Hivi mtu akifa huwa anaenda wapi?

Ili uitwe MTU unahitaji vitu viwili mwili na roho! Muunganiko wa hivi viwili ndio hukamilisha ile dhana ya MTU, nje ya hapo kuna 'mwili wake' 'roho yake'
Kwahiyo tendo la kufa ni hali ya mwili kuachana na roho moja kwa moja
Mwili ni jumba tu la kubeba roho kwahiyo vinapotengana mwili huoza na kwisha kabisa na roho huendelea kuwayawaya duniani,ahera au peponi kulingana na imani za watu
 
afrika dini tumeletewa je waliokufa kabla ya dini kuja afrika na ambao walikua wanaabudu kwenye miamba walipokufa walienda wapi?
 
afrika dini tumeletewa je waliokufa kabla ya dini kuja afrika na ambao walikua wanaabudu kwenye miamba walipokufa walienda wapi?

Dini tulikuwa nazo lakini hazikuwa za kumuabudu Mungu mkuu tulikuwa na dini za kuabudu miungu kama mungu wa jua mungu wa mvua mungu was magonjwa mungu was utajiri bahati na kupendwa nk nk

Tulikuwa na ibada za mizimu kwakuwa tuliamini waliokufa hawakuwa mbali nasi na likipotokea tatizo kwenye jamii tulienda kwenye makaburi ya wafu kuomba wepesi
 
Mwagitho, naona majibu-mzaha yamekuwa mengi. Mie natoa jibu 'serious' ambalo pia ni 'practical', ila nitatumia kiswaenglish. A man has three parts. 1. Body/Mwili, 2. Soul/Nafsi (a soul is a seat of mind+affection+emotion) na 3. human Spirit.

Mwili ni nini?
- Unaufahamu-sihitaji kueleza; ila imeandikwa 'Bwana akafanya mtu toka katika udongo'. Mwili umetoka udongoni. Mtu akifa, Mwili unapelekwa kaburini, 'wewe ni mavumbi na mavumbini utarudi' Mwili ni mchanganyiko wa calcium - mifupani, water-ktk damu na nyama, madini ya chumvi za aina mbalimbali ambavyo vyote vinapatikana udongoni vilipotoka!

Human Spirit ni nini? Ni 'pumzi ya uhai' toka kwa Mungu. 'Bwana akampulizia 'pumzi ya uhai' huyo mtu aliyefanywa kwa udongo, na huyo mtu akawa NAFSI HAI'. Nafsi ni matokeo ya human spirit kuungana na human body.

- Pia 'a spirit' is a person. Huyu 'spirit' akipokea nguvu za ki-Mungu/ki-Yesu na Mungu akitaka, anaweza kumpa uwezo mara mojamoja (occassionally) wa kuona baadhi ya mambo ktk ulimwengu wa roho - the invisible spiritual world, lakini ni kwa lengo maalumu mfano- vita ya kiroho, kuchochea maombi maalumu, etc. Kwenye invisible spiritual world kuna spirits wengine ambao ni non-human; spirits hao ni 1. angels, 2 God (katika utatu wake) na 3 Satan and his demons (shetani na mapepo/majini yake).

Huyu human spirit akipokea nguvu za ki-shetani au ki-pepo-wabaya anakuwa na uwezo wa kuamua mwenyewe kufanya mambo kadhaa mfano: - kuruka usiku akiacha mwili wake kitandani, kinachoruka ni spirit na soul. Pia anakuwa na uwezo wa kusoma nyota, viganja, kutabiri - kwa maana ya fore-telling. Pia wengi wa wanao-advance sana katika Yoga, Kung-fu, Karate, Ninju-tsu, Witchcraft, Mazingaombwe, transcendental meditation, n.k. huwa wamepokea nguvu hizi za ki-pepo. The climax of all these demonic powers ndio akina ILLUMINATI, hasa wale INNER CIRCLE.

