Hizi ishu za Mungu/Dini ni very complicated

Hizi ishu za Mungu/Dini ni very complicated

Mungu hakumwumba mwanadamu kuwa dhaifu isipokuwa wanadamu tunaozaliwa leo tunazaliwa katika dunia ambayo imeshaathirika na matokeo ya uasi.

Mfano; Biblia inasema baada ya Mungu kuumba kila kitu akatazama na kuona kila kitu kuwa ni chema sana. Mwanzo 1:31.

Hata kuna wakati Mungu aliwahi kumwita Ayubu kuwa ni mtu mkamilifu. Kwa hiyo kusema kwamba wanadamu wote ni dhaifu au hakuna mkamilifu sio sawa labda kama unajilinganisha na Malaika ambao waliumbwa tofauti na wanadamu

Ayubu 1:8
Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu.


Mungu hakumwumba mwanadamu kuwa roboti bali alimwumba awe mtu mwenye maamuzi. Kwa sababu Mungu alitaka kuwe na mahusiano ya upendo kati yake na mwanadamu aliyemwumba ndo maana ilibidi kumpa uhuru kamili wa kuamua kumpenda Mungu au kutompenda.

Mungu asingeweza kujisikia kupendwa na mwanadamu ambaye hana utashi wake binafsi yani kama tungeumbwa as programmed creatures. Ukweli ya kwamba tuna uwezo wa kuamua kumtii au kutomtii Mungu ni udhihirisho tosha kuwa Mungu alituachia uhuru mkubwa ili Upendo utakaooneshwa kutoka kwetu Kwenda kwake uwe Upendo halisi.

Mungu hachoki. Isaya 40:28 “Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, Bwana, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki.”

Biblia inaposema Mungu alistarehe siku ya saba haina maana kuwa alichoka, ni lugha ya picha kuonesha kazi maalum ya Uumbaji aliikamilisha na aliacha kufanya uumbaji, lakini sio kwamba alikuwa amechoka na wala sio kwamba aliacha kufanya kazi kabisa.

Mwanzo 2:2
"Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya."

Mwanzo 2:3
"Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya."

Yohana 5:17
"Akawajibu, Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi."

Sina majibu ya kila swali ulilouliza lakini nadhani nitakuwa nimesaidia kupunguza mzigo wa maswali yako
Majibu mazuri sana mkuu
 
Nimekuwa nikikutana na maswali mbalimbali kuhusu dini au Mungu mfano

Niliwahi kuulizwa matendo mema yaliumbwa na nani nikajibu Mungu aliumba mema. Nikaulizwa tena mabaya yaliumbwa na nani nikakosa jibu.

Jamaa akaniambia Mungu wako aliumba mema na mabaya na akakuumba binadamu dhaifu na ukifanya mabaya au kumchagua shetani unapelekwa motoni . Swali ni je ikiwa unajua binadamu ni dhaifu kwanini umuwekee ujuzi wa mabaya na akikosea aende motoni kwanini mabaya yasiondolewe binadamu abaki na ujuzi wa mema au kwanini akimchagua shetani umchome moto...

Kingine Kwa msisitizo, KAMA MUNGU ANAJUA YA MBELE (KUWA ADAMU ATAASI)au SHETANI ATAASI KULIKUWA NA HAJA GANI KUJISUMBUA KUUMBA DUNIA MPAKA AKACHOKA NA KUPUMZIKA. UNGEKUWA WEWE UNGEJENGA NYUMBA AMBAYO UNAJUA KESHO INAENDA KUBOMOKA? MAMBO MENGINE TUSIWEKE UGUMU KUELEWA.

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
Screenshot_20240213-082650_Quora.jpg
 
Mungu hakumwumba mwanadamu kuwa dhaifu isipokuwa wanadamu tunaozaliwa leo tunazaliwa katika dunia ambayo imeshaathirika na matokeo ya uasi.

Mfano; Biblia inasema baada ya Mungu kuumba kila kitu akatazama na kuona kila kitu kuwa ni chema sana. Mwanzo 1:31.

Hata kuna wakati Mungu aliwahi kumwita Ayubu kuwa ni mtu mkamilifu. Kwa hiyo kusema kwamba wanadamu wote ni dhaifu au hakuna mkamilifu sio sawa labda kama unajilinganisha na Malaika ambao waliumbwa tofauti na wanadamu

Ayubu 1:8
Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu.


Mungu hakumwumba mwanadamu kuwa roboti bali alimwumba awe mtu mwenye maamuzi. Kwa sababu Mungu alitaka kuwe na mahusiano ya upendo kati yake na mwanadamu aliyemwumba ndo maana ilibidi kumpa uhuru kamili wa kuamua kumpenda Mungu au kutompenda.

Mungu asingeweza kujisikia kupendwa na mwanadamu ambaye hana utashi wake binafsi yani kama tungeumbwa as programmed creatures. Ukweli ya kwamba tuna uwezo wa kuamua kumtii au kutomtii Mungu ni udhihirisho tosha kuwa Mungu alituachia uhuru mkubwa ili Upendo utakaooneshwa kutoka kwetu Kwenda kwake uwe Upendo halisi.

