Tatizo sio lugha sababu Mel. John Okumu akiwasomea swali na nyie mnaliona kwenye screen, unaweza ukawa umeshaelewa swali kabla hajamaliza kusoma tatizo ni content katika Elimu yetu... Kwa mfano kulikuwa na swali umawekewa picha utaje ni ua gani I have no idea, ila teammate wangu aliyesoma Kenya aliyapata sababu alisema hayo walikuwa wanafundishwa shuleni... Na ukiangalia maswali mengi ni general knowledge ila Elimu yetu haina hizo issue ingekuwa sio udadisi wetu na kuwa tunapenda kujisomea vingi tusingejua.. Kwa upande wangu knowledge ya vitu vingi vile ilitokana na Mimi kuwa napenda kujisomea sana kuna kipindi nilikuwa nmesoma vitabu vyote vilivyoko maktaba ya chini Arusha Library
Sent using Jamii Forums mobile app
Mdau, naomba kuweka kumbukumbu sawa ,
Sijajua umeshiriki mwaka gani , lakini mimi nilishiriki , inaugural event ya mwaka 2007 , ambapo vyuo viwili vya Tanzania Mzumbe, ikiongozwa na Prof Kamuzora, ambaye alikuja kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Sayansi na sasa ni RAS Kagera kama sikosei na UDSM ikiongozwa na Dr Laurean Ndumbaro, ambaye sasa ni Katibu Mkuu Utumishi, vyote UDSM na Mzumbe viliingia robo fainali , mwaka huo event hii ilikuwa Inaitwa Celtel Africa Challenge, baada ya Celtel kubadili jina ndo ikaitwa Zain Africa Challenge.
Ni kweli klikuwa moja kati ya vipindi bora sana kwenye TV, kwa jinsi nilivyosikia ni Kuwa Airtel , hawakutaka kuendelea kutoa pesa ya kudhamini kipindi hiki na gharama zingine za production kwenda kwa Richard Reid Productions ya Marekani ambao ndio walikuwa wanahusika na kurekodi kipindi, kama walivyofanya wenzao Zain na Celtel. Nami nimekuwa najiuliza sijui kwa nini kampuni Kubwa kama Coca Cola au Matajiri wanaopenda kuendeleza Social Enterprises na Education Initiatives kama kina Tony Elumelu hawajajitoekeza kudhamini kipindi hiki.
Kama waziri wa elimu anasema Tanzania imetokana na kuungana kwa Zanzibar na Zimbabwe unatarajia wanafunzi wawe wa aina gani?Shindano hilo lilipoteza mvuto baada ya Tanzania kila mara kushika mkia hivyo washindani wakawa ni walewale Kenya na Uganda.
Kumbe nyie ndio mlienda kutuletea aibu!Mlikuwa mnapewa category, halafu mnaenda kujiandaa kilingana na hizo. Ila muda wa kujiandaa ni mfupi kama saa hivi.
Dah umenikumbusha mbali sana.. Nilikuwa kwenye celtel Africa challenge ya kwanza kabisa Nairobi... Duuh we really had fun....Hakika kilikuwa ni kipindi kinachovutia wengi; watoto, vijana na hata wazee. Umaridadi wa bwana John Sibi-Okumu katika kuuliza maswali ulikifanya kipindi na mvuto maradufu.
Wale jamaa walikuwa sharp sana, maana kuna muda kabla hata muulizaji hajamaliza kuuliza swali, tayari alikuwa anapewa jibu.
Je, nini kilifanya hiki kipindi kupotea licha ya mvuto wake?
Nini kilikuwa kinakuvutia kwenye hiki kipindi ?
Was epic I can tell you... Those good daysMojawapo ya kipindi bora japo wabongo hatukutamba sana ila uwakilishi niliuona, nilichopenda ni kuona jinsi wanafunzi wanavyochuana
aim for the stars
Uongo nabisha.. Nilikuwa mmoja wa washiriki wa kwanza kabisa kipind ndio imekuwa launched... Wala sio kweli ni liveHawakuwa sharp kivile coz kipindi kilikuwa kinaeditiwa....nenda youtube angalia behind the scene utaona walivyokuwa wanachukua muda kujibu baadhi ya maswali hata yule muuliza maswali kuna muda alikuwa anakosea hadi kuuliza.
