Hizi ishu za Mungu/Dini ni very complicated

Hizi ishu za Mungu/Dini ni very complicated

Nadhani Haya mambo yanahitaji level flani ya mambo ya kiimani zaidi
MUNGU aliumba kwa ukamilifu, lakini Kuna mifumo/systems alitengeneza ili vyote vikafanyike kwa hiyo. Bila uhuru upendo ni batili, vyote vifanyikavyo sio kwa kupenda/kutokupenda bali kwa kufuata na kuheshimu mifumo aliyoiweka humo. Ni ngumu kuelezea jambo zito linalohitaji sio tu ufahamu wa kawaida bali zaidi ya hapo.
Long story short: Mungu ni Dhahiri na vyote vifanyikavyo ni thabiti kwa kufuwata sheria na mifumo iliyoandaliwa.
Kama Mungu huyo aliumba kila kitu kwa ukamilifu.

Halafu kuna systems zikaja kuzingua, Basi kazi yake ya uumbaji haina ukamilifu bali ina dosari na kasoro.

Na huyo Mungu sio mkamilifu na kazi zake zina weaknesses.
 
Mungu hakumwumba mwanadamu kuwa dhaifu isipokuwa wanadamu tunaozaliwa leo tunazaliwa katika dunia ambayo imeshaathirika na matokeo ya uasi.

Mfano; Biblia inasema baada ya Mungu kuumba kila kitu akatazama na kuona kila kitu kuwa ni chema sana. Mwanzo 1:31.

Hata kuna wakati Mungu aliwahi kumwita Ayubu kuwa ni mtu mkamilifu. Kwa hiyo kusema kwamba wanadamu wote ni dhaifu au hakuna mkamilifu sio sawa labda kama unajilinganisha na Malaika ambao waliumbwa tofauti na wanadamu

Ayubu 1:8
Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu.


Mungu hakumwumba mwanadamu kuwa roboti bali alimwumba awe mtu mwenye maamuzi. Kwa sababu Mungu alitaka kuwe na mahusiano ya upendo kati yake na mwanadamu aliyemwumba ndo maana ilibidi kumpa uhuru kamili wa kuamua kumpenda Mungu au kutompenda.

Mungu asingeweza kujisikia kupendwa na mwanadamu ambaye hana utashi wake binafsi yani kama tungeumbwa as programmed creatures. Ukweli ya kwamba tuna uwezo wa kuamua kumtii au kutomtii Mungu ni udhihirisho tosha kuwa Mungu alituachia uhuru mkubwa ili Upendo utakaooneshwa kutoka kwetu Kwenda kwake uwe Upendo halisi.

Mungu hachoki. Isaya 40:28 “Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, Bwana, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki.”

Biblia inaposema Mungu alistarehe siku ya saba haina maana kuwa alichoka, ni lugha ya picha kuonesha kazi maalum ya Uumbaji aliikamilisha na aliacha kufanya uumbaji, lakini sio kwamba alikuwa amechoka na wala sio kwamba aliacha kufanya kazi kabisa.

Mwanzo 2:2
"Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya."

Mwanzo 2:3
"Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya."

Yohana 5:17
"Akawajibu, Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi."

Sina majibu ya kila swali ulilouliza lakini nadhani nitakuwa nimesaidia kupunguza mzigo wa maswali yako
Dunia yenye uasi iliwezaje kuwepo kwa Mungu mwenye kujua yote tangu mwanzo na hata milele?

Huyo Mungu Hakujua kwamba uasi utakuja kuwepo audhibiti mapema?

Mungu huyo, Alishindwaje kuumba dunia isiyo na uasi?

Je Hakujua?

Au ni plan zake dunia iwe na uasi?

Yeye si mnadai ni Mungu mwenye kujua yote tangu mwanzo na hata milele?
 
Mungu hawezi kua sawa na Samia. Samia kila mtu atamuongelea jinsi anavyomjua, anavyofaidika na yeye na mambo kama hayo. Pia mtu anaemjua Samia utotoni atamuongelea tofauti na Samia na mtu mwigine aliemjua ukubwani, mume wake atamuongelea tofauti na watoto wake, ndugu zake wa damu watamuongelea tofauti na rafiki zake.

Tunapozungumzia Mungu tunaongelea kitu tofauti, hatutegemei kiwe na maelezo tofauti ya kubadilika badilika kulingana na wakati . Umesahau Biblia inasema Mungu ni yule yule jana , leo na hata milele? Mungu ni yule yule asie badilika? Soma biblia.

Sasa kama Mungu ni yule yule jana , leo na hata milele, hawezi kua na maelezo tofauti tofauti, atakua ni yule yule siku zote.