Mungu hachoki. Isaya 40:28 “Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, Bwana, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki.”

Biblia inaposema Mungu alistarehe siku ya saba haina maana kuwa alichoka, ni lugha ya picha kuonesha kazi maalum ya Uumbaji aliikamilisha na aliacha kufanya uumbaji, lakini sio kwamba alikuwa amechoka na wala sio kwamba aliacha kufanya kazi kabisa.

Mwanzo 2:2
"Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya."

Mwanzo 2:3
"Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya."

Yohana 5:17
"Akawajibu, Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi."

Sina majibu ya kila swali ulilouliza lakini nadhani nitakuwa nimesaidia kupunguza mzigo wa maswali yako
Big up!!
 
Wafuasi wa dini ni watu wajinga na wapumbavu wasiopenda kutumia akili

Kipindi utakachoanza kutumia akili ndicho hichi kipindi utakachoshindwana na hao wachungaji na makondoo zao hao wafuasi wanaoaminishwa mambo ya Mungu hayachunguziki

Yaani waliona watu wakihoji mambo ya kiimani na wangegundua kuna uongo basi watu wangeachana na dini, hawa jamaa wakaamua kuweka vitisho ktk hizo dini zao na vitabu vyao vya uongo.

Ukitaka kujua hawa jamaa ni wajinga kiasi gani basi watakushambulia badala ya kukujibu kwa facts, na facts sikuzote huwezi kuzijibu kwa kutumia maandiko ya kidini ambayo hayana ushahidi wala proof of existence kwa characters wake.

Manabii sijui na mitume wa dini zote walitungwa tu kama stories za Tommy&Jelly special kwa kutawala akili za wajinga haswa Waafrika.

Mungu wa ukristo&uislam ni gaidi nambari moja
Duu ....
 
Naunga mkono hoja, ila sina imani saana na dini. Nachojua hata babu zangu waliabudu hata kabla ya kuletewa imani za kigeni.. maana walijua ipo nguvu kuliko was, almost jamii zote duniani ziliabudu kwa namna tofauti tofauti..
Sahihi kbsa
 
Labda pengine tunamtafuta mahali asipokuwepo, ama tumemuacha mbali sana! Maana kuna mafundisho ukiyasikiliza, mpaka umpate ni zaidi ya ngamia kupenya kwenye tundu la sindano... anyway sitaki kukufuru, moto sio mzuri.
[emoji16][emoji16]
 
Kuna pahala nimewahi sikia kuwa 'yupo mkuu wa anga, kazi yake ni kuzuia maombi kwenda juu.. kuvuka hapa si kazi ndogo, binafsi sielewi kwanini awe na nguvu hivi..
Ndiyo mkuu wa anga yupo kuzuia maombi ...na wanasema ana nguvu kweli kweli ....bado ukienda baharini sjui Kuna shetani gani Yani kila aina ya vinyamkera vipo
 
Mkuu sijui kama unaelewa, nimekwambia kitu kimoja hakiwezi kua na maelezo tofauti halafu bado kikawa kitu kile kile.

Mtu akikwambia Samia ni mrefu, mwingine akasema samia mfupi, mwingine akasema Samia ni bonge, mwingine akasema Samia ni mwembamba mrefu, mwingine akasema Samia ni andunje, hapo ni kwa muonekano wa nje.

Ikaja tena mtu mwingine akasema samia ana upendo, mwingine akasema Samia ana roho mbaya sana, mwingine akasema Samia ni vile, ni hivi.

Kwa Samia hayo maelezo yatakua mashaka kwamba eitha samia hayupo ama wote ni waongo.

Sasa kwa Mungu tunaongelea ishu tofauti, soma sifa za Mungu alizopewa kwenye biblia na quran, hizo sifa ndio zinahitimisha zenyewe kwamba hicho kitu kinachozungumziwa hakipo ama kama kipo basi kimepewa sifa za uongo ambazo hakina.

Mungu ni hadithi tu zisizo na kichwa wala miguu, hayupo.
Nimetoa mfano wa Rais Samia kuonyesha kwamba watu wanaweza kumuelezea kwa sifa tofauti na hata wewe umetolea mifano ya sifa tofauti ambazo watu wanaweza kumpa Samia, kwahiyo inawezekana hizo sifa zengine sio za kweli ila tunajua Rais Samia yupo.

Sasa ajabu tunapokuja kwenye suala la Mungu unakimbilia kuhitimisha hakuna Mungu sababu anaelezwa kwa sifa tofauti ambazo zengine si za kweli, hapo ndio tunaposhindwa kuelewana sioni hoja yako ya msingi kufanya ukimbilie kuhitimisha hakuna Mungu kabisa.
 
