichek labda wamesha weka matokeo ya urais 2010
 
Last edited by a moderator:
H20

Cha mtoto hiyo, hapa Dar nina uhakika wa kura 29 za uhalali through Chadema na Arusha vijana wangu wanazo karibia ya 100 pamoja na majina na namba za simu za wakereketwa kwani ilibidi niwapigie kuwauliza. I am sure hata tume ya mawasiliano ya kudaka maongezi ya watu binafsi through simu wanaweza kuhakikisha hii. Yes, I'm working diligently kuiua CCM, so what? Hawa wasanii wa CCM wako tu pale kwa ajili ya kuifilisi nchi na kujinufaisha wao wenyewe.
 
Last edited by a moderator:
Ukawa wamebeba kirahisi sana,messi kabadili matokeo dk za majeruhi...
 
Hapa home Lowassa anakura 5 kati ya 6 na wote wana BVR. Kuna mtu mmoja tu cjui alikuanywa maji ya bendera ni mbishi balaaa
 
Naomba mchanganuo KAMA CHARITY BEGINS AT HOME nielezwe kwa miaka 25 EL akiwa mbunge wa monduli kuna upungufu wa umaskini kiasi gani au maendeleo kiasi gani ukilinganisha majimbo mengine?
 
H20

Mimi nimewashawishi wazazi wangu kutokana na makatizo na majanga ya umeme na wamekubali na tena uzuri mmoja ni wazee kwa hiyo watahitaji msaidizi ni mimi kwenye maupigaji ya kura lazima nihakikishe LOWASSA.
 
Last edited by a moderator:
Nina wadada wakazi wawili na shamba boy mmoja wote nimewapeleka kuwaandikisha na wote nimewapa maagizo ya nani wa kumpigia sio mwingine bali ni lowassa so hizo tatu plus mume wangu na wazazi wangu na wakwe zangu na mawifi wote kura ni kwa lowassaaaa...nahamasisha pia maids wa marafiki zetu walijiandikisha wakampigie lowassa...mwaka huu ushindi ni wetu!! Peoplessssss
 
Mimi nilielewesha familia yangu yote kwa ujumla tupo 8, wote walinielewa na wakaenda kuchukua vichinjio vyao BVR tayari kwa kuipoteza CCM...
 
Back
Top Bottom