Mdau, naomba kuweka kumbukumbu sawa ,
Sijajua umeshiriki mwaka gani , lakini mimi nilishiriki , inaugural event ya mwaka 2007 , ambapo vyuo viwili vya Tanzania Mzumbe, ikiongozwa na Prof Kamuzora, ambaye alikuja kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Sayansi na sasa ni RAS Kagera kama sikosei na UDSM ikiongozwa na Dr Laurean Ndumbaro, ambaye sasa ni Katibu Mkuu Utumishi, vyote UDSM na Mzumbe viliingia robo fainali , mwaka huo event hii ilikuwa Inaitwa Celtel Africa Challenge, baada ya Celtel kubadili jina ndo ikaitwa Zain Africa Challenge.
Ni kweli klikuwa moja kati ya vipindi bora sana kwenye TV, kwa jinsi nilivyosikia ni Kuwa Airtel , hawakutaka kuendelea kutoa pesa ya kudhamini kipindi hiki na gharama zingine za production kwenda kwa Richard Reid Productions ya Marekani ambao ndio walikuwa wanahusika na kurekodi kipindi, kama walivyofanya wenzao Zain na Celtel. Nami nimekuwa najiuliza sijui kwa nini kampuni Kubwa kama Coca Cola au Matajiri wanaopenda kuendeleza Social Enterprises na Education Initiatives kama kina Tony Elumelu hawajajitoekeza kudhamini kipindi hiki.