Hizi ishu za Mungu/Dini ni very complicated

Hizi ishu za Mungu/Dini ni very complicated

Kwanini usiseme hakuna uhakika wa kujua kama Mungu yupo au hayupo kwa sababu hakuna njia ya kuhakiki hilo? Wapo wenye mtazamo huo kwamba hakuna njia ya kujua ya kuweza kuthibitisha uwepo wake ila wewe unakimbilia kusema hayupo.

Hizo sifa tofauti za Mungu hazitoi hitimisho la kuwa hakuna Mungu.
Sina sababu ya kusema hakuna uhakika, kwa sababu ukisema huna uhakika maana yake ni wewe ndio huna uhakika ila wengine wana uhakika. Ukiwaomba hao wengine taarifa ili na wewe uhakikishe na wao pia hawana.

Sasa kama kila mtu hana uhakika, maana yake kitu kinachozungumziwa hakipo. Hitimisho ni kwamba hicho kitu hakipo.

Mungu hayupo.
 
Hayo Maswali Unajiuliza Kwasababu Unaiwaza Sana Dunia Jambo Ambalo Haliwezi Kukupa Majibu Ya Hayo Maswali Kwamwee

Kwanza Unapaswa Kujua MWENYEZI MUNGU Hakumuumba Mwanaadamu Kwasababu Ya Maisha Ya Dunia Bali Dunia Ni Njia Tu Ya Kufika Huko Penye Uzima Wa Milele Ndio Maana Unaona Mapungufu Mengi Katika Dunia Kwasababu Sio Sehemu Rasmi Ya Wewe Kuishi Hapa

Katika Qur'an M/MUNGU Anasema "Hayakuwa Maisha Ya Dunia Isipokuwa Ni Starehe Fupi Tu Yenye Kupita" Nafikiri Unafahamu Maisha Ni Mafupi Sana Hivyo Mfano Kama Unapita Sehemu Ya Mapumziko Katika Safari Yako Yenye Haraka Na Ya Muda Mfupi Huwezi Kufanya Vitu Vyote Unavyovipenda Kwasababu Sio Sehemu Sahihi Na Rasmi Kwa Hivyo Vitu Ukizingatia Na Muda.

Pengine M/MUNGU Akasema "Na Akhera Ni Bora Kwenu Kuliko Maisha Ya Kwanza" Hapa Tunaona Ametumia Neno Bora Kwamaana Ule Ubora Na Utimamu Mnaoutaka Upo Huko Akhera Na Sio Duniani Ndio Maana Hakuna Sehemu Dunia Imetajwa Kuwa Bora

NB: Umavyozidi Kujipa Mashaka Ya Uwepo Wa Mungu Basi Shetani Nae Ndio Anazidi Kukupa Maswali Ya Kuzidisha Mashaka Yako
Wewe shtuka mapema hakuna mbingu hizo ni hadithi za watoto.
 
Kwanini usiseme hakuna uhakika wa kujua kama Mungu yupo au hayupo kwa sababu hakuna njia ya kuhakiki hilo? Wapo wenye mtazamo huo kwamba hakuna njia ya kujua ya kuweza kuthibitisha uwepo wake ila wewe unakimbilia kusema hayupo.

Hizo sifa tofauti za Mungu hazitoi hitimisho la kuwa hakuna Mungu.
Kitu kisichoweza kuthibitishwa kuwa kipo basi hicho kitu hakipo. Kama wewe unaweza mthibitishia kuwa Mungu yupo pasipo kuacha shaka fanya hivyo. Huwezi sema Mungu yupo kwa kusoma na kukariri hadithi za watu waliokufa.
 
Sio jibu sahihi, kwa nini tukeshe tunabuabudu na kutoa sadaka? Kama vipi si asingeumba tu huu ulimwengu!! Watu wanatupiga hela sana kwa kutumia imani.
Sio jibu sahihi kwa maana ipi kwamba hana haki ya kuamuru watu wamuabudu?
 
Kitu kisichoweza kuthibitishwa kuwa kipo basi hicho kitu hakipo. Kama wewe unaweza mthibitishia kuwa Mungu yupo pasipo kuacha shaka fanya hivyo. Huwezi sema Mungu yupo kwa kusoma na kukariri hadithi za watu waliokufa.
Kwahiyo wewe ukiiba halafu watu wakishindwa kuthibitishwa kuiba kwako hiyo inafanya kuwa wewe haujaiba au inakuwa watu wameshindwa tu kuthibitisha?
 
Sina sababu ya kusema hakuna uhakika, kwa sababu ukisema huna uhakika maana yake ni wewe ndio huna uhakika ila wengine wana uhakika. Ukiwaomba hao wengine taarifa ili na wewe uhakikishe na wao pia hawana.

Sasa kama kila mtu hana uhakika, maana yake kitu kinachozungumziwa hakipo. Hitimisho ni kwamba hicho kitu hakipo.

Mungu hayupo.
Sio kwamba nakuzuia wewe kusema Mungu hayupo ila hoja zako zenye kufanya useme hakuna Mungu ni hoja dhaifu hazina nguvu za kuhitimisha hakuna Mungu, huwezi kuniambia et kwa sababu Mungu anaelezwa kwa sifa tofauti tofauti basi ndio uhitimishe huyo Mungu hayupo. Kama hata wewe inawezekana kuelezewa kwa sifa tofauti za kwako kweli na zisizo za kwako sasa iweje Mungu kuelezwa kwa sifa tofauti wewe ukimbilie tu kuhitimisha hakuna Mungu?
 
Sio kwamba nakuzuia wewe kusema Mungu hayupo ila hoja zako zenye kufanya useme hakuna Mungu ni hoja dhaifu hazina nguvu za kuhitimisha hakuna Mungu, huwezi kuniambia et kwa sababu Mungu anaelezwa kwa sifa tofauti tofauti basi ndio uhitimishe huyo Mungu hayupo. Kama hata wewe inawezekana kuelezewa kwa sifa tofauti za kwako kweli na zisizo za kwako sasa iweje Mungu kuelezwa kwa sifa tofauti wewe ukimbilie tu kuhitimisha hakuna Mungu?
Basi mkuu tumalize ubishani, nionyeshe huyo Mungu yuko wapi.
 
Princes of Hell:
1. Satan from the south,
2. Lucifer from the east,
3. Belial from the north, and
4. Leviathan from the west

Tazama symbol ya baphomet.
 
Kiarabu/kilatini/Hebrew ni lugha ambayo waabudu shetani wanaitumia. Soma hapa chini..

The magical language used in Satanic ritual is Enochian, a language thought to be older than Sanskrit, with a sound grammatical and syntactical bases. It resembles Arabic in some sounds and Hebrew and Latin in others. It first appeared in print in
1659 in a biography of John Dee, the famous Sixteenth Century seer and court astrologer. This work, by Meric Casaubon, describes the occultist Dee's activities with his associate, Edward Kelly, in the art of scrying or crystal gazing.

kwa maana hiyo wale waleta dini za ukristo, uyahudi, uislam ndio wanaojua tofauti kati ya hizo dini na ushetani.
 
Mkuu we acha kuzurura kwa maneno we thibitisha kuwa Mungu yupo.
Uwepo wa Mungu unakubalika kwa imani na si kwa uthibitisho sasa kama utaniambia hakuna Mungu kwa sababu hakuna uthibitisho basi itakuwa hujui unajadili nini.
 
Nimekuwa nikikutana na maswali mbalimbali kuhusu dini au Mungu mfano

Niliwahi kuulizwa matendo mema yaliumbwa na nani nikajibu Mungu aliumba mema. Nikaulizwa tena mabaya yaliumbwa na nani nikakosa jibu.

Jamaa akaniambia Mungu wako aliumba mema na mabaya na akakuumba binadamu dhaifu na ukifanya mabaya au kumchagua shetani unapelekwa motoni . Swali ni je ikiwa unajua binadamu ni dhaifu kwanini umuwekee ujuzi wa mabaya na akikosea aende motoni kwanini mabaya yasiondolewe binadamu abaki na ujuzi wa mema au kwanini akimchagua shetani umchome moto...

Kingine Kwa msisitizo, KAMA MUNGU ANAJUA YA MBELE (KUWA ADAMU ATAASI)au SHETANI ATAASI KULIKUWA NA HAJA GANI KUJISUMBUA KUUMBA DUNIA MPAKA AKACHOKA NA KUPUMZIKA. UNGEKUWA WEWE UNGEJENGA NYUMBA AMBAYO UNAJUA KESHO INAENDA KUBOMOKA? MAMBO MENGINE TUSIWEKE UGUMU KUELEWA.

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
Huyo Mungu hayupo.

Hizo habari za Mungu zimetungwa na watu kwa kuungaunga, ndiyo maana unaona maswali mengi na contradictions zisizotatulika.
 
Back
Top Bottom