Kwa msingi huo Mungu anaetajwa kwenye dini hayupo.
Ulisema kitu kimoja hakiwezi kuwa na maelezo tofauti, nimetoa mfano wa Rais Samia kuonyesha kuwa kunaweza kuwa na maelezo tofauti ila anayekusudiwa ni mmoja ndio maana hata kama hayo maelezo yanaji contradict bado hatuwezi kuhitimisha kwa kusema Rais Samia hayupo.
 
Wafuasi wa dini ni watu wajinga na wapumbavu wasiopenda kutumia akili

Kipindi utakachoanza kutumia akili ndicho hichi kipindi utakachoshindwana na hao wachungaji na makondoo zao hao wafuasi wanaoaminishwa mambo ya Mungu hayachunguziki

Yaani waliona watu wakihoji mambo ya kiimani na wangegundua kuna uongo basi watu wangeachana na dini, hawa jamaa wakaamua kuweka vitisho ktk hizo dini zao na vitabu vyao vya uongo.

Ukitaka kujua hawa jamaa ni wajinga kiasi gani basi watakushambulia badala ya kukujibu kwa facts, na facts sikuzote huwezi kuzijibu kwa kutumia maandiko ya kidini ambayo hayana ushahidi wala proof of existence kwa characters wake.

Manabii sijui na mitume wa dini zote walitungwa tu kama stories za Tommy&Jelly special kwa kutawala akili za wajinga haswa Waafrika.

Mungu wa ukristo&uislam ni gaidi nambari moja
 
Mim nachoweza kusema hatujui njia ya kumfikia Mungu ili ajibu maombi yetu manake mambo yanavyoenda ni vice versa kbsa Yani Kuna wakati kama maombi hayajibiwi japo majaribu ni sehem ya maisha yetu

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
Kama anaona watu hawajui wanampata vipi kwanini ajifiche? Kwaninis asijidhirishe basi hata kwa njia yoyote ile ili watu wamuamini? Basi alete hao manabii wake kama wale tuliosimuliwa na vitabu?

Yaani Mungu wa hizi dini anabehave kama mwanamke vile anayependa kunyenyekewa na kutongozwa tongozwa ili afurahi kiufupi ana aibu na anapenda attention za kijinga, Mungu muweza wa yote watu wanamlilia kila siku makanisan na misikitin lkn hakuna hata moja alilowai kujibu, kazi yake ni kula bata tu huko mbinguni akizungukwa na hao manyani wake wanaomjaza misifa ya kijinga badala ya kumchana ukweli juu ya maisha mabovu ya viumbe wake hapa duniani, inawezekana pia huyu Mungu keshalizika na yanayoendelea au hawa malaika na washauri wake wanamdanganya na kumshauri ujinga ili kumgombanisha na watu, alafu baadae akija kustuka shetan atampipga gape kubwa sana huyo Mungu, huenda huko mawinguni sijui mbinguni kuna mawakala na maspy wa shetan ambao wanakaa meza moja na Mungu wakiiba siri na kumpotosha juu ya yanayoendelea hapa duniani, sasa huyo Muweza wa yote ni Mungu gani?.

Kiufupi Huyo Mungu wa hizi dini hayupo watu wasijichoshe kuomba na kuamini ktk upuuzi
 
Dini hazina magumu ila ni binaadamu ndio anajichanganya mwenyewe na kuvuruga.
Dini ni kumfanya binaadamu aishi na wenzake kwa wema na amani na kutii amri za Mungu ambazo wote tunakubaliana nazo.
 
Dini hazina magumu ila ni binaadamu ndio anajichanganya mwenyewe na kuvuruga.
Dini ni kumfanya binaadamu aishi na wenzake kwa wema na amani na kutii amri za Mungu ambazo wote tunakubaliana nazo.
Wacha upuuzi wewe itakuwa hujui hata historia za dini, kabla ya kuundwa hizi takataka ziitwazo dini watu waliishi kwa amani bila mitengano ya kijinga, vita vya kijinga kisa utofauti wa imani, alafu hizi dini ndizo zimeleta machafuko na tabia za kishenzi.

Chunguza hata ushoga unaenezwa na dini, huko makanisani na misikitini mnajuwa kuwa watoto zenu wanachofanyiwa na hao watu wenu wa kidini?

Mnajua kuwa kipindi cha kueneza dini ni maelfu ya wangapi walipoteza maisha?, hivi hizo akili za kutetea dini mnazipata wapi?
 
[emoji16][emoji16][emoji16]siwezi nikajifanya sielewi ,na hapa ndo chimbuko LA maswali hayo kwenye post , pia labda inawezekana mpaka Sasa kizazi cha Leo hatujajua Mungu anafikiwaje,japo binafsi naamini Mungu yupo ila usije sema nithibitishe ,siwezi kuthibitisha ila naamini Mungu yupo

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
Naunga mkono hoja, ila sina imani saana na dini. Nachojua hata babu zangu waliabudu hata kabla ya kuletewa imani za kigeni.. maana walijua ipo nguvu kuliko was, almost jamii zote duniani ziliabudu kwa namna tofauti tofauti..
 