Soul/Nafsi ni nini?
Kulingana na bible, soul/nafsi ni matokeo ya kuunganika kwa human spirit na mwili wa udongoni. Bwana alipompulizia 'pumzi ya uhai' yule mtu wa udongo, ikatokea NAFSI. Nafsi nayo 'is a person' ila hawezi kufanya jambo independent of a spirit. Na anasukumwa na spirit mojawapo kati ya 'human spirit or God's spirit' au 'demonic/satanic spirit' Nafsi ndio wewe haswaaa! Nafsi ndio kiti cha 'mind, emotions na affection'. 1 toa 2 unapata ngapi? kinachojibu swali hilo ni soul-mind. Kama wee ni mwanaume unapenda mwanamke mnene au mwembamba? Anayejibu swali hilo ni soul-affection; swali jingine, mtu akikurushia maji machafu ya mvua kwa kuyakanyaga kwa gari lake kwa makusudi saa mbili asubuhi ukiwa njiani kuelekea ofisini/kibaruani, how angry do you become? hiyo hasira inatoka kwa soul-emotion. Ila kama nilivyosema hapo juu, chochote kitokacho kwa SOUL huwa kimeanzia kwa human spirit or demonic spirit or God's spirit.

Sasa baada ya 'definition' ndefu. Mtu akifa huenda wapi?

Mwili huzikwa kaburini ulikotoka

Nafsi ambayo ni wewe haswaaa hupotea mara baada ya human spirit kutengana na mwili. Nafsi ilitokea baada ya mwili kuungana na spirit/roho. Pia nafsi hupotea pale mwili unapotengana na human spirit. Pia Nafsi na mwili vitafufuliwa siku ya ufufuo/kiyama.

Human spirit never dies. Kwa mwanadamu aliyeshika njia ya Mungu wa Yesu Kristu hadi mwisho wa uhai wake, human spirit inarudi kwa Mungu na inaendelea kuishi huko. Sijui kama inakuwa idle ikingojea ufufuo wa mwili au kuna activity wanafanya. Hiyo experience sina.

Kwa mwanadamu aliyeenda kinyume na njia ya Yesu hadi mwisho wa maisha yake ya hapa, pia sina experience kuhusu human spirit yake huenda wapi - ila kwa mujibu wa maandiko inaenda mahali pa huzuni kubwa ikisubiri hukumu ya mwisho.

Kwa heri

Bonge la elimu mkuu
 
Katika kutafakari hoja hii nzito, sina budi kukubaliana na Maelezo yakinifu ya #Rapture Man kwamba mwanadamu yu katika hali tatu, yaani mwili, nafsi na roho!
Kwa kweli kwa kuwa mwili umetokana na mavumbi, basi hurudi mavumbini. Hiyo haina mjadala, ni ukweli usio na shaka. Huko mavumbini huirudia hali yake ya awali. Hakuna maarifa, wala kumbukumbu ya lolote.
Roho ambayo ndo pumzi ya uhai, umrudia yeye aliyeitoa na hapo hakuna cha dini wala dhehebu, ni kwa kila mtu. Kuna sehemu mbili za kuhifadhiwa roho, sehemu ya utulivu (amani) na sehemu ya wasiwasi (maangaiko)!
Ni muhimu kuelewa kuwa Mungu ni mtakatifu na hana urafiki na uovu uwao wote na pia wanadamu kwa asili yao ni waovu, yaani kwa kuzaliwa, kwa sababu huzaliwa ktk polluted world. Hivyo Mungu mwenyewe kwa wale aliowaridhia kuishi nao milele baada ya maisha haya, huwajaalia kile kinachoitwa neema kwa kuwaandaa kwa ajili ya maisha hayo yasiyo na mwisho/ya milele. Hao ndio roho zao huhifadhiwa sehemu tulivu ya amani wakisubiri wenzao ambao bado wangali duniani na wale waovu (ambao hawakujaaliwa neema hiyo) huhifadhiwa sehemu ile nyingine wakisubiri wenzao walioko duniani.
Baada ya mfumo huu wa mambo kuisha, waovu watapelekwa kule atakapokuwa shetani na malaika zake(mapepo, majini nk) kwa maisha ya milele na wema wataishi milele na Mungu kuwa ukumbusho wa kudumu kwamba kuliwahi kuwepo maisha kabla ya hayo!
Kuhusu nafsi hiyo haijadiliki kwa sababu haikuumbwa bali ilitokea kwa sababu ya contact btn spirit and body. Hivyo disconnection ya spirit and body inaua presence of soul. Na kazi ya soul ni kwa ajili ya mwili si kwa ajili ya roho. Nafsi hupotea the same way mshumaa unapozimika. Goes no where. Cease to exist, either in the spiritual realm or this tangible world!
Ndiyo maana hakuna kumbukumbu yoyote kwa mtu aliyekufa kuhusu mambo ya duniani. Iwe kwa mwili huu wa nyama ulioko kaburini au ule wa roho ulioko kule kwingineko!
Sijui kama mtoa mada una wasiwasi mpaka hapo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom