Je, Tanzania ni masikini hivi kuendelea kupokea mikopo na misaada yenye masharti kinyume cha uhuru wetu?, au tukatae kama Nyerere?.

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,513
113,638
Wanabodi,
Jumatatu ya leo, nimepata fursa ya kuendelea na zile makala zangu, za Kwa Maslahi ya Taifa, makala ya leo nikihoji kuu umasikini wa Tanzania yetu na kupokea mikopo na misaada yenye masharti.

Naomba nianze kwa nukuu ya Mwalimu Nyerere kuwa "Umasikini mkubwa kabisa na mbaya kabisa, ni umasikini wa fikra" "poverty mentality"
Mwalimu akimaanisha kuwa umasikini mkubwa zaidi na mbaya zaidi, ni ukiwa na mawazo ya kimasikini.

Hivyo hoja kuwa Tanzania ni nchi masikini ni hoja muflisi kwa watu waliofilisika kimawazo, hivyo kitendo cha kuita nchi yetu kuwa nchi masikini, kunapalekea sisi kujisikia wanyonge.

Ukweli halisi kuhusu Tanzania, sio nchi masikini and has never been a poor county kwa sababu Tanzania ni nchi tajiri kwa utajiri mkubwa wa rasilimali za asili, madini, maliasli, mifugo, samaki, udongo wenye rutuba, vyanzo vya maji, vivutio vya utalii etc.

Kama Tanzania tuna utajiri wote huu, kwa nini nchi yetu bado ni masikini?. Naomba mimi nisilijibu swali hili, japo nakijua chanzo cha umasikini huu wa taifa letu, nisije nikachafua hali ya hewa ya bandiko hili.

Ndio maana, Rais wetu Dr. John Pombe Joseph Magufuli alipoingia tuu madarakani aliposema Tanzania sio masikini, Tanzania ni nchi tajiri na soon tutakuwa a Donner country wengi wetu tulimuunga mkono na kumpongeza.

Ila pamoja na utajiri wote huu tulionao ambao ndio unaotufanya Tanzania tuwe ni nchi tajiri, lakini Watanzania ni watu masikini wa kutupwa, wanaoishi kwenye umasikini uliotopea, wa kipato cha chini ya Dola kwa siku, na bajeti yetu a taifa, bado ni bajeti tegemezi inayowategemea wafadhili, misaada na mikopo, ya Mashirika yao ya misaada na mikopo, likiwemo Shirika la IMF na World Bank, kwa hiyo mwisho wa siku hutuamulia mambo yetu kupitia masharti ya mikopo na misaada yao.

CNN walipotangaza uongo huu,
CNN: Tanzania loses $300m World Bank loan amid crackdown concerns - JamiiForums

mimi ni miongoni mwa watu tulipinga na kushauri
Hata Nyerere alikataa, Rais Magufuli usikubali, shikilia msimamo. Tz tusikubali misaada na mikopo yenye masharti kuingilia sovereignty yetu - JamiiForums
Sasa nimesikia juu huu kuwa huu mkopo wa WB, ambao mwanzo ulizuiliwa kwa hoja za kauli ya Rais Magufuli kuhusu kutosomesha watoto wa kike wanaopata ujauzito wakiwa shuleni, hatimaye sasa mkopo huu utatolewa kwa masharti ya kulazimisha mtoto wa kike atakaeshika ujauzito akiwa shule lazima aendelezwe baada ya kujifungua.

Kama shurti hili ni kweli ni miongoni mwa masharti ya ukopo huu, jee tuupokee tuu kumaanisha tumekubali masherti?.

Kama rais wetu aliishatoa msimamo kuwa "hatusomeshi kwa fedha za serikali, wasichana wanaopata mimba shuleni".

Na kwa vile nchi yetu ni masikini, tunakwenda kuomba mkopo wa WB kuboresha elimu, mtoa mkopo anatuwekea shurti la kusomesha mtoto wa kike anayepata ujauzito, jee tupokee tuu kwa vile ni masikini na hizo fedha tunashida nazo, au tuwagomee kwa kunyesha kuwa Tanzania japo kweli ni masikini, lakini, kwenye kutuingilia mambo yetu ya ndani, sisi ni masikini jeuri, jee tuupokee tuu na kujidhalilisha uhuru wetu mbele ya matajiri hawa, au tuwagomee na kulinda heshima yetu, pamoja na umasikini wetu wote, lakini tulinde uhuru wetu, na hata ikibidi nchi yetu, kujifanya kuwa kama "Kozi Mwana Mandanda, Kulala Njaa Kupenda".

