Hivi Laana ni nini?

Hawa wao walilaaniwa na mungu ?! Mbona watu humsingizia shetani ndiye mwenye kulaani watu na sio mungu?!
OK, laana zote zinatoka kwa Mungu na sio watu tunakua tunajidanganya tu.
Na mara nyingi anaelaaniwa ni yule ambae atakua anatenda Dhabi ambazo zimezidi kiwango...
Kwa mfano kusema "hakuna Mungu" hii ni laana kwa huyo mtu ambayo atalaaniwa na huyo ambae anasema hayupo angali yupo.
Vipo vitu vitu duniani ambavyo vimelaaniwa na hata mtumiaji akiwemo.
 
WAKUU neno laana uslitafsiri kwa elim ulio nayo hutoweza hata kidogo, Laana nineno kubwa niongoni mwa maneno makubwa sana!" LAANA INATOKEA KWA MTU YEYOTE ALIE FANYA MABAYA MAKUU, HAIWEZEKANI UKATENDA MEMA KISHA UKA LAANIWA, MFANO umedhulumu mali ya kanisa au msikiti nilazima waumini wataumia sana nyoyo zao na nafsi pia, katka hilo pia MUNGU HAPENDI KITENDO ULICHO KIFANYA, HAPA MAJIBU YAKE WAUMINI WAMEMUACHIA MUNGU MAANA YEYE NDIE MUWEZA WA YOTE, JAPO KUTAKUWEPO MAOMBI KWA WAUMINI HAO, HAKIKA MUNGU ATAJIBU, MAANA MUNGU MWENYEWE AMEKATAZA UHALIFU KAMA WIZI NK. NI HALI KADHALIKA UKIMFANYIA UBAYA MWENNZO ALIE KUTENDEA WEMA SIKU ZOTE, MFANO MAMA KAKUBEBA TUMBONI MIEZ9 KAKULEA MIAka yote, Matokeo yake unamdharau na kumpuuza, humueshimu nk, Akichukia lazima udhurike maana hata mungu Anachukia matendo hayo, HESHIMA,HEKIMA NA BUSARA NI VITU VIKUBWA SANA,, UKIVIKOSA VYOTE HIVYO LAZIMA UWE NI MTU USIE ENDANA NA JAMII MAANA YAKE UMEINGIWA NA NA LAANA AU BALAA, NA MUTU HUYO AKIFA MAISHA YAKE NIMOTONI
Hivyo Hekima, Heshima na Busara ndiyo chanjo au ya laana?! Unapataje hekuma na busara kama hunazo?! Je laana hutolewa na Wazazi au ni mungu hutoa hii laana?! Wazazi wana umri stahiki wa kutoa laana au mzazi umri wowote anaweza kulaani?! Vipi mtu asiye mzazi wako anaweza kukulaani pia?! Sifa za mlaani au mtoa laana ni zipi?!
 
OK, laana zote zinatoka kwa Mungu na sio watu tunakua tunajidanganya tu.
Na mara nyingi anaelaaniwa ni yule ambae atakua anatenda Dhabi ambazo zimezidi kiwango...
Kwa mfano kusema "hakuna Mungu" hii ni laana kwa huyo mtu ambayo atalaaniwa na huyo ambae anasema hayupo angali yupo.
Vipo vitu vitu duniani ambavyo vimelaaniwa na hata mtumiaji akiwemo.
Hapa nahitaji elimu, huwa nasikia dhambi zina uzito sawa kwenye mzani wa mungu, kwamba hakuna dhambi kubwa wala ndogo. Unaposema unapata laana kwa dhambi zilizozidi kiwango, kiwango cha kawaida cha dhambi ni kipi na nikiasi gani unakua umezidi/umezidisha?!
Kwa maelezo yako ni mungu tu ndiye anatoa laana, kumbe hii nadharia ya wazazi au babu/bibi kulaani ni uongo tu?! Na nikimkosea mungu tu ndiye atanilaani na ndiye mwenye mamlaka, vipi nikikukosea wewe na nisikuombe msamaha, hii ikoje?!
 
Huwa siamini sana kwenye huu ' Upuuzi / Uswahili ' kwani kuna Mtu mmoja nakumbuka aliambiwa na tena akahakikishiwa kuwa ' atalaaniwa ' ili maisha yampige na awe ' hohehahe / masikini ' wa kutupwa lakini cha kushangaza hadi hivi sasa huyo Jamaa ( aliyeambiwa atalaaniwa ) ana Hela / Pesa na zinazidi tu kumtembelea na maendeleo kibao / lukuki huku Yule Yule aliyetamba ' Kumlaani ' umasikini ndiyo umemzidi hadi katika ' Kope ' zake za macho.
mkuu umeelewa tofauti, laana sio kukosekana kwa pesa hapana, haiko hivyo duuh!!* kiufupi mimi siwezi nikakusababishia wewe ulaanike kw matamko tuu!!, nilitoa mfano kama ulinisoma, kwmba laana nikitu kikubwa sana, ukitaka kujuwa laana ni nini mpige mama yako au mtukane, au fanya kitu kibaya chochote kw mzazi wako kwa makusudi, yaani kusudia kufanya kitu kw wazee wako, huu ni mfano wa haraka haraka tu,, lingine em telekeza family yako kwa makusudi tu, Jamba ambalo mungu mwenyewe anahudhunika, **** jamaa alitelekeza familia yake yaani mke tena anamtoto mchanga kabisa, siku moja akarudi nyumbani Saa 9 mchana akamkuta mama anabembeleza mtoto wake akamsalimiavkabla mama hajaitikia salam mtoto akamsemesha baba yake, kwa mara yakwanza mtoto mchanga akaongea kwa kumwambia Baba kwanini Unatutesaa???# mtoto hakurudiavkusema chochote,, Na baba aliondoka kama kaenda kukojoa ndo mazima hadi leo zaidi ya miaka 20* hajulikani alipo wala fununu.
 