Sent using Jamii Forums mobile app
Woow.. Kumbe nawe ulishiriki.. Mimi nilishiriki the first year they started it....Sio kweli maswali in live sema wnaunganisha unapomaliza first segment mnapumzika kuendelea na segment nyingine ... Mimeshiriki na tulikuwa chuo cha kwanza from Tanzania kufika quarter final
Sent using Jamii Forums mobile app
Kabla ya zain kulikuwa kinaitwa celtel Africa challengeLakini kipindi kingeweza kuendelezwa licha ya Zain kubadilika. Kingeweza kupewa hata jina jingine ila content ikabaki.
Sasa hivi ni gavana wa MachakosCobra squad series ya Kenya hii, ilitungwa na Alfred Mutua msemaji wa serikali ya Kenya enzi za mwai kibaki ,sasa HV sijui ana cheo gani
Sisi tulikuwa tunalala safari Park HotelTulilazwa by then millenium towers..room $250, ilikuwa experience nzuri sana.
Uongo sio kweli.. Mimi nilikuwa sua na nilishiriki pia... Mwaka huo huo 2007.... Weka taarifa yako ya vyuo vizuri....Mdau, naomba kuweka kumbukumbu sawa ,
Sijajua umeshiriki mwaka gani , lakini mimi nilishiriki , inaugural event ya mwaka 2007 , ambapo vyuo viwili vya Tanzania Mzumbe, ikiongozwa na Prof Kamuzora, ambaye alikuja kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Sayansi na sasa ni RAS Kagera kama sikosei na UDSM ikiongozwa na Dr Laurean Ndumbaro, ambaye sasa ni Katibu Mkuu Utumishi, vyote UDSM na Mzumbe viliingia robo fainali , mwaka huo event hii ilikuwa Inaitwa Celtel Africa Challenge, baada ya Celtel kubadili jina ndo ikaitwa Zain Africa Challenge.
Ni kweli klikuwa moja kati ya vipindi bora sana kwenye TV, kwa jinsi nilivyosikia ni Kuwa Airtel , hawakutaka kuendelea kutoa pesa ya kudhamini kipindi hiki na gharama zingine za production kwenda kwa Richard Reid Productions ya Marekani ambao ndio walikuwa wanahusika na kurekodi kipindi, kama walivyofanya wenzao Zain na Celtel. Nami nimekuwa najiuliza sijui kwa nini kampuni Kubwa kama Coca Cola au Matajiri wanaopenda kuendeleza Social Enterprises na Education Initiatives kama kina Tony Elumelu hawajajitoekeza kudhamini kipindi hiki.
Oohooo safi.. Sisi intake ya 2007 tulikwea Kenya Airways tukafikia safari Park Hotel. It was quite an experience experience during that timeMimi nilishiriki two times ya kwanza ilikuwa celtel challenge nikiwa first year tukaishia Dar.. Ya pili ilikuwa zain challenge tukatoboa mpaka Uganda...
It was amazing experience tulifikia millennium tower baada ya kupanda ndege na Kampala Serena Uganda
Sent using Jamii Forums mobile app
Maswali mlikuwa mnapewa muda gani kabla ya kwenda kwenye shindano ?Maswali yalikuwepo mnapewa CD yalikuwa mengi category tofauti tofauti tulichokuwa tunafanya tunaangalia categories then tunajisomea kupata general knowledge...
Pia mbali na Zain kuwa wadhamini maswali na program yote ilikuwa chini ya kampuni ya Kimarekani iliyokuwa inaandaa maswali na programs
Sent using Jamii Forums mobile app
HahahahaMbona kuna watu mnadai mlishiriki halafu taarifa mnazotoa wenzenu pia ambao nao wanadai walishiriki zinakinzana?
Hapo ndio utata, lkn labda kwakua vyuo tofauti tofauti ,walikua wakienda tofauti piaShindano moja, Ila kila mtu anakuja na maelezo ya utofauti.
Ndo anataka kuujua huo mwisho ilikuwaje...Kila chenye mwanzo kina mwisho