Wakati wa Nyerere, baada ya Vita ya Kagera, mwaka 1879, Mwalimu Nyerere alitutangazia taifa "miezi 18 ya kukaza mikanda" hii ni miezi 18 ya shida na hali ngumu.

Tukaomba mikopo WB na IMF, wakatupa masherti magumu, Mwalimu alikataa kata kata, hivyo ile miezi 18 ya shida , badala ya kuwa miezi 18, ili extend kwa miaka 6, hadi 1985, Mwalimu Nyerere alipoamua kuliko kugeuka nyuma akageuka jiwe la chumvi, akaamua kuachia usukani, akaachia ngazi, akaghatuka na kumpisha rais Mwinyi, aliyekuja kuruhusu kila kitu, hivyo kuitwa Mzee wa Rukhsa".

Enzi hizo, kiukweli hali ilikuwa mbaya, hivyo kuilazimu kukubali kila kitu yakiwemo masherti hayo magumu.

Lakini kwa Tanzania ya leo, nchi ya uchumi wa gesi, tunaelekea Tanzania ya viwanda, tunaweza kujenga miradi mikubwa ya SGR, Stigler Gorge kwa fedha zetu wenyewe za ndani, tunaweza kununua ndege Dreamliner kwa cash money, jee tuna umasikini gani hadi tupokee mkopo wenye masharti yanayokwenda kinyume cha kauli ya kiongozi wetu?.

Hakafu kamkopo kwenyewe tunako nyanyasiwa na kudhalilishwa ni ka tu dola Milioni 300 tuu!. Hii ni pesa gani ya kuinyenyekea wakati juzi kati tuu, yule mzungu wa Canada, katuahidi kutupa bure bila masherti yoyote!.
Kama hili ni kweli, pamoja na ukali wote ule rais Magufuli aliounyesha kwenye suala hili la mimba za mashuleni, halafu ni rais Magufuli yule yule aliyekuwa anafurahia msaada huu na masharti haya, hii inaonyesha, kumbe Tanzania pamoja na kuwa ni nchi huru, na tuna misimamo yetu, lakini mwamuzi wa mwisho kumbe sio sisi bali ni wenye kisu kikali kama ilivyo kwa mpiga zumari, kumbe nyimbo nyingine, hatuchagui sisi bali huchagua aliyemlipa mpiga zumari. Hivyo wanasiasa wa upinzani mliozuiliwa mikutano ya siasa, wakubwa wakiamua, mtashangaa mikutano inaruhusiwa.

Hivi kweli Tanzania ni masikini ki hivi hadi tupokee mikopo ya masherti hivi, na masherti mengine ni ya udhalilishaji wa uhuru wetu na viongozi wetu?.

Namalizia kwa hili swali,
Jee Tanzania ni Masikini Hivi Hadi Tuendelee Kupokea Mikopo na Misaada Yenye Masharti Kwa Ajili Tuu ya Umasikini Wetu, Au Tufike Mahali Tuwe Masikini Jeuri, Tukatae?

Wasalaam
Nawatakia Jumatatu Njema.
Paskali
 
kwenye uchumi fikra za mwalimu zilifeli, kitu cha msingi ni kujaribu kufanya kinyume cha sera zake za uchumi na ndicho awamu 3 zilizopita wamekifanya (kwa mafanikio kiasi). Tanzania ni miongoni mwa nchi masikini sana (ukiwa ndani ya nchi unaweza usilione hilo) hivyo kuwaletea jeuri wahisani kutawaumiza wananchi masikini zaidi. Joni na familia yake watakula na kulala kwa amani pale paradiso ya magogoni wakati masikini wakifa kwa stress za kufuatilia mafao yao!
 
Uhuru wetu ndio upi? Haki sawa kwa wote pasi na ubaguzi wa aina yoyote kwa kuzingatia misingi ya Katiba na sheria za nchi kwa mambo yote ndio nguzo namba moja ya uhuru. Uhuru ni kuwa na vyombo vya kiserikali vilivyo huru kutenda kwa mujibu wa Katiba na sheria pasi na kuingiliwa na yeyote kwa manufaa ya kikundi au chama fulani.
 
Hapana Paskali, Tanzania sio maskini kabisa kiasi hicho..sisi ni " dona kantri". Tuna donate madini yetu, gesi yetu, korosho ghafi huko nchi za nje.
Kwanza hilo swali lako ni la kichochezi...ungekuwa mtu baki hungepata mda wa kuuliza maswali hayo. We are in the right "track" to hell....
 