Halafu jingine, amenyamaza kimya kama vile hayupo.
Wananzengo wanatumia huo mwanya kuwapiga hela wanaomtafuta.
Labda pengine tunamtafuta mahali asipokuwepo, ama tumemuacha mbali sana! Maana kuna mafundisho ukiyasikiliza, mpaka umpate ni zaidi ya ngamia kupenya kwenye tundu la sindano... anyway sitaki kukufuru, moto sio mzuri.
 
Mim nachoweza kusema hatujui njia ya kumfikia Mungu ili ajibu maombi yetu manake mambo yanavyoenda ni vice versa kbsa Yani Kuna wakati kama maombi hayajibiwi japo majaribu ni sehem ya maisha yetu

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
Kuna pahala nimewahi sikia kuwa 'yupo mkuu wa anga, kazi yake ni kuzuia maombi kwenda juu.. kuvuka hapa si kazi ndogo, binafsi sielewi kwanini awe na nguvu hivi..
 
Hayo Maswali Unajiuliza Kwasababu Unaiwaza Sana Dunia Jambo Ambalo Haliwezi Kukupa Majibu Ya Hayo Maswali Kwamwee

Kwanza Unapaswa Kujua MWENYEZI MUNGU Hakumuumba Mwanaadamu Kwasababu Ya Maisha Ya Dunia Bali Dunia Ni Njia Tu Ya Kufika Huko Penye Uzima Wa Milele Ndio Maana Unaona Mapungufu Mengi Katika Dunia Kwasababu Sio Sehemu Rasmi Ya Wewe Kuishi Hapa

Katika Qur'an M/MUNGU Anasema "Hayakuwa Maisha Ya Dunia Isipokuwa Ni Starehe Fupi Tu Yenye Kupita" Nafikiri Unafahamu Maisha Ni Mafupi Sana Hivyo Mfano Kama Unapita Sehemu Ya Mapumziko Katika Safari Yako Yenye Haraka Na Ya Muda Mfupi Huwezi Kufanya Vitu Vyote Unavyovipenda Kwasababu Sio Sehemu Sahihi Na Rasmi Kwa Hivyo Vitu Ukizingatia Na Muda.

Pengine M/MUNGU Akasema "Na Akhera Ni Bora Kwenu Kuliko Maisha Ya Kwanza" Hapa Tunaona Ametumia Neno Bora Kwamaana Ule Ubora Na Utimamu Mnaoutaka Upo Huko Akhera Na Sio Duniani Ndio Maana Hakuna Sehemu Dunia Imetajwa Kuwa Bora

NB: Umavyozidi Kujipa Mashaka Ya Uwepo Wa Mungu Basi Shetani Nae Ndio Anazidi Kukupa Maswali Ya Kuzidisha Mashaka Yako
 
Ulisema kitu kimoja hakiwezi kuwa na maelezo tofauti, nimetoa mfano wa Rais Samia kuonyesha kuwa kunaweza kuwa na maelezo tofauti ila anayekusudiwa ni mmoja ndio maana hata kama hayo maelezo yanaji contradict bado hatuwezi kuhitimisha kwa kusema Rais Samia hayupo.
Mkuu sijui kama unaelewa, nimekwambia kitu kimoja hakiwezi kua na maelezo tofauti halafu bado kikawa kitu kile kile.

Mtu akikwambia Samia ni mrefu, mwingine akasema samia mfupi, mwingine akasema Samia ni bonge, mwingine akasema Samia ni mwembamba mrefu, mwingine akasema Samia ni andunje, hapo ni kwa muonekano wa nje.

Ikaja tena mtu mwingine akasema samia ana upendo, mwingine akasema Samia ana roho mbaya sana, mwingine akasema Samia ni vile, ni hivi.

Kwa Samia hayo maelezo yatakua mashaka kwamba eitha samia hayupo ama wote ni waongo.

Sasa kwa Mungu tunaongelea ishu tofauti, soma sifa za Mungu alizopewa kwenye biblia na quran, hizo sifa ndio zinahitimisha zenyewe kwamba hicho kitu kinachozungumziwa hakipo ama kama kipo basi kimepewa sifa za uongo ambazo hakina.

Mungu ni hadithi tu zisizo na kichwa wala miguu, hayupo.
 
Na hata huyo binadamu mwenyewe akitengeneza kitu chochote iwe mashine au chochote kile hakiwezi kua 100% perfect yaani coefficient of machine haiwezi kua 100% hata itoke kiwandani muda huu na chochote kile kingine mpaka vyakula, lazima kitakua na kasoro fulani
Kwa hiyo uwezo wa mwanadamu ni sawa na Mungu?

If yes, ina maana Mungu sio perfect kama tunavyoambiwa.
 
Back
Top Bottom