Hivi Kwanini Lowassa anautaka Urais?

Heshima Mