Bufa
JF-Expert Member
- Mar 31, 2012
- 10,665
- 21,099
Issue sio Uislm but ni Uaarabu na resources zilizo katika hizo Nchi Indonesia & Malaysia hazina resources zozote za maana kama zilivyo Nchi za kiarabu.
Turkey kinacho msaidia ni geographical position yake dhidi ya adui wa USA & West countries ambaye ni Russia.Turkey inatumika kimkakati kuua nguvu za Russia kimkakati.
Muwe mnashirikisha ubongo na kufanya research kabla hamjachangia pumba. Unaijua Indonesia wewe? Unasema Indonesia haina resources zozote za maana, really? Nchi gani ya kiarabu, in the middle East rather inaigusa Indonesia kwa rasilimali?
Kwanza unajua GDP ya Indonesia ni over 1 trillion USD, hamna nchi ya arabuni inagusa hapo.
Unajua Indonesia inazalisha mafuta ya kutosha na ilikua OPEC na kusitisha ushirikiwa wake voluntarily twice? Unajua Indonesia inazalisha gold, copper, mbao nk. Unajua Indonesia ina mbuga za wanyama, misitu ya mvua, ardhi yenye rotuba nk? Indonesia ina visiwa zaidi ya 15,000 (Elfu kumi na tano) na 5,000 (Elfu tano tu) ndo inhabited. Nchi gani ya arabuni inagusa hata kimoja wapo hapo.
Ukitoa mafuta arabuni kuna nini kingine in terms of natural resources? Name just two.
FYI Indonesia na Congo ndo nchi zinazochuana when it comes to rasilimali.
Mmemkaa bongo mnajazwa ujinga na CCM nyie ndo matajiri pekee wa rasilimali kila mtu anawaonea wivu na nyie mnaamini.