Chagu wa Malunde
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 8,708
- 5,711
Rais Magufuli ni Rais asiyependa kuona watu wanafanyiwa dhuluma na kunyanyaswa.
Mfano mzuri ni alipokuwa kahama alimuonea huruma toka moyoni kabisa mama ambae mume wake aligongwa gari na polisi traffic.
Ila kiuhalisia huku ngazi za chini wananchi bado wanadhulumiwa na kunyanyaswa sana. Hasa maeneo ya vijijini.
Watendaji wa kata wamejipa madaraka makubwa mno, wanawakamata watu wanawafungia katika lock up zao kinyume na Sheria.
Maana Mtendaji wa Kata haruhusiwi kisheria kusikiliza kesi za jinai, ila kama mlinzi wa amani anatakiwa akamate watuhumiwa kisha awapeleke polisi.
Lakini mambo ni tofauti. Wanakamata watu wanawapiga na kutengeneza mazingira ya kupewa rushwa.
Katika kila wilaya kuna Mkuu wa Wilaya na kamati yake ya ulinzi na usalama ya wilaya Je hawayaoni haya na kumpa taarifa Rais?
Maana kila kukicha ni matukio yanayofanana tu hasa maeneo ya vijijini.
Mfano mzuri ni alipokuwa kahama alimuonea huruma toka moyoni kabisa mama ambae mume wake aligongwa gari na polisi traffic.
Ila kiuhalisia huku ngazi za chini wananchi bado wanadhulumiwa na kunyanyaswa sana. Hasa maeneo ya vijijini.
Watendaji wa kata wamejipa madaraka makubwa mno, wanawakamata watu wanawafungia katika lock up zao kinyume na Sheria.
Maana Mtendaji wa Kata haruhusiwi kisheria kusikiliza kesi za jinai, ila kama mlinzi wa amani anatakiwa akamate watuhumiwa kisha awapeleke polisi.
Lakini mambo ni tofauti. Wanakamata watu wanawapiga na kutengeneza mazingira ya kupewa rushwa.
Katika kila wilaya kuna Mkuu wa Wilaya na kamati yake ya ulinzi na usalama ya wilaya Je hawayaoni haya na kumpa taarifa Rais?
Maana kila kukicha ni matukio yanayofanana tu hasa maeneo ya vijijini.