Katika watu ambao bots(jingalao & co) wanapata tabu kumtetea ni huyu ndg "dona kantri" mana kwanza ni Muongo na kigeugeu na ni mwepesi sana akitishwa kakaziwa na wazungu kdg kabadlisha mismamo yote. Pole SNA bwana dr mdiplomasia mkuu wa Puerto rico najua adha unayopata lkn uzalendo wako ndio unaoufanya uvumilie hapo
 
Mayalla ujue umaskini mbaya sana kaka yangu, ni kweli rais wetu ana nia niema sana ya kuliondoa taifa hili katika umasikini. Ila sasa tuna simama taratibu, tayari tanzania ni donor country toka enzi za nyerere. Ila tu wazungu wanaturudisha nyuma. Huu mkopo rais alitakiwa aukatae maana alisema mwenyewe yeye hatasomesha mtoto mwenye mimba, ila pia sheria yetu inasema ukimpa mimba mwanafunzi unapigwa miaka 30 wewe mpigaji mimba na mpigwaji mimba( naomba kusahihishwa kama nimekosea) sasa hii misaada itawezaje kumsomesha mwanafunzi. Mi nafikiri wazungu wameingizwa choo cha kike na rais sababu wahusika wote watakuwa gerezani. Ama la sivyo tukubali kuifuta sheria hii na tutegemee mafuriko ya waschana kubendishwa
 
Zimbabwe walikua maskini jeuri chini ya Mugabe.

Venezuela pia.

Na Kenya.

Nafikiri tutenganishe juu ya nchi kua maskini wa uchumi na kutokua maskini wa rasilimali.

Ni kweli tuna utajiri wa rasilimali kama ulivyoainisha lakini ili tuziconvert kua fedha ni mchakato kidogo ambao una vigingi vyake mfano sera mbovu, mikataba waliyoingia watawala waliopita na competence ya watawala.

Sisi ni maskini kiasi cha kuhitaji misaada? Ndiyo.

Tunaweza kusurvive bila kushirikiana na watoa misaada? Hapana.

Tunahitaji nini sasa?

Tuanze na mapinduzi ya kilimo. Tukifanikiwa kuna vitu vitakuja naturally.

Pia sitaki kuipita hii chance. Pascal Mayala nimescreenshot hapo ulipokosea chingereza iwe reference ya kijiweni kwangu, sitakuquote ili ukiamua ubadilishe.
 
kwenye uchumi fikra za mwalimu zilifeli, kitu cha msingi ni kujaribu kufanya kinyume cha sera zake za uchumi na ndicho awamu 3 zilizopita wamekifanya (kwa mafanikio kiasi). Tanzania ni miongoni mwa nchi masikini sana (ukiwa ndani ya nchi unaweza usilione hilo) hivyo kuwaletea jeuri wahisani kutawaumiza wananchi masikini zaidi. Joni na familia yake watakula na kulala kwa amani pale paradiso ya magogoni wakati masikini wakifa kwa stress za kufuatilia mafao yao!
Hoja nzuri mkuu, nilianzisha uzi jana wa kulaani vyombo vya habari vya nje kuangalia mabaya ya serikali ya Tanzania tu haswa hawa cnn, na bdye huo msaada waliposema kuwa wanautoa hivyo vyombo havikurusha hiyo habari nzuri kwa Tanzania kuwa benki ya dunia imeridhia kuuachia msaada iliyojuwa imegoma kuutoa, nilishangaa sana mods wakaufuta huo uzi kana kwamba wanafurahia hizi habar za nchi yetu kuandikwa kwa mabaya tu, mazuri no.
 
Hoja nzuri mkuu, nilianzisha uzi jana wa kulaani vyombo vya habari vya nje kuangalia mabaya ya serikali ya Tanzania tu haswa hawa cnn, na bdye huo msaada waliposema kuwa wanautoa hivyo vyombo havikurusha hiyo habari nzuri kwa Tanzania kuwa benki ya dunia imeridhia kuuachia msaada iliyojuwa imegoma kuutoa, nilishangaa sana mods wakaufuta huo uzi kana kwamba wanafurahia hizi habar za nchi yetu kuandikwa kwa mabaya tu, mazuri no.
Leo shift ya mepama sana umeingia hongera
 
