Hizi kodi zinalipika vipi jamani?

Master Legendary

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
550
786
TRA kuweni serious !

Kwenye Mshahara wangu wa mwezi nakatwa kodi na madudu mengine karibu nusu ya Mshahara kabla sijaupokea, nafungua Biashara mnataka Kodi kabla sijaanza,Mwenye Nyumba ya Biashara anataka Kodi kabla sijaingia.

Mwenye Nyumba ya kuishi anataka kodi kabla sijaingia,Manispaa wanataka kodi ya Leseni na Kodi ya Ushuru wa huduma kabla sijaanza Biashara.

Osha wanataka Kodi,Zimamoto Kodi,Wakusanya taka Kodi,Sungusungu Kodi,nk

Manunuzi yoyo te ninayoyafanya hata kama nakunywa soda nalipa Kodi.

Ukigeuka huku kuna Kodi ya Ardhi,jengo,sijui na vitu gani!

Bado Mamlaka zina yake sijui kupima Afya wafanyakazi Kodi,kulipia Leseni za Taaluma Kodi.

Bado Maafisa wa Serikali wanataka Kodi za Familia zao kila wakija kukukagua.

Hizi Kodi zinalipwa vipi jamani!Hata mtu akishindwa au akikwepa analaumiwaje?Ni biashara gani utafanya uweze kulipa utitiri wa kodi zote hizi bila kufilisika?

Serikali haioni tatizo ikaja na Mamlaka na Sheria moja tu ya kukusanya Kodi ukilipa umemaliza vyote?
 
🤣🤣🤣🤣 Umenikumbusha kunakipindi nilifungua biashara, Tena enzi hizo watu wanaendesha biashara hata leseni hawana na maisha yanaenda tu. Mimi nikajifanya nimeelimika lipa Kodi bila shuruti, chapu huku nishaipata fremu nikaenda manispaa kukata leseni.

Pale kwenye leseni wakaniambia nipambanie Tin namba kwanza, kweli nikasogea TRA nipo moto kweli. Basi nikakadiriwa na Kodi nitakatopaswa kulipa Kwa mwaka japo itakuwa Kwa hawamu. Nikafungua biashara miezi sita biashara ya moto naiendesha Kwa hasara.

Nikaona hapa nitapoteza mtaji Bora niifunge kwanza. Niliposogea TRA kwenda kusitisha biashara nikaambiwa andika barua kwenda Kwa Meneja.

Baada ya wiki tatu nikaambiwa nikachukie barua yangu meneja ashanijibu, Ile nafungua ndani naambiwa nadaiwa 180000 Kodi ya miezi sita. Nikamfuata meneja nikamwambia hivi kama ningekuwa napata faida biashara ningeifunga kweli? Kwa hiyo mnataka kula mtaji wangu?
 
......ndo ivo mkuu ukitaka walau upumue inabidi uwe machinga, ukijiroga tu uweke kafrem hata kama ni ka mbao, TRA hawa hapa na taasisi zingine, ukiweka kifrem unaonekana tajiri hata kama unauza biskuti mbili....BTW tulipe Kodi kwa maendeleo ya taifa.......
 
Nchi ya makusanyo hii,tunakamuliwa Kodi wanene wanajichana na kuzipiga bila huruma,
Na mikwara na vitisho tunavipata
 
Hii issue ni hatariii sana kwa afya ya uchumi wetu. Binafsi nimehonga maafsa mpaka nimechoka sasa ila sina namna... Walau wanachukua nusu na kuniachia nusu ila roho inauma sana.
 
Kulipa kodi sio vibaya ila ubaya hio kodi inakwenda kumfaidisha bepari peke yake tu. Watu wa chini hawapati maendeleo na kodi ya nchi
 
TRA kuweni serious !

Kwenye Mshahara wangu wa mwezi nakatwa kodi na madudu mengine karibu nusu ya Mshahara kabla sijaupokea,nafungua Biashara mnataka Kodi kabla sijaanza,Mwenye Nyumba ya Biashara anataka Kodi kabla sijaingia...
Marekebisho kidogo

TRA kama ni biashara za kawaida sio kwamba wanataka ulipo unapo anza bali wanataka wakukadirie.

Malipo ya Q1 mwisho ni 31 March kila mwaka

Malipo ya Q2 mwisho 30 June Kila mwaka

Na malipo ya Q3 mwisho ni 31 Dec kila mwaka

Hivyo kusema TRA wanataka kodi kabla ya kuanza biashara sio kweli
 
Karibu Tanzania, ukiweza kwepa,au nenda Msumbiji au Zambia na Malawi kafanye Biashara.

Hata Uganda kama una Mtaji wako unafanya Biashara za kutosha nenda kanunie Mahogany Red Wood kutoka DRC upeleke Uarabuni na Asia ukapige pesa ondoka huku Uswahilini.
 
Umenikumbusha kunakipindi nilifungua biashara, Tena enzi hizo watu wanaendesha biashara hata leseni hawana na maisha yanaenda tu. Mimi nikajifanya nimeelimika lipa Kodi bila shuruti, chapu huku nishaipata fremu nikaenda manispaa kukata leseni.

Pale kwenye leseni wakaniambia nipambanie Tin namba kwanza, kweli nikasogea TRA nipo moto kweli. Basi nikakadiriwa na Kodi nitakatopaswa kulipa Kwa mwaka japo itakuwa Kwa hawamu. Nikafungua biashara miezi sita biashara ya moto naiendesha Kwa hasara.

Nikaona hapa nitapoteza mtaji Bora niifunge kwanza. Niliposogea TRA kwenda kusitisha biashara nikaambiwa andika barua kwenda Kwa Meneja.

Baada ya wiki tatu nikaambiwa nikachukie barua yangu meneja ashanijibu, Ile nafungua ndani naambiwa nadaiwa 180000 Kodi ya miezi sita. Nikamfuata meneja nikamwambia hivi kama ningekuwa napata faida biashara ningeifunga kweli? Kwa hiyo mnataka kula mtaji wangu?
Meneja alikujibu vipi?
 
TRA kuweni serious !

Kwenye Mshahara wangu wa mwezi nakatwa kodi na madudu mengine karibu nusu ya Mshahara kabla sijaupokea, nafungua Biashara mnataka Kodi kabla sijaanza,Mwenye Nyumba ya Biashara anataka Kodi kabla sijaingia.

Mwenye Nyumba ya kuishi anataka kodi kabla sijaingia,Manispaa wanataka kodi ya Leseni na Kodi ya Ushuru wa huduma kabla sijaanza Biashara.

Osha wanataka Kodi,Zimamoto Kodi,Wakusanya taka Kodi,Sungusungu Kodi,nk

Manunuzi yoyo te ninayoyafanya hata kama nakunywa soda nalipa Kodi.

Ukigeuka huku kuna Kodi ya Ardhi,jengo,sijui na vitu gani!

Bado Mamlaka zina yake sijui kupima Afya wafanyakazi Kodi,kulipia Leseni za Taaluma Kodi.

Bado Maafisa wa Serikali wanataka Kodi za Familia zao kila wakija kukukagua.

Hizi Kodi zinalipwa vipi jamani!Hata mtu akishindwa au akikwepa analaumiwaje?Ni biashara gani utafanya uweze kulipa utitiri wa kodi zote hizi bila kufilisika?

Serikali haioni tatizo ikaja na Mamlaka na Sheria moja tu ya kukusanya Kodi ukilipa umemaliza vyote?
TRA hawana shida, kujieleza wanakusikiliza na kukishauri vizuri, shida ni leseni na kodi uchwara za halmashauri hawatoshewki na leseni, mara kodi ya taka halafu hakuna taka, mimi nafagia karatasi chacha na kuzichoma, bado kodi ya mabango kodi kubwa kweli, sasa watu wameamua kuondia mabango, sijui hawana tax consultant, inatoza bango kudi kubwa halafu watu wanaondoa mabango si bora utoze kodi ya elfu 15 ili watu wasishushe mabango waendelee kulipa kodi.
 
Bado Tozo ya 2000 kila laini ya simu itaanza , hapo luku unamlipia mwenye nyumba 1500 kila mwezi
sasa ndugu mtanzania kama hadi leo wapangaji hamjasort out suala la kodi ya jengo kupitia luku na mwenye nyumba, serikali ina haki ya kutunyonya tu, tuongezewe kodi zaidi
 
TRA kuweni serious !

Kwenye Mshahara wangu wa mwezi nakatwa kodi na madudu mengine karibu nusu ya Mshahara kabla sijaupokea, nafungua Biashara mnataka Kodi kabla sijaanza,Mwenye Nyumba ya Biashara anataka Kodi kabla sijaingia.

Mwenye Nyumba ya kuishi anataka kodi kabla sijaingia,Manispaa wanataka kodi ya Leseni na Kodi ya Ushuru wa huduma kabla sijaanza Biashara.

Osha wanataka Kodi,Zimamoto Kodi,Wakusanya taka Kodi,Sungusungu Kodi,nk

Manunuzi yoyo te ninayoyafanya hata kama nakunywa soda nalipa Kodi.

Ukigeuka huku kuna Kodi ya Ardhi,jengo,sijui na vitu gani!

Bado Mamlaka zina yake sijui kupima Afya wafanyakazi Kodi,kulipia Leseni za Taaluma Kodi.

Bado Maafisa wa Serikali wanataka Kodi za Familia zao kila wakija kukukagua.

Hizi Kodi zinalipwa vipi jamani!Hata mtu akishindwa au akikwepa analaumiwaje?Ni biashara gani utafanya uweze kulipa utitiri wa kodi zote hizi bila kufilisika?

Serikali haioni tatizo ikaja na Mamlaka na Sheria moja tu ya kukusanya Kodi ukilipa umemaliza vyote?
CCM MBELE KWA MBELE ACHA KULIA LIA
 
Meneja alikujibu vipi?
Aliniambia huo ndio utaratibu pambana ulipe hiyo pesa. Aisee, nikajaribu kuomba omba ushauri Kwa wadau wakaniambia Kwa sababu ushakuwa registered Kwa jina lako huko mbeleni watakuja kukukamata iwapo itafungua biashara nyingine. Tena utalipa na riba. Kiukweli niliilipa lakini sikuhizi naenda nao kiakili Sana
 
Back
Top Bottom