Hivi, uislamu uliwahi kuleta nini?

Hivi, uislamu uliwahi kuleta nini?

uislamu upo karibia miaka 1000 pwani yetu na sehemu nyinginezo, hivi kipi haswa kimeletwa na uislamu kwa maana ya civilization na maendeleo ya jamii? hata tu mazao labda kuna zao gani ambalo lililetwa na uiaslamu hapa kwetu ?
Vitu vingi sana kuanzia hesabu hadi medical science ,vifaa vingi unavyoviona leo mahospitalini alivumbua mtu anaitwa zahrawi ambaye vitabu vyake hadi leo bado wazungu wanatumia kufundishia ulaya
Algebra etc vyote hivyo walileta muslim scholars
 
Mimi nimesema hivo sio kwa kudhani, ni kweli kabisa. We nenda kwenye websites za matokeo uone shule za zenji zinavyozalisha vilaza. Kila mwaka zinakuwaga za mwisho. Hiyo inatokana na kutokuzingatia mambo ya shule wao kila kukicha ni madrasa tu kufundishana upuuzi.
Hayo ni matokeo ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na Nyerere,unazani ingekuwepo ile Zanzibar ya Sultani wa Zanzibar Tanganyika ingeona ndani leo hii,kweli wajinga wengi sana, Zanzibar ilikuwa zaidi ya Dubai watu walikuwa wanatoka sehemu mbalimbali ya Afrika kwenda kusoma Zanziba,historia inaweza kuhalibiwa na watu kwa makusudi na wajinga wakaja kutukana
 
Ni nzuri ili tuweza kuwaelimisha wengine,kuna inchi zilikuwa na Ustarabu mpaka wakoloni wenyewe walishanga,kuna Nyumba wanajua Mzungu na ukristo ndivyo vilivyoleta ustarabu, umeshawahi kusikia historia ya Misri? Mungu mwenyewe anamwambia nabii Ibrahimu,usikae bure tembeatembea ukaone wenzako walivyostarabika,anafika Misri na kukutana na bonge la mji likiwa na kila kitu,mpaka wakamya'nganya mke wake Sala?
So what is your point here!!!

Kabla ya hizi dini iwe yoyote ile unadhani mwenye kitovu cha ukoo wenu (babu wa mababu zako) yeye hakuwa mstaarabu kulingana na mazingira ya wakati wake?kwamba kama siyo kuja mwarabu au mzungu basi leo tungeishia kuwa viumbe visivyostaarabika duniani!au una maana gani?
 
Uisilamu ulileta Biashara na Trade katika pwani yetu ya Afrika ya Mashariki na ndio sababu ya kuzaliwa kwa lugha ya Kiswahili.
Asante , shikamoo, madrasa, mwalimu,marahaba ,gari,gunia,dunia hayo ni baadhi ya maneno yaliyoletwa na hao wageni kutoka mashariki ya mbali na kati
Na kifanya lugha ya kiswahili kuzid kukua
 
Uleta viungo kama iliki ,mdalasini, binzari nyembamba,karafuu pilipili manga nk
Vyakula kama pilau
Pia shanga ,vyombo vya udongo
Mavazi kama hijabu na kanzu
 
Umeleta Alkasusu mujarab...
download (1).jpeg
 
Asante , shikamoo, madrasa, mwalimu,marahaba ,gari,gunia,dunia hayo ni baadhi ya maneno yaliyoletwa na hao wageni kutoka mashariki
Uko sahihi kabisa, lakini nadhani SHIKAMOO ni Kibantu GARI ni Kihindi DUNIA ni Kihindi MADRASA ni Kiarabu
 
uislamu upo karibia miaka 1000 pwani yetu na sehemu nyinginezo, hivi kipi haswa kimeletwa na uislamu kwa maana ya civilization na maendeleo ya jamii? hata tu mazao labda kuna zao gani ambalo lililetwa na uiaslamu hapa kwetu ?
Unajua hata hiyo covid vaccine ya pfizer wagunduzi ni waislamu kutoka turkey?
Na unajua hata hiyo alcohol unayoiona kwenyenye kila pombe wagunduzi ni waislamu?
 
