Hivi RC Agrey Mwanri ni mchekeshaji?

Hivi RC Agrey Mwanri ni mchekeshaji?

Katika wakuu wa mkoa wanaopiga kazi ni pamoja na huyo mshua, sema tu anamaneno fulani na namna anavyoongea watu wanaona comedy au anatafuta media attention ila kiukweli ndivyo alivyo hivyo sisi watu wa mboka tunamjua kitambo
 
Watu wengi wamemjua Aggrey Mwanri kipindi hiki
Ila nimtu mzuri sana ninauwakika angekuwa waziri wa kilimo au biashara JPM asingepata tabuu
 
Anataka Mkuru amuone kuwa anachapakazi kumbe ni usaaniiiiiiiiiiiiiiii mtupu,kuna watu wanachapa kazi hata hizo mbwe mbwe hawana
 
Mshua anapiga kazi, na ana malengo.
mie wala sion i tatizo lake.
 
Jamaa hayuko normal yule kabisa. Lakini hiyo ni mbinu wanayotumia ma DC na ma RC kutafuta kiki. Wanakwenda nahali wakiwa na watu waliowaanda kuwapiga picha za video halafu wanaanza kufoka foka, kutishia waliochini yao, kutoa maagizo, wengine wanasukuma kuta zilizoandaliwa kwa show, kupima kwa tape nk halafu wanazirusha kwenye mitandao. Lakini ma DC na ma RC wanaopiga kazi zao bila kiki kama akina Mtaka huwezi kuwasikia au kuwaona wakifanya ujinga huo. Tumeshawang'amua
 
Mbona umeuliza na kutoa jibu hapo hapo? Katika hii awamu hao ndio wanaotakiwa...waliofyatuka! Hivyo ndivyo alivyowahi kutamka "BWANA YULE" kwamba ni kichaa na sifa kubwa anayoitaka anapoteua ni hiyo, wawe vichaa kama yeye. Sasa ikitokea kwamba alifanya makosa alipokuteuwa kwani hukuwa kichaa lazima sasa uoneshe kuwa na wewe umo.

Ukilegealegea na kuanza kutumia busara badala ya ukichaa, lazima utumbuliwe. Watu kama Nape walishindwa kutambua hili mapema hivyo walijaribu kutenda majukumu yao wakitanguliza hekima na kilichowapata hawatakisahau. Alionesha ukichaa ulivyo hadharinj kwa kutolewa bastola na toka siku hiyo anajua hatari ya kichaa kupewa rungu.

RC Agrey Mwanri huenda akawa kipenzi cha bosi wake labda hata zaidi ya waliomtangulia kwani ni katika wale wanaojua namna ya kuji-adapt katika mazingira chini ya huu utawala. Asiachie hapo, aongeze juhudi hadi hata familia yake ione tofauti na kwamba baba kabadilika. Hongera Mwanri! Milango karibu itafunguka kwani katika awamu hii ukichaa unalipa.


Mkuu labda ungetaka nani wawe wakuu wa mikoa yote? Wabongo hawaheshimu busara.
 
Wabongo shida sana, mtu asipofanya kazi yake ni shida sana, akifanya ndio tabu mara 2, tumezidi uvuvi wa mwili na kiakili kwa kweli..


Tunapenda vilaza wazembe, wahuni,
lakini wawe wanacheka sana, hata kama hawana uwezo, umakini wa kuendesha nchi, kutumia kodi zetu ipasanyo, kusimamia serikali zetu, pesa zetu, rasimali zetu, kuwawezesha watu wetu, kusimama na kuwa na msimamo, kushikamana hatuna uwo uwezo.

Tukipata watu wazuri tunakarisika, tunawafukuza, tunahitaji mbwembwe, maigizo, wahuni.

Ila ipo siku tutapata akili za ukweli.
 
Huyu RC Agrey Mwanri sasa amegeuka kuwa comedian wa Tabora.

Kila siku vyombo vya habari vimekuwa vikitoa clips mbalimbali ambazo anafanya vituko na ukimuangalia ni kama kwa sasa haziko level.

Mara fyekelea mbali, Sukumia ndani, jifanye unajikuna, akienda huko site ni makelele tu daah!

Any way ndiye aina ya watu anaowataka "BWANA YULE"
Na watu wendawazimu kama WEWE fyekelea mbali, sukuma ndani.
 
sio mchekeshaji ila ni kichekesho, kwa umri wake, maneno ya kihuni awaachie wenyewe


Uhuni unapimwaje atamtukana nani, kumuonea mtu gani bila sababu.

Kwake ni muhimu kuona kazi inafanyika ya ukweli,pesa zetu zote zinatumia vizuri., kodi yako hailiwi na wahuni wenye maneno mazuri. Au huo ndio uonevu.
 
Huyu RC Agrey Mwanri sasa amegeuka kuwa comedian wa Tabora.

Kila siku vyombo vya habari vimekuwa vikitoa clips mbalimbali ambazo anafanya vituko na ukimuangalia ni kama kwa sasa haziko level.

Mara fyekelea mbali, Sukumia ndani, jifanye unajikuna, akienda huko site ni makelele tu daah!

Any way ndiye aina ya watu anaowataka "BWANA YULE"
Amuulize mwijage
 
Huyu jamaa inabidi amtafute blogger awe ana updates vituko vyake maana daah...nyoosha uone, emb jifanye unajikuna, jifanye unajikuna halafu uone!

Kawaida sana kutumia lugha watu wako, wananchi wako wanayoielewa. Wewe hivi ungetumia lugha gani?
 
Back
Top Bottom