"Ukweli halisi kuhusu Tanzania, sio nchi masikini and has never been a poor county kwa sababu Tanzania ni nchi tajiri kwa utajiri mkubwa wa rasilimali za asili, madini, maliasli, mifugo, samaki, udongo wenye rutuba, vyanzo vya maji, vivutio vya utalii etc"

Hivyo vyote vinahitaji mitaji mikubwa kutoka nchi za wazungu....sisi nimasikini living in "absolute poverty" hizo ni propaganda za CCM, tunazo lishwa katika shule zetu za msingi,
 
CNN trump aliwatukana matusi ya nguini na kuwafukza kwenye press conference aloifanya, so siwashangai sana kuona wanaripoti upumbavu kiasi kile
 
Hapana Paskali, Tanzania sio maskini kabisa kiasi hicho..sisi ni " dona kantri". Tuna donate madini yetu, gesi yetu, korosho ghafi huko nchi za nje.
Kwanza hilo swali lako ni la kichochezi...ungekuwa mtu baki hungepata mda wa kuuliza maswali hayo. We are in the right "track" to hell....


nimeishia kucheka😅😂
 
Wanabodi,
Jumatatu ya leo, nimepata fursa ya kuendelea na zile makala zangu, za Kwa Maslahi ya Taifa, makala ya leo nikihoji kuu umasikini wa Tanzania yetu na kupokea mikopo na misaada yenye masharti.

Naomba nianze kwa nukuu ya Mwalimu Nyerere kuwa "Umasikini mkubwa kabisa na mbaya kabisa, ni umasikini wa fikra" "poverty mentality"
Mwalimu akimaanisha kuwa umasikini mkubwa zaidi na mbaya zaidi, ni ukiwa na mawazo ya kimasikini.

Hivyo hoja kuwa Tanzania ni nchi masikini ni hoja muflisi kwa watu waliofilisika kimawazo, hivyo kitendo cha kuita nchi yetu kuwa nchi masikini, kunapalekea sisi kujisikia wanyonge.

Ukweli halisi kuhusu Tanzania, sio nchi masikini and has never been a poor county kwa sababu Tanzania ni nchi tajiri kwa utajiri mkubwa wa rasilimali za asili, madini, maliasli, mifugo, samaki, udongo wenye rutuba, vyanzo vya maji, vivutio vya utalii etc.

Kama Tanzania tuna utajiri wote huu, kwa nini nchi yetu bado ni masikini?. Naomba mimi nisilijibu swali hili, japo nakijua chanzo cha umasikini huu wa taifa letu, nisije nikachafua hali ya hewa ya bandiko hili.

Ndio maana, Rais wetu Dr. John Pombe Joseph Magufuli alipoingia tuu madarakani aliposema Tanzania sio masikini, Tanzania ni nchi tajiri na soon tutakuwa a Donner country wengi wetu tulimuunga mkono na kumpongeza.

Ila pamoja na utajiri wote huu tulionao, Tanzania bado hatujaweza kujitegemea na kujitosheleza, hivyo bado tunategemea misaada toka nchi wafadhili na Mashirika yao ya misaada na mikopo, likiwemo Shirika la IMF na World Bank.

CNN walipotangaza uongo huu,
CNN: Tanzania loses $300m World Bank loan amid crackdown concerns - JamiiForums

mimi ni miongoni mwa watu tulipinga na kushauri
Hata Nyerere alikataa, Rais Magufuli usikubali, shikilia msimamo. Tz tusikubali misaada na mikopo yenye masharti kuingilia sovereignty yetu - JamiiForums

Hivi kweli Tanzania ni masikini ki hivi hadi tupokee mikopo ya masherti hivi, na masherti mengine ni ya udhalilishaji wa uhuru wetu na viongozi wetu?.

Namalizia kwa hili swali,
Jee Tanzania ni Masikini Hivi Hadi Tuendelee Kupokea Mikopo na Misaada Yenye Masharti Kwa Ajili Tuu ya Umasikini Wetu, Au Tufike Mahali Tuwe Masikini Jeuri, Tukatae?

