Hivi mafundi cherehani wana laana gani?

Hivi mafundi cherehani wana laana gani?

Kesho kama haitapatikana namsamehe tu pamoja na hela ya kushonea. Maana ndio anachokitaka
 
Nimekuwa nikizisikia tu kero za mafundi cherehani lakini na mimi yamenikuta.
Kuna fundi hapa Sinza Madukani nimempa suruari yangu apunguze kiuno, huu mwezi sasa imeshindikana.
Ilikuwa hivi. Nilipa suruali na hela kabisa ya kazi, akaniambia nifuate kesho yake. Ilikuwa jumamosi, jumapili sikwenda, nikaenda juma tatu, akasema bado. Wiki hiyo nikapata safari ya wiki nzima mkoani.
Niliporudi akasema ndio ameanza kushona hivyo nije kesho yake. Bahati mbaya au nzuri nikapata tena safari. Kurudi baada ya wiki anasema bado hajamaliza.
Jana nimekwenda sikumkuta. Leo nimemkuta eti anasema ile suruali haionekani hivyo nisubiri aitafute leo na kesho.
Hivi nimfanyeje huyu fundi? Halafu ni mtu mzima na heshima zake na ana ofisi kubwa tu!
Hakuna fundi yeyote mwaminifu awe seremala, umeme, nyumba, gari/pikipiki/baiskeli, TV, simu, saa. Sijui wamelaaniwa. Nilimpa fundi simu yangu aiflash nikafuatilia mwaka mzima mpaka nikaamua kusamehe.
 
mafundi wengi ni waongo ila mafundi nguo wamezidi me kuna fundi nguo ilibaki kidogo tu tupigane ngumi.

nimempa nguo yangu arekebishe akaniambia kesho itakuwa tayari, kesho sikupata nafasi nikamuibukia baada ya week sikumkuta nilikuwa nimetoa pesa nusu ila nguo haijarekebishwa nikaichukua nikampelekea fundi mwingine.

kesho yake napita zangu mtaani nikamkuta fundi ofisini kwake namuuliza eti anabisha na analeta ubabe weee! ilibaki kidogo tu tupigane ngumi jiwe.
 
Kakihusudu kidudu chako, huwa anatililia mwenyewe anapoenda kwa mrembo wake. Mvizie utakuta kidudu chako kimetinga kiunoni kwake tena na mkanda wa haja.
 
Mafundi wengi Ni waongo, Ila hii yote inasabishwa na tamaa na uvivu, hivi ingekuwaje kama tungekuwa kama Una mpenzi Wako unampa gegedo lako akakutimizie hamu yako nyumbani halafu kesho akurudishie, nadhani wengine ingefika hadi muda WA kuoa hajarudishiwa gegedo lake
 
Alafu km wamesomea saikolojia hta uwatukane vp hawakasiriki anakufariji tu
 
mgegede, shenz kabisa.., mi nilifanyiwa ufirauni wa kimbwa kama huo na fundi pasi.., nilimpa na pesa kabisa.., ikabidi nimwachie tu.
 
Na umefanya vibaya ulivomlipa kabisa.

Kuna bro mmoja yeye fundi viatu alikua anamzusha ivo ivo. Siku ya siku alimuamulia tu, keshachoka nenda rudi alimpiga kibao kimoja tu fundi alizunguruka kama pia, then jamaa akabeba viatu vyake huyooo.

Mie siku hizi nimeamua kwenda kutundua tu dukani, nimechoka kuhangaishwa nao. Anaenipata fundi wa uniform za wanangu tu za shule maana ndo sina la kufanya
 
Watanzania wana vituko! Eti suruali ipunguzwe kiuno, ina maana umekonda au ulinunua ukiwa hujui size ya kiuno chako?
 
Kuna fundi seremala nilimpa kazi yangu na hela nusu ili akimaliza nimlipe kiasi kilichobaki. Ulipita mwaka Mzima ndiyo akamaliza kazi yangu. Aliponikabidhi nikamwambia sikiliza, pesa iliyobaki nitakulipa baada ya mwaka Mzima kama ulivyonifanyia. Jamaa alilalamika sana, nikamwambia na wewe sikilizia kidogo hiyo adha
 
Back
Top Bottom