Hivi maana halisi ya 'Madhabahu' ni nini? Kwanini Bwana huwapa baraka ya kudumu wanaomjengea 'Madhabahu'?

Hivi maana halisi ya 'Madhabahu' ni nini? Kwanini Bwana huwapa baraka ya kudumu wanaomjengea 'Madhabahu'?

Mikopo Consultant

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2024
Posts
2,235
Reaction score
4,382
Nimejeuka kusoma soma Biblia kwa hii miezi michache, kuna jambo kama limeitekenya akili yangu. Kwanza, kwenye agano la kale, waliopewa uongozi wote waliishia kumjengea Bwana Madhabahu. Nuhu, Abrahamu, Daudi etc etc

Na kwenye agano la kale, 'Madhabahu' imetajwa sana. Katika kusoma kwangu, kwenye agano la kale, madhabahu imeonekana kama ni mahali physical ambapo ni maalumu kumtolea Bwana sadaka na kuzungumza naye.

Na ukiendelea kusoma Biblia, kuna mahali inakuambia 'Madhabahu' inazungumza.

Lakini kitu kingine nilichogundua, kuna madhabahu ya utawala wa Bwana na madhabahu ya shetani (hii niliijua baada ya kusoma ufunuo)

Sasa jamani, embu tutete hili suala.

Hivi kwa sasa, unamjengea vipi Bwana madhabahu?

Na madhabahu ni kitu gani haswa, kwa lugha ya picha na kiroho?
 
Nimejeuka kusoma soma Biblia kwa hii miezi michache, kuna jambo kama limeitekenya akili yangu. Kwanza, kwenye agano la kale, waliopewa uongozi wote waliishia kumjengea Bwana Madhabahu. Nuhu, Abrahamu, Daudi etc etc

Na kwenye agano la kale, 'Madhabahu' imetajwa sana. Katika kusoma kwangu, kwenye agano la kale, madhabahu imeonekana kama ni mahali physical ambapo ni maalumu kumtolea Bwana sadaka na kuzungumza naye.

Na ukiendelea kusoma Biblia, kuna mahali inakuambia 'Madhabahu' inazungumza.

Lakini kitu kingine nilichogundua, kuna madhabahu ya utawala wa Bwana na madhabahu ya shetani (hii niliijua baada ya kusoma ufunuo)

Sasa jamani, embu tutete hili suala.

Hivi kwa sasa, unamjengea vipi Bwana madhabahu?

Na madhabahu ni kitu gani haswa, kwa lugha ya picha na kiroho?
Madhabahu
1. Kimwili: ni mahali ambapo dhabihu huwekwa juu yake na kutolea kwa Mungu. Ni jiwe, ardhi, altare, ubao, etc
2. Kiroho: ni mahali pa kukutana na Mungu. Pahali pa sala na maombi. Ni moyo wa mtu mbele ya Mungu wake. Ni nafasi ya Mungu katika maisha ya mwanadamu. Ni yale yote yanayomkutanisha mwanadamu na Mungu.
 
Nimejeuka kusoma soma Biblia kwa hii miezi michache, kuna jambo kama limeitekenya akili yangu. Kwanza, kwenye agano la kale, waliopewa uongozi wote waliishia kumjengea Bwana Madhabahu. Nuhu, Abrahamu, Daudi etc etc

Na kwenye agano la kale, 'Madhabahu' imetajwa sana. Katika kusoma kwangu, kwenye agano la kale, madhabahu imeonekana kama ni mahali physical ambapo ni maalumu kumtolea Bwana sadaka na kuzungumza naye.

Na ukiendelea kusoma Biblia, kuna mahali inakuambia 'Madhabahu' inazungumza.

Lakini kitu kingine nilichogundua, kuna madhabahu ya utawala wa Bwana na madhabahu ya shetani (hii niliijua baada ya kusoma ufunuo)

Sasa jamani, embu tutete hili suala.

Hivi kwa sasa, unamjengea vipi Bwana madhabahu?

Na madhabahu ni kitu gani haswa, kwa lugha ya picha na kiroho?
Madhabahu ni eneo mahususi ambapo kiimani Mungu huja moja kwa moja, yeye mwenyewe kwa dhumuni la kukutana na mwanadamu, hicho kitendo huitwa ibada. Na ili iwe safi (takatifu) ni lazima iandaliwe na kutakaswa.

