msabillah
JF-Expert Member
- Dec 5, 2011
- 4,764
- 3,189
Safi sana.Pandachigiza ni moja ya kata iliyopo shinyanga vijijini ambayo hata ukigoogle unaweza usiipate !
Hivi tukitumia frontal lobes za brain zetu ...mtu anayeishi los angels au edinburgh au philadelphia au munich anaweza kujua updates za changamoto zinazowakabili wasiojulikana wanaoishi kata ya Pandachigiza na vijiji vyake?
Hebu watanzania tuachage mizaha na tutumie wakati wetu vizuri ili tujikwamue na effects za kuwa nyuma ya wakati.
Tuachane na midomo ya kimbea ya watoto wa kishua ambao hawajawahi kung'atwa na mbu au kuathirika na maji yanayowasha ya mashamba ya mpunga.
Tujitahidi kuwa busy kujikwamua katika umasikini na tutumie elimu zetu kwa wale tuliobahatika kutoboa ili tuwasaidie walalahoi wanaoishi ibinzamata au lokisale.
Muheshimiwa Rais unalindwa na katiba katika kuwanyoosha vilivyo wanaotaka kutuondoa kwenye mada ya msingi ya kuhakikisha masikini wa kutupwa wanafanikiwa kimaisha baada ya miaka mingi ya kuteseka.
Mheshimiwa Rais una haki ya kikatiba ya kumfanyia lolote kwa yoyote bila kujali kelele za mafisadi wachache ambao wanataka kukwamisha zeal ya kuuletea umma masikini wa watanzania maendeleo.
TUACHE VICHEKESHO NA TUWE SERIOUS ...NA PIA TUTAMBUE NYAKATI ZIMEBADILIKA...TUPO KWENYE ERA YA BUSINESS UNUSUAL!
Tutake au tusitake ni lazima tunyookee njia moja tu... yaani njia nzuri na iliyokubaliwa na watanzania ....kwa gharama yoyote ile!!