Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon imejibu jinai zinazoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza kwa kushambulia ngome za jeshi la utawala huo ghasibu.
Kwa mujibu wa televisheni ya Al-Jazeera, vikosi vya Hizbullah ya Lebanon vimeshambulia kwa kombora linaloongozwa kwa mitambo ngome ya kijeshi ya Al-Abad ya utawala wa Kizayuni iliyoko karibu na kitongoji cha Hula.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, vikosi vya Hizbullah vimerusha kombora la kutungua kifaru pia kuelekea ngome ya kijeshi ya Khurbatul-Manara.
Wakati huohuo, mizinga ya utawala wa Kizayuni imelenga maeneo ya Aljabin na Yarin yaliyoko kusini magharibi mwa Lebanon.
Katika siku zilizopita pia, jeshi la Kizayuni lilishambulia kwa mizinga maeneo ya mpakani mwa Lebanon.
Shambulio la kombora la Hizbullah
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, hadi sasa makumi ya maelfu ya Wazayuni wamehama katika vitongoji vya walowezi vilivyoko kwenye mpaka wa pamoja na Lebanon kwa kuhofia mashambulizi ya Muqawama.
Siku ya Jumamosi, tarehe 7 Oktoba 2023, wanamapambano wa Muqawama wa Palestina walianzisha operesheni ya kushtukiza iliyopewa jina la Kimbunga cha Al-Aqsa kutokea Gaza (kusini mwa Palestina) dhidi ya ngome za utawala wa Kizayuni unaoikalia Quds kwa mabavu.
Katika hatua ya kulipiza kisasi na kufidia kipigo kikali na pigo kubwa ulilopata, utawala wa Kizayuni umechukua hatua ya kufunga vivuko vyote vya Gaza na hivi sasa unaendeleza mashambulio ya mtawalia dhidi ya maeneo ya makazi ya watu na vituo vya tiba vya Ukanda huo.
Uungaji mkono wa tawala za Magharibi kwa Israel kwa kisingizio cha kujilinda kumekuwa sawa na kutoa kibali kwa utawala huo wa Kizayuni cha kuendeleza mauaji ya kikatili na kinyama ya watoto na wanawake wa Kipalestina.
Kwa mujibu wa televisheni ya Al-Jazeera, vikosi vya Hizbullah ya Lebanon vimeshambulia kwa kombora linaloongozwa kwa mitambo ngome ya kijeshi ya Al-Abad ya utawala wa Kizayuni iliyoko karibu na kitongoji cha Hula.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, vikosi vya Hizbullah vimerusha kombora la kutungua kifaru pia kuelekea ngome ya kijeshi ya Khurbatul-Manara.
Wakati huohuo, mizinga ya utawala wa Kizayuni imelenga maeneo ya Aljabin na Yarin yaliyoko kusini magharibi mwa Lebanon.
Katika siku zilizopita pia, jeshi la Kizayuni lilishambulia kwa mizinga maeneo ya mpakani mwa Lebanon.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, hadi sasa makumi ya maelfu ya Wazayuni wamehama katika vitongoji vya walowezi vilivyoko kwenye mpaka wa pamoja na Lebanon kwa kuhofia mashambulizi ya Muqawama.
Siku ya Jumamosi, tarehe 7 Oktoba 2023, wanamapambano wa Muqawama wa Palestina walianzisha operesheni ya kushtukiza iliyopewa jina la Kimbunga cha Al-Aqsa kutokea Gaza (kusini mwa Palestina) dhidi ya ngome za utawala wa Kizayuni unaoikalia Quds kwa mabavu.
Katika hatua ya kulipiza kisasi na kufidia kipigo kikali na pigo kubwa ulilopata, utawala wa Kizayuni umechukua hatua ya kufunga vivuko vyote vya Gaza na hivi sasa unaendeleza mashambulio ya mtawalia dhidi ya maeneo ya makazi ya watu na vituo vya tiba vya Ukanda huo.
Uungaji mkono wa tawala za Magharibi kwa Israel kwa kisingizio cha kujilinda kumekuwa sawa na kutoa kibali kwa utawala huo wa Kizayuni cha kuendeleza mauaji ya kikatili na kinyama ya watoto na wanawake wa Kipalestina.