Wasalaam
Nawatakia Jumatatu Njema.
Paskali
Hoja nzuri mkuu, nilianzisha uzi jana wa kulaani vyombo vya habari vya nje kuangalia mabaya ya serikali ya Tanzania tu haswa hawa cnn, na bdye huo msaada waliposema kuwa wanautoa hivyo vyombo havikurusha hiyo habari nzuri kwa Tanzania kuwa benki ya dunia imeridhia kuuachia msaada iliyojuwa imegoma kuutoa, nilishangaa sana mods wakaufuta huo uzi kana kwamba wanafurahia hizi habar za nchi yetu kuandikwa kwa mabaya tu, mazuri no...na kuhusu hoja yako ya sisi kuwa maskini, ni ndio, hatujawa wa kujitegemea wenyewe hilo haliba ubishi, ila tukubali, tungekuwa tunajimudu wenyewe, tusingepewa mikopo kwa mashart ya kuvunja mila na destur za utamaduni wetu ili kuwafurahisha wazungu
 
Wanabodi,
Jumatatu ya leo, nimepata fursa ya kuendelea na zile makala zangu, za Kwa Maslahi ya Taifa, makala ya leo nikihoji kuu umasikini wa Tanzania yetu na kupokea mikopo na misaada yenye masharti.

Naomba nianze kwa nukuu ya Mwalimu Nyerere kuwa "Umasikini mkubwa kabisa na mbaya kabisa, ni umasikini wa fikra" "poverty mentality"
Mwalimu akimaanisha kuwa umasikini mkubwa zaidi na mbaya zaidi, ni ukiwa na mawazo ya kimasikini.

Hivyo hoja kuwa Tanzania ni nchi masikini ni hoja muflisi kwa watu waliofilisika kimawazo, hivyo kitendo cha kuita nchi yetu kuwa nchi masikini, kunapalekea sisi kujisikia wanyonge.

Ukweli halisi kuhusu Tanzania, sio nchi masikini and has never been a poor county kwa sababu Tanzania ni nchi tajiri kwa utajiri mkubwa wa rasilimali za asili, madini, maliasli, mifugo, samaki, udongo wenye rutuba, vyanzo vya maji, vivutio vya utalii etc.

Kama Tanzania tuna utajiri wote huu, kwa nini nchi yetu bado ni masikini?. Naomba mimi nisilijibu swali hili, japo nakijua chanzo cha umasikini huu wa taifa letu, nisije nikachafua hali ya hewa ya bandiko hili.

Ndio maana, Rais wetu Dr. John Pombe Joseph Magufuli alipoingia tuu madarakani aliposema Tanzania sio masikini, Tanzania ni nchi tajiri na soon tutakuwa a Donner country wengi wetu tulimuunga mkono na kumpongeza.

Ila pamoja na utajiri wote huu tulionao, Tanzania bado hatujaweza kujitegemea na kujitosheleza, hivyo bado tunategemea misaada toka nchi wafadhili na Mashirika yao ya misaada na mikopo, likiwemo Shirika la IMF na World Bank.

CNN walipotangaza uongo huu,
CNN: Tanzania loses $300m World Bank loan amid crackdown concerns - JamiiForums

mimi ni miongoni mwa watu tulipinga na kushauri
Hata Nyerere alikataa, Rais Magufuli usikubali, shikilia msimamo. Tz tusikubali misaada na mikopo yenye masharti kuingilia sovereignty yetu - JamiiForums

Hivi kweli Tanzania ni masikini ki hivi hadi tupokee mikopo ya masherti hivi, na masherti mengine ni ya udhalilishaji wa uhuru wetu na viongozi wetu?.

Namalizia kwa hili swali,
Jee Tanzania ni Masikini Hivi Hadi Tuendelee Kupokea Mikopo na Misaada Yenye Masharti Kwa Ajili Tuu ya Umasikini Wetu, Au Tufike Mahali Tuwe Masikini Jeuri, Tukatae?

Wasalaam
Nawatakia Jumatatu Njema.
Paskali
Hapana, Tanzania ni ya pili toka mwisho
 
kwenye uchumi fikra za mwalimu zilifeli, kitu cha msingi ni kujaribu kufanya kinyume cha sera zake za uchumi na ndicho awamu 3 zilizopita wamekifanya (kwa mafanikio kiasi). Tanzania ni miongoni mwa nchi masikini sana (ukiwa ndani ya nchi unaweza usilione hilo) hivyo kuwaletea jeuri wahisani kutawaumiza wananchi masikini zaidi. Joni na familia yake watakula na kulala kwa amani pale paradiso ya magogoni wakati masikini wakifa kwa stress za kufuatilia mafao yao!
Mimi sijuagi hata kwanini tunaonekana maskini hivyo kwenye list zao. Nimeenda nchi kama Cameroon,Malawi,Msumbiji, Central africa,Niger,Zambia na kujikuta nasema Bongo tuna afadhali mara 1000.
Kuna nchi ni maskini kama ubongo wa kuku.
 
Back
Top Bottom