Hizi ndio sababu huwa sitaki kuwaweka ndugu kwenye biashara zangu, Ni heri niwape mitaji wafungue biashara zao wapambane kivyao !!

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,033
Biashara ntashirikisha familia yangu niliyoijenga (hasa watoto) ama familia niliyotokea (kaka, dada, wadogo zangu, wazazi), nje ya hapo hawa watoto wa mjomba, ma mkubwa, ba mkubwa, ba mdogo, ndugu flani, n.k. sidhani kwakweli, undugu uwepo na ninaweza kuwasaidia mitaji ama kuwasimesha pamoja na kuwa mteja wa biashara zao lakini tusiingiliane kwenye usimamizi wa Biashara zangu

Unakuta wafanyakazi wengine wanafika saa moja asubuhi ndugu anafika saa mbili ama tatu, Ndugu akiumwa hata mafua anaweza asije kazini, hii inanijengea chuki kwa wafanyakazi wengine kwa kuona nina upendeleo wa wazi wazi.

Kuna ndugu wanajikuta wao mabosi kuwa sawa na mimi kisa tu tuna undugu, wanapitiliza kuanza kuwavimbia wafanya kazi wengine, huanza kujiona miungu watu kwa wafanyakazi wengine, hawa ndugu wa kiume baadhi yao huanza kutumia nafasi hii kuwanyanyasa kingono wafanyakazi wa kike

Ndugu hasa wasio na majukumu wanaanza kunichora kwamba naingiza pesa nyingi, maneno yanaanza kupelekwa vijijini kwamba naingiza pesa nyingi lakini siwasaidii kwa uwiano wa kiasi nachoingiza, hapo hawajui kwamba nalipa marejesho ya mkopo, nalipa kodi, nalipa mishahara, nalipia ulinzi, n.k.
 
wafanyakazi wengine wanafika saa moja asubuhi ndugu anafika saa mbili ama tatu na hatea kazini anatoka toka, hii inanijengea chuki kwa wafanyakazi wengine kwa kuona nina upendeleo wa wazi wazi...
Ndugu ndiyo inatakiwa awe mfano bora kazini.

Huyo ambae hana nidhamu na kazi hata kupewa msingi hafai, labda iwe umeamuwa kumpa sadaka zako tu, azifanyie atakavyo yeye.
 
Mkuu inategemea mtu na mtu mfano nina mdogo wangu anasimamia mradi wangu mahali yule dogo aiseee anabidii na anauchukulia mradi kama wakwake na tayari mipango imeshaiva kwamba nitahakikisha namkatia kipande na yeye aamze kumiliki vitu vyake.

Hivyo inategemea na mtu anawaza nini na anayatafsiri vipi mazingira pamoja na uelewa wake kuhusu biashara au mradi husika na jinsi ya kuundesha
 
Mkuu inategemea mtu na mtu mfano nina mdogo wangu anasimamia mradi wangu mahali yule dogo aiseee anabidii na anauchukulia mradi kama wakwake na tayari mipango imeshaiva kwamba nitahakikisha namkatia kipande na yeye aamze kumiliki vitu vyake.
Hivyo inategemea na mtu anawaza nini na anayatafsiri vipi mazingira pamoja na uelewa wake kuhusu biashara au mradi husika na jinsi ya kuundesha
Huyo ni mdogo wako ni mwanafamilia sio ndugu
 
Biashara ntashirikisha familia yangu niliyoijenga ama familia niliyotokea, nje ya hapo hawa watoto wa mjomba, ma mkubwa, ba mkubwa, ba mdogo, ndugu flani, n.k. sidhani kwakweli.

Unakuta wafanyakazi wengine wanafika saa moja asubuhi ndugu anafika saa mbili ama tatu, Ndugu akiumwa hata mafua anaweza asije kazini, hii inanijengea chuki kwa wafanyakazi wengine kwa kuona nina upendeleo wa wazi wazi.

Kuna ndugu wanajikuta wao mabosi kuwa sawa na mimi kisa tu tuna undugu, wanapitiliza kuanza kuwavimbia wafanya kazi wengine, huanza kujiona miungu watu kwa wafanyakazi wengine, hawa ndugu wa kiume baadhi yao huanza kutumia nafasi hii kuwanyanyasa kingono wafanyakazi wa kike

Ndugu hasa wasio na majukumu wanaanza kunichora kwamba naingiza pesa nyingi, maneno yanaanza kupelekwa vijijini kwamba naingiza pesa nyingi lakini siwasaidii kwa uwiano wa kiasi nachoingiza, hapo hawajui kwamba nalipa marejesho ya mkopo, nalipa kodi, nalipa mishahara, nalipia ulinzi, n.k.
Uko sahihi kabisa,kwani wewe ulipewa huo mtaji si washukuru wanapo hata pa kuanzia!
 
Mkuu inategemea mtu na mtu mfano nina mdogo wangu anasimamia mradi wangu mahali yule dogo aiseee anabidii na anauchukulia mradi kama wakwake na tayari mipango imeshaiva kwamba nitahakikisha namkatia kipande na yeye aamze kumiliki vitu vyake.
Hivyo inategemea na mtu anawaza nini na anayatafsiri vipi mazingira pamoja na uelewa wake kuhusu biashara au mradi husika na jinsi ya kuundesha
Mpe maua yake!
 
Usifanye hiyo mistake kwani ndugu ndo chanzo Cha utajiri wa familia kudumu ila inavyoonekana Bado hakuna mstari unaotenganisha biashara na undugu ndo maana ndugu wanabweteka .
Fanya kikao Cha menejimenti na haya muyazungumze maana mawasiliano ni Tiba Bora na majukumu na uwajibishaji viwe ktk ajenda ila ndugu SI wa kuwatupa
 
Tumetofautiana, Kuna jamii zipo hata vijijini hawarudi labda mpaka baba afariki, mfano hapa kuna makabila ya Ruvuma, hizi jamii huwezi hata kuwajua ndugu aisee,
Mara ya mwisho kuonana na Ndugu Ni mwaka 2011 Nikiwa form one baada ya wao kunizuia nisiendelee na shule. Nikapambana huku namtanguliza Mungu, nikamaliza University, nikapata kazi sasaiv Nina maisha yangu na Sina habari nao. Huku Nimenunua kiwanja ambacho nimeandika waraka in case nikifa ghafla mwili wangu utazikwa hapa bila kuitwa Ndugu
 
Mara ya mwisho kuonana na Ndugu Ni mwaka 2011 Nikiwa form one baada ya wao kunizuia nisiendelee na shule. Nikapambana huku namtanguliza Mungu, nikamaliza University, nikapata kazi sasaiv Nina maisha yangu na Sina habari nao. Huku Nimenunua kiwanja ambacho nimeandika waraka in case nikifa ghafla mwili wangu utazikwa hapa bila kuitwa Ndugu
Kwenu wapi ?
 
Back
Top Bottom