Mwanamayu
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 11,701
- 6,936
Juzi nilipita mtaa mmoja pale Sinza karibu na kituo cha daladala cha Mugabe, na kuona geti jeusi la nyumba moja lenye tangazo: "Private House, Nyumba Binafsi". Haraka nilipelekea kuwa wakazi wa nyumba hiyo usumbuliwa na wageni (dar to dar) ambao udhani nyumba hiyo ni gesti, tena labda gesti bubu. Je yawezekana nyumba asilimia kubwa Sinza ni gesti bubu? Na ndio uwanja mkubwa wa ngono hapa Dar? Je, wakazi wa Sinza mnaliongeleaje hili?