Waliweza kujenga misikiti na majengo katika miji ya bagamoyo, kilwa ,tanga na zanzibar ila kwa sasa yamebaki kama maghofu
 
uislamu upo karibia miaka 1000 pwani yetu na sehemu nyinginezo, hivi kipi haswa kimeletwa na uislamu kwa maana ya civilization na maendeleo ya jamii? hata tu mazao labda kuna zao gani ambalo lililetwa na uiaslamu hapa kwetu ?
Mambo mengi
1. Ugaidi
2. Uuaji wa kukata watu vichwa
3. Ahadi ya bikra 72
4. Unafiq
 
Swali lako ni zuri sana
Uislamu imeleta mambo Mengi afrika
1. DIni watu walikua wanabudu Mizimu ilipofika wakati uislamu unaingia afrika tukambiwa Kuna Mungu wa kweli ambaye Yeye ndo kila kitu anaitwa Allah ✅

2. Watu walikua hawana Stara( Uislamu ukaleta mwanaume anajistiri vipi na mwanamke anajistiri vipi )

3. Biashara uislamu ukaleta biashara afrika kilimo cha karafu nk

4. Upendo tukafundishwa binadamu kupendana tusichukiane, tuheshimiane mkubwa kwa mdogo au mdogo kwa mkubwa.

5. Mahali pa kufanyia nyumba za ibada misikiti ikajengwa kilwa, Zanzibar, mtwara nk

Kwa ufupi TU ndo hivyo Kuna vingi vimeletwa
 
Ulileta ustaarabu na maendeleo kwani haujasoma historia ya miji ya kilwa, sofara, bagamoyo nk nenda kaone maendeleo mabaki ya magofu kule
 
Uislam umeleta ustaarabu na biashara Pwani na ndio sababu Makafiri wamehamia Dar kwa wingi.
Leo makafiri wanakimbia makwao kwenda kwa waswahili kutafuta maisha
Wacha weeeeeeeeh.... Ustaarabu wa vigodoro, ushoga, umaskini,ujinga, kubeba mabusha, uvivu, unywaji kahawa siku nzima.... Angalia maeneo yaliyojawa na waislamu hata Dar.ni maeneo ya watu waswahili maskini. Temeke, Buguruni kwa mnyamani, tandale,mbagala,vingunguti,mburahati. Asilimia 80 plus kumejaa waislamu.
 
Uislamu ulileta maandiko ya Kiarabu, ambayo yalichangia kuanzishwa kwa mfumo wa elimu ya Kiislamu kupitia madrasa.

Maarifa ya hesabu (hisabati), unajimu, tiba, na jiografia yaliletwa kupitia maandiko ya Kiarabu na yalifundishwa katika miji mikubwa kama Kilwa, Mombasa, na Zanzibar.

Kiswahili, ambacho ni lugha mchanganyiko ya Kibantu na Kiarabu, kilikuza mawasiliano na biashara.

Maandishi ya Kiarabu yalichangia kuendeleza Kiswahili kama lugha ya kibiashara na kidini.

Uislamu ulileta utaratibu wa biashara wenye misingi ya haki na uaminifu kupitia sheria za Kiislamu (Sharia).

Biashara ya kimataifa ilistawi kupitia biashara ya dhahabu, pembe za ndovu, viungo (spices), na bidhaa nyingine kupitia pwani ya Afrika Mashariki.

Uislamu ulileta mtindo wa ujenzi wa misikiti, majumba, na miji, kama vile Kilwa na Lamu, kwa kutumia mitindo ya Kiislamu na Kiarabu kama mihrab, minara, na mapambo ya jiwe na mbao.

Ingawa baadhi ya mazao yalikuwepo kabla ya Uislamu, wafanyabiashara Waarabu walileta mazao mapya kama vile:

Mikahawa (kahawa)
Mpunga (aina fulani za mchele)
Miwa (sukari)
Ndimu na machungwa
Maharage na viungo kama karafuu (cloves) ambazo zilipandwa sana Zanzibar na Pemba.

Uislamu ulileta desturi za ndoa, mavazi (kama vile hijab na kanzu), na sheria za kijamii zilizoendana na mafundisho ya dini.

Sherehe kama Iddi na Sunna zilianzishwa na kuendelezwa katika jamii za pwani.

Kwa ujumla, uislamu ulileta ustaarabu kwa kuunganisha elimu, biashara, kilimo, na utawala, na hivyo kuchangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
 
Back
Top Bottom