Kikristo, baada ya Yesu kuja duniani, kufa msalabani na kufufuka, madhabahu zote za kimwili zilifutwa, na madhabahu ikabakia kuwa ni moja tu, na kila mtu atakuwa nayo, nayo ni Moyo wako. Na kuufanya moyo uwe safi (mtakatifu) kufaa kutumiwa na Mungu kama madhabahu ni lazima itakaswe kwa damu ya Yesu (ukiri wa kafara ya Yesu kufa msalabani).
Maandiko ni haya.

YEREMIA 31:33
Baada ya siku hizo, nitafanya agano lifuatalo na Waisraeli: Nitaiweka sheria yangu ndani yao, na kuiandika katika mioyo yao. Mimi nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

WAIBRANIA 8:10
Hili ndilo agano nitakalofanya na watu wa Israeli siku zijazo, asema Bwana: Nitaweka sheria zangu akilini mwao, na kuziandika mioyoni mwao. Mimi nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.

YOHANA 4:24
Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.

UFUNUO 3:20
Tazama, nasimama mlangoni napiga hodi. Mtu ye yote akisikia sauti yangu na kufungua mlango, nitaingia ndani na kula pamoja naye, naye pamoja nami.
 
Nimejeuka kusoma soma Biblia kwa hii miezi michache, kuna jambo kama limeitekenya akili yangu. Kwanza, kwenye agano la kale, waliopewa uongozi wote waliishia kumjengea Bwana Madhabahu. Nuhu, Abrahamu, Daudi etc etc

Na kwenye agano la kale, 'Madhabahu' imetajwa sana. Katika kusoma kwangu, kwenye agano la kale, madhabahu imeonekana kama ni mahali physical ambapo ni maalumu kumtolea Bwana sadaka na kuzungumza naye.

Na ukiendelea kusoma Biblia, kuna mahali inakuambia 'Madhabahu' inazungumza.

Lakini kitu kingine nilichogundua, kuna madhabahu ya utawala wa Bwana na madhabahu ya shetani (hii niliijua baada ya kusoma ufunuo)

Sasa jamani, embu tutete hili suala.

Hivi kwa sasa, unamjengea vipi Bwana madhabahu?

Na madhabahu ni kitu gani haswa, kwa lugha ya picha na kiroho?
Madhabahu maana yake Machinjio
Kwa Kiingereza " Butchery "
 
Madhabahu
1. Kimwili: ni mahali ambapo dhabihu huwekwa juu yake na kutolea kwa Mungu. Ni jiwe, ardhi, altare, ubao, etc
2. Kiroho: ni mahali pa kukutana na Mungu. Pahali pa sala na maombi. Ni moyo wa mtu mbele ya Mungu wake. Ni nafasi ya Mungu katika maisha ya mwanadamu. Ni yale yote yanayomkutanisha mwanadamu na Mungu.
Nimekuelewa kabisaa
 
Madhabahu ni eneo mahususi ambapo kiimani Mungu huja moja kwa moja, yeye mwenyewe kwa dhumuni la kukutana na mwanadamu, hicho kitendo huitwa ibada. Na ili iwe safi (takatifu) ni lazima iandaliwe na kutakaswa.

Kikristo, baada ya Yesu kuja duniani, kufa msalabani na kufufuka, madhabahu zote za kimwili zilifutwa, na madhabahu ikabakia kuwa ni moja tu, na kila mtu atakuwa nayo, nayo ni Moyo wako. Na kuufanya moyo uwe safi (mtakatifu) kufaa kutumiwa na Mungu kama madhabahu ni lazima itakaswe kwa damu ya Yesu (ukiri wa kafara ya Yesu kufa msalabani).
Maandiko ni haya.

YEREMIA 31:33
Baada ya siku hizo, nitafanya agano lifuatalo na Waisraeli: Nitaiweka sheria yangu ndani yao, na kuiandika katika mioyo yao. Mimi nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

WAIBRANIA 8:10
Hili ndilo agano nitakalofanya na watu wa Israeli siku zijazo, asema Bwana: Nitaweka sheria zangu akilini mwao, na kuziandika mioyoni mwao. Mimi nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.

YOHANA 4:24
Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.

UFUNUO 3:20
Tazama, nasimama mlangoni napiga hodi. Mtu ye yote akisikia sauti yangu na kufungua mlango, nitaingia ndani na kula pamoja naye, naye pamoja nami.
Amen mkuu, umeeleweka vyema kabisa, maana yake sala na ibada ndo kila kitu
 
Back
Top Bottom