Dah....usiumize kichwa...laana ni neno rahisi LA kisiasa lenye kumaananisha kutounga mkono tukio fulani....Tanzania yalaani ndoa za mashoga.....Trump alaani majaribio ya makombora ya Korea....wala hata Prof mshana jr hahitajiki pia hata kiingereza hakihitajiki ili uelewe
Hahaha huwa wanasema eti huu uongozi umelaanika, kumbe siasa tu. Wanapotoa/kutumia hili neno (laani) huwa ni katazo au tangazo?!
 
Ukiangalia mambo yanayofanywa na serikali ya Tanzania utaelewa nin maana ya laana. Mfano mwanasiasa eg. Mbunge ambaye hajasoma na kaipata kazi yake kwa rushwa na wizi wa kura tena kwa kupga kelele majukwaan kwa muda wa mwezi mmoja tu analipwa vizur na anaenjoy maisha zaid kuliko daktari aliesomea kazi yake miaka 5 tena kwa mkopo ambao ni lazima alipe huk akilipishwa kodi kubwa akinyimwa haki zake za msingi kama nyumba(malazi) na usafiri pale anapoajiriwa hata vya mkopo. Mfano mwingne pale kiongozi anapohimiza wananchi wachague kiongozi wa chama tawala ili wasipatwe na madhira ya kubomolewa nyumba zao pale watakapochagua kiongozi toka upinzan. Hii ndo maana halisi ya laana. In shot ukipata laana unafanya mambo bila commom sense. Binafsi nimeshindwa kabisa kua mzalendo kwenye hili taifa lililojaa laana.
 
Laana ni deni ya kisasi cha mtu kwa mtu aliemkosea against pure coincidences ya matatizo yanayompata yule mtu mkosaji..Hakuna scientific correlation kabisa!
Naamini wote tunakoseana at one point in life, ndii kusema woote tumelaanika/tumelaaniwa.
Matatizo watu husema ni sehemu ya maisha, ni matatizo kiasi gani ukipata utasema hii ni laana na ni kiasi gani utasema hii ni kawaida/sawa na sio laana.
Kwa maana yako Laana is direct proportional to dhambi/makosa/matatizo. Laana nyingi matatizo mengi, laana kidogo matatizo kidogo?!
 
Hahaha yani kwa ki hebrania mnaita Depression kukosa raha ya nafsi. Lakini hii inadawa kule hospitali huwa wana vidonge vya anti-depressants, Na ukiachilia hiyo, hili la mafanikio ni kiasi gani mtu ukifanikiwa unasema hujalaanika au hakuna limit ya juu ya mafanikio je limit ya chini au minimum success ni kiasi gani ili kusema hujalaanika?!

Swali lako ni zuri lakini linahitaji mjadala mpana Kama topic inayojitegemea!
 
Ukiangalia mambo yanayofanywa na serikali ya Tanzania utaelewa nin maana ya laana. Mfano mwanasiasa eg. Mbunge ambaye hajasoma na kaipata kazi yake kwa rushwa na wizi wa kura tena kwa kupga kelele majukwaan kwa muda wa mwezi mmoja tu analipwa vizur na anaenjoy maisha zaid kuliko daktari aliesomea kazi yake miaka 5 tena kwa mkopo ambao ni lazima alipe huk akilipishwa kodi kubwa akinyimwa haki zake za msingi kama nyumba(malazi) na usafiri pale anapoajiriwa hata vya mkopo. Mfano mwingne pale kiongozi anapohimiza wananchi wachague kiongozi wa chama tawala ili wasipatwe na madhira ya kubomolewa nyumba zao pale watakapochagua kiongozi toka upinzan. Hii ndo maana halisi ya laana. In shot ukipata laana unafanya mambo bila commom sense. Binafsi nimeshindwa kabisa kua mzalendo kwenye hili taifa lililojaa laana.
Hivyo serikali imelaanika?! Nani kailaani?! Hawa watawala wamelaanika?! Operational standard ya serikali ni ipi ili tuifuate, yani tuipe scale kwamba hapa normal, hapa below na hapa ni high au beyond normal ili ikifanya tunajua hii ni abnormal, and it is out normalcy.
Duh Laana siyo mchezo.
 