Nimetoa mfano wa Rais Samia kuonyesha kwamba watu wanaweza kumuelezea kwa sifa tofauti na hata wewe umetolea mifano ya sifa tofauti ambazo watu wanaweza kumpa Samia, kwahiyo inawezekana hizo sifa zengine sio za kweli ila tunajua Rais Samia yupo.

Sasa ajabu tunapokuja kwenye suala la Mungu unakimbilia kuhitimisha hakuna Mungu sababu anaelezwa kwa sifa tofauti ambazo zengine si za kweli, hapo ndio tunaposhindwa kuelewana sioni hoja yako ya msingi kufanya ukimbilie kuhitimisha hakuna Mungu kabisa.
Yes, tunajua Samia yupo na tunaweza kuthibitisha kwa kumuona na kuondoa sintofahamu iliyotolewa na watu tofauti tofauti kumhusu yeye, mfano mtu akisema Samia ni mrefu, wewe ukaenda kumuona na kukuta ni mfupi ni sawa, umethibitisha na umemuona na ukaondoa sintofahamu iliyotolewa hapo kabla.

Shida inakuja kwa Mungu, kila mtu ana sifa tofauti kumhusu yeye, kila mtu ana sifa na maelezo tofauti kuhusu Mungu. Hilo sio tatizo.

Tatizo linakuja pale ambapo, kila mtu ana sifa za Mungu ambazo ni tofauti na mwenzake na kila mtu anasisitiza hizo sifa ndio sahihi na kweli tupu halafu hakuna mahala pa kuthibitishwa hizo sifa. Hilo inakuletea jibu moja kwamba hicho kitu hakipo kwa sababu hizo sifa wao wamezitoa wapi kama hicho kitu hawajawahi kukiona?

Mbaya Zaidi sifa wanazotaja ni kwamba Mungu ni yule yule asiebadilika jana, leo na hata milele, sasa ni asiebadilika lakini ana sifa tofauti tofauti kwa kila mtu 'aliemuona', hicho kitu kipo ama ni hadithi tu?

Jibu ni moja, Mungu hayupo.
 
Yes, tunajua Samia yupo na tunaweza kuthibitisha kwa kumuona na kuondoa sintofahamu iliyotolewa na watu tofauti tofauti kumhusu yeye, mfano mtu akisema Samia ni mrefu, wewe ukaenda kumuona na kukuta ni mfupi ni sawa, umethibitisha na umemuona na ukaondoa sintofahamu iliyotolewa hapo kabla.

Shida inakuja kwa Mungu, kila mtu ana sifa tofauti kumhusu yeye, kila mtu ana sifa na maelezo tofauti kuhusu Mungu. Hilo sio tatizo.

Tatizo linakuja pale ambapo, kila mtu ana sifa za Mungu ambazo ni tofauti na mwenzake na kila mtu anasisitiza hizo sifa ndio sahihi na kweli tupu halafu hakuna mahala pa kuthibitishwa hizo sifa. Hilo inakuletea jibu moja kwamba hicho kitu hakipo kwa sababu hizo sifa wao wamezitoa wapi kama hicho kitu hawajawahi kukiona?

Mbaya Zaidi sifa wanazotaja ni kwamba Mungu ni yule yule asiebadilika jana, leo na hata milele, sasa ni asiebadilika lakini ana sifa tofauti tofauti kwa kila mtu 'aliemuona', hicho kitu kipo ama ni hadithi tu?

Jibu ni moja, Mungu hayupo.
Kwanini usiseme hakuna uhakika wa kujua kama Mungu yupo au hayupo kwa sababu hakuna njia ya kuhakiki hilo? Wapo wenye mtazamo huo kwamba hakuna njia ya kujua ya kuweza kuthibitisha uwepo wake ila wewe unakimbilia kusema hayupo.

Hizo sifa tofauti za Mungu hazitoi hitimisho la kuwa hakuna Mungu.
 
Duu mim naamini yupo manake jua ,mwezi nyota na sayari zingine haziwezi kutokea tu bila kuwepo nguvu ya ziada na hiyo nguvu ndo Mungu ...
Hata huyo Mungu hawezi kutokea tu from nothing.

Kama kila kitu kilichopo lazima kiwe kimetokana na nguvu fulani, Hata huyo Mungu lazima awe ametokana na nguvu fulani.

Na hiyo nguvu fulani iwe imetokana na nguvu fulani, Na mwendelezo huu uendelee kwa nguvu nyingi endless zisizo na mwisho.

Pasiwepo kitu chochote kile kilicho jitokeza chenyewe pasipo nguvu fulani.

Vinginevyo, Hakuna ulazima wa kwamba jua,nyota na sayari zingine zimetokana na nguvu fulani.
 
Kwani wewe mkuu huwezi kuamuru na kutumia utakavyo kitu chako?
Sio jibu sahihi, kwa nini tukeshe tunabuabudu na kutoa sadaka? Kama vipi si asingeumba tu huu ulimwengu!! Watu wanatupiga hela sana kwa kutumia imani.
 
Back
Top Bottom