Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,587
- 23,947
Wajerumani wa leo bado wanashangaa ilikuwakuwaje hadi babu na bibi zao kumtukuza na kumshangilia Hitler wakimuona kama mkombozi. Wengine wao wamebaki wakijiuliza kinachoweza kuwapata watu wenye akili timamu hadi kumhusudu binadamu mwenzao na kumuona kama mungu-mtu na kauli yake kuwa sheria.
Ingawa Historia inafundisha mengi na kutuonya juu ya hali kama hizo, wengi tumeshindwa kujifunza na kwa Watanzania wenzangu sishangai hata kidogo. Kwa miaka sitini tumeruhusu mambo yale yale, watu wale wale, mfumo ule ule...hakika hali hii inatisha, inaudhi na inakasirisha na mwisho wake hauwezi kuwa mzuri.
Leo hii polisi anayetakiwa kulinda usalama wa raia na mali yake, anaamka asubuhi, anavaa magwanda yake, anaingia mtaani na si kutimiza wajibu wake kikatiba ...la hasha, kumsaka au kumvizia raia, kumnyanyasa kwa kumbambikizia kosa na hatimaye kumpora kidogo alicho nacho ili asifiwe kwa kuiingizia serikali mapato, huku tukipiga makofi.
Kwamba Katiba inaweza kuwekwa kando kwa kisingizio cha kunyosha nchi na sisi tukapiga vigelegele ni dalili mbaya sana. Tunaumwa na bila kutambua kwamba tunahitaji matibabu ya haraka tunaelekea kubaya. Kwamba mwenzetu anaweza kukamatwa kwa kutoa maoni na sisi tukashangilia ni kwamba tumekufa kiakili ingawa tunatembea.
Ingawa Historia inafundisha mengi na kutuonya juu ya hali kama hizo, wengi tumeshindwa kujifunza na kwa Watanzania wenzangu sishangai hata kidogo. Kwa miaka sitini tumeruhusu mambo yale yale, watu wale wale, mfumo ule ule...hakika hali hii inatisha, inaudhi na inakasirisha na mwisho wake hauwezi kuwa mzuri.
Leo hii polisi anayetakiwa kulinda usalama wa raia na mali yake, anaamka asubuhi, anavaa magwanda yake, anaingia mtaani na si kutimiza wajibu wake kikatiba ...la hasha, kumsaka au kumvizia raia, kumnyanyasa kwa kumbambikizia kosa na hatimaye kumpora kidogo alicho nacho ili asifiwe kwa kuiingizia serikali mapato, huku tukipiga makofi.
Kwamba Katiba inaweza kuwekwa kando kwa kisingizio cha kunyosha nchi na sisi tukapiga vigelegele ni dalili mbaya sana. Tunaumwa na bila kutambua kwamba tunahitaji matibabu ya haraka tunaelekea kubaya. Kwamba mwenzetu anaweza kukamatwa kwa kutoa maoni na sisi tukashangilia ni kwamba tumekufa kiakili ingawa tunatembea.