Hivi mafundi cherehani wana laana gani?

Hivi mafundi cherehani wana laana gani?

Parabolic

JF-Expert Member
Joined
Dec 3, 2013
Posts
2,750
Reaction score
2,636
Nimekuwa nikizisikia tu kero za mafundi cherehani lakini na mimi yamenikuta.

Kuna fundi hapa Sinza Madukani nimempa suruali yangu apunguze kiuno, huu mwezi sasa imeshindikana.

Ilikuwa hivi, Nilipa suruali na hela kabisa ya kazi, akaniambia nifuate kesho yake. Ilikuwa Jumamosi, Jumapili sikwenda, nikaenda Jumatatu, akasema bado. Wiki hiyo nikapata safari ya wiki nzima mkoani.

Niliporudi akasema ndio ameanza kushona hivyo nije kesho yake. Bahati mbaya au nzuri nikapata tena safari.

Kurudi baada ya wiki anasema bado hajamaliza.

Jana nimekwenda sikumkuta. Leo nimemkuta eti anasema ile suruali haionekani hivyo nisubiri aitafute leo na kesho.

Hivi nimfanyeje huyu fundi? Halafu ni mtu mzima na heshima zake na ana ofisi kubwa tu!
 
Nimekuwa nikizisikia tu kero za mafundi cherehani lakini na mimi yamenikuta.
Kuna fundi hapa Sinza Madukani nimempa suruari yangu apunguze kiuno, huu mwezi sasa imeshindikana.
Ilikuwa hivi. Nilipa suruali na hela kabisa ya kazi, akaniambia nifuate kesho yake. Ilikuwa jumamosi, jumapili sikwenda, nikaenda juma tatu, akasema bado. Wiki hiyo nikapata safari ya wiki nzima mkoani.
Niliporudi akasema ndio ameanza kushona hivyo nije kesho yake. Bahati mbaya au nzuri nikapata tena safari. Kurudi baada ya wiki anasema bado hajamaliza.
Jana nimekwenda sikumkuta. Leo nimemkuta eti anasema ile suruali haionekani hivyo nisubiri aitafute leo na kesho.
Hivi nimfanyeje huyu fundi? Halafu ni mtu mzima na heshima zake na ana ofisi kubwa tu!

Watu ka hawa unatungua tu na manati ya mzungu.
 
Hawa mafundi wameweka kipaumbele kwa wanawake ila kama we ni ME, sahau kupatiwa huduma kwa wakati muhafaka.
 
Maji yakimwagika huwa hayazoleki ni kushukuru mungu tuu
 
Wanapenda kufanya kazi za wanawake ili waje wawashike shike ma.t.a.k.o kwenye kuwapima. Ila kama wewe ni mwanaume ni kama unampotezea muda wake tu
 
Hiyo style ya kupoteza nguo ameiwahisha mbona? Huwa n ya mwisho kuna zinazo tangulia mf ninauguza njoo kesho,jiran ana msiba sikuwepo kazin,vdonda vya tumbo vinasumbua Nina siku 3 sijaja kazini, vipimo nilipoteza nikupime tena,duka ninalonunua material limefungwa jamaa kafata mzigo mbeya,etc af ndo unakuja hiyo ya kupoteza sasa

Ushaur

Mkazie haswa, km vp ondoka na kichwa cha cherehan, au pi ga mkwara umepata dharura tarime mdogo wako amekata MTU kichwa hivyo baada siku 7 unakuja kuchukua nguo. Naamin utaikuta had ameipasi
 
Ulikosea, ulipeleka nguo ikalekebishwe na Fundi Cherehani? yeye anajua kutengeneza chereheni mbovu, imekula kwako...! Next time peleka kwa Fundi nguo anayetumia cherehani wengi wao ni Wangoni. Ukifika msalimie "moniile" akikujibu mpe nguo, tangu lini Fundi nguo akawa mzaramo?
 
Yaan mie sipati kusema kero za mafundi nguo. Kuna fundi kakaa na kitenge changu 2yrs now. Kila nikienda ananipiga kalenda. Mpaka nachoka saasa
 
Yaan mie sipati kusema kero za mafundi nguo. Kuna fundi kakaa na kitenge changu 2yrs now. Kila nikienda ananipiga kalenda. Mpaka nachoka saasa

We acha tu kuna siku nina sendoff ya best frend nikampa fundi anishonee week hola kila nkienda nenda rudi...
We siku nikamuamulia akaishona usiki giza na mwanga wa simu yake ya torch...
daaa halafu inakera ujue wewe umekasirika mwenzako hakasiriki....
 
We acha tu kuna siku nina sendoff ya best frend nikampa fundi anishonee week hola kila nkienda nenda rudi...
We siku nikamuamulia akaishona usiki giza na mwanga wa simu yake ya torch...
daaa halafu inakera ujue wewe umekasirika mwenzako hakasiriki....

Yaan inaboaje!!
 

Hawa jamaa ni mabingwa wa kuuguza na kufiwa.

Na ukimchekea eti kisa mtu mzima,itakula kwako.

 
Back
Top Bottom