Swali lako ni zuri lakini linahitaji mjadala mpana Kama topic inayojitegemea!
Hahaha anzisha uni tag tueleweshane. Au tiririka hapa kwa faida ya JF members, it is gratifying to dare to empty with no fear or malice or prejudice.
Leta vitu mkuu hii JF hakuna limit panuka tu.
 
Dhambi zinazidiana kuna kubwa na ndogo, kuzini kunatofautiana na kutukana wazazi wako.
Hahaha huu mzani wako wa dhambi au wa mungu /high power?! Unatumia kigezo/standard gani kuipa zinaa uzito mkubwa au Tusi kwa mzazi linakuwaje na uzito mkubwa kuliko tusi kwangu au kwako?! Nimewahi kuambiwa dhambi ni dhambi tu hakuna iliyo kuu. Nitaanza kuzipima inawezekana una point nisiyoiona.
 
Mfano wa mafanikio ni Kama vile;
Umeshawahi kuona Mtu ana Mali Kama vile majumba lakini wanaofaidika ni watu baki!
Wapangaji wanaishi hawalipi kodi wala nini !
Yani sijui ni semeji
 
Mfano wa mafanikio ni Kama vile;
Umeshawahi kuona Mtu ana Mali Kama vile majumba lakini wanaofaidika ni watu baki!
Wapangaji wanaishi hawalipi kodi wala nini !
Yani sijui ni semeji
Kwa mfano wako nilidhani huyo mtu sasa ana neemeka kwa baraka kusaidia wenzake?! Mpangaji halipi kwamba hataki au mwenye nyumba hapokei pesa kwa sababu kalaanika?!
Hivi ile kusaidia bila kujali au kiebrania mnaita good samaritan au kujitolea ina maana gani ikiwa kila kitu kinapimwa kwa faida.
Ni lini mtu atapata baraka/rehema au positive karma kwa kusaidia wengine/watu baki.
 
Naamini wote tunakoseana at one point in life, ndii kusema woote tumelaanika/tumelaaniwa.
Matatizo watu husema ni sehemu ya maisha, ni matatizo kiasi gani ukipata utasema hii ni laana na ni kiasi gani utasema hii ni kawaida/sawa na sio laana.
Kwa maana yako Laana is direct proportional to dhambi/makosa/matatizo. Laana nyingi matatizo mengi, laana kidogo matatizo kidogo?!


Mshua

Yaani sentensi yangu ya pili nimeikataa kabisa ile definition ya kutoka sentensi yangu ya kwanza.Definition yangu ni very abstract,ni hypothetical ambapo kiuhalisia si kweli...

Unachokisema ni sawa kabisa.Ni ishu very subjective,na kitu kishakua subjective kinakua si halisi kabisa.

Laana ni kitu kisichokuwepo kiukweli...Ni hypothetical belief tu mkuu.

Yaani nakuelewa sana jembe!
 
Laana ni tendo linalompata mtu linalosababisha mtu huyo kupata mikasa mbalimbali na hata akienda kutibiwa kwa waganga wa kienyeji mikasa haitoki ,akiombewa kanisani pia haitoki.

Na hii humtokea mtu aliyedharau mzazi wake baada ya mtu huyo kujua MWEMA na mabaya yeye hawatendei mema wazazi wake.

Lakini pia anakuwa na tabia ya kuwatendea mabaya watu ambao hawana uwezo wa kumlipa kisasi kwa sababu mbali mbali za kiuwezo hivyo manung' uniko,kilio na malalamiko yao hupelekea kumdhuru yule anayewatendea, wakati mwingine kizazi chake kinaweza kupatwa na madhara yaliyotikana na hayo matendo yaliyotendwa na huyo aliyejiona yeye huwezi kupata madhara.

Laana haionekani kwa macho tena ni ugonjwa hatari hauna tiba wala chanjo kwa mtu lakini una kinga tu! Na kinga Yake ni kuacha k kufanya hayo niliyoeleza hapo juu.
umemaliza mkuu, kiziwi hawezi kisikia hata ukipiga kipenga ktk masikio yake
 
Kwa mfano wako nilidhani huyo mtu sasa ana neemeka kwa baraka kusaidia wenzake?! Mpangaji halipi kwamba hataki au mwenye nyumba hapokei pesa kwa sababu kalaanika?!
Hivi ile kusaidia bila kujali au kiebrania mnaita good samaritan au kujitolea ina maana gani ikiwa kila kitu kinapimwa kwa faida.
Ni lini mtu atapata baraka/rehema au positive karma kwa kusaidia wengine/watu baki.

kwa aliyekusudia kufanya hivyo kwa ajili ya kusaidia watu yaweza kuwa baraka.
Lakini kwa Mtu mwenye laana yeye Hata hajielewi yupo yupo tu!
Nimependa michango yako iko na changamoto ndani Yake !
 
Hahaha karibu tuendelee kuchangia, tueleweshane zaidi.
kwa aliyekusudia kufanya hivyo kwa ajili ya kusaidia watu yaweza kuwa baraka.
Lakini kwa Mtu mwenye laana yeye Hata hajielewi yupo yupo tu!
Nimependa michango yako iko na changamoto ndani Yake !
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom