Issue ya Mungu ni very complicated, but existence ya binadamu na uhai Kwenye Sayari ya Dunia pekee (Hadi sasa hatujui, mahari popote kwenye Uhai) ni more complicated.
According to Science (I'm scientist too)
Dunia ina Miaka zaidi ya 4.5 billions ilichukua Miaka billion 3.5 dunia na condition za mwanzo zilizosababisha Maisha from simple cellular life.
Katika kipindi hiki, Dunia iligongana na Sayari inaitwa Theia ambayo Ndio chanzo Cha Dunia kuwa na Mwezi tunouona, Licha ya hii impact kuwa mbaya Lakini ilisababisha msingi muhimu wa upekee wa Dunia, Hili lilifanya Dunia kuwa tilt kwa nyuzi 23, pia ikasababisha core(kokwa la Dunia) kuzunguka kwa kasi sana, hii Ndio sababu Dunia ina strong Magnetic field ambayo inazuia Solar winds kufika ardhini na pia inasababisha atmosphere ya Dunia isipotee na hivyo maji kukakua(Maji Ndio msingi wa aina zote za Maisha Dunia).
Si kuwa tulipata hayo Mabadiliko Lakini pia tulipata mwezi ambao unachangia sana tabia ya nchi na vitu kama tidal waves
Hili tukio lilitokea kipindi Maji wala Maisha Bado hayajatokea Duniani.
Kumbuka Mars haina atmosphere na Usumaku kama wa Dunia na Ndio sababu ya maji yake yako chini ya ardhi na mengine yalipotea, but si asilimia impact kama ya Dunia na Theia inagarantee mabadiliko kama yalitokea kwa Dunia.
Jupiter, uwepo wa Jupiter umbali uliopo uanilinda sana Dunia dhidi ya Vimondo na Magimba mengine ambayo yangeigonga Dunia na kusababisha madhara kwa Dunia na binadamu, hakuna mpangilio mwingine kama huu kwenye Planetary Systems zingine.
Venus, Kwenye Solar System yetu kuna Sayari 4 ambazo zimeundwa kwa miamba ambazo zinaweza kuhifadhi maji na kuruhusu Maisha, but Dunia ni ya kipekee na yenye Bahati, why?
Mercury iko karibu sana na Jua na ni tidally locked (Upande mmoja tu Ndio unaiona Jua na upande mwingine always ni Giza) ukiachia joto ni Eneo dogo sana lingepata maji na kuwa na uhai, Venus Ndio Sayari yenye joto sana kwenye Solar system na inazunguka anti-clockwise, Licha ya hali yake Venus ilikuwa inafanana na Dunia kwa zaidi ya asilimia 90 na pengine ilikuwa na Maji na miti au some cellular life lakini ikagongana na Other body ikaisababishia hali iliyopo sana, Mars haina atmosphere, wala Usumaku na kokwa lake limeganda, hivyo maji wala atmosphere haiwezi kukata, But kwa upekee na Bahati Dunia imepona na kuwa kama ilivo Leo.
Jambo lingine la kipekee ni Extinction of dangerous Dinosaurs, baada ya miaka na miaka Solar system ikawa Stable na maisha yakatokea Duniani na viumbe wa aina tofauti wakatokea, Moja ya hao viumbe ni Dinosaur hawa walikuwa wakubwa na wanakula viumbe vidogo vidogo, kwa maana nyingine Maisha ya Binadamu na utashi wake usinge kuwepo kama Dinosaur wangeishi wakati mmoja na Binadamu, Lakini kwa upekee na maajabu Dunia ikaangukiwa na Kimondo ambacho kilisababisha Dinosaur kufa wakabaki ndege tu ambao Ndio chakula chetu.
Haya matukio ni ya kipekee na ya Bahati sana, huwa najiuliza kwanini Yalitokea kwa Dunia tu, hili swali hunifanya nijisemee inawezekana Mungu yuko, ila anavosemwa na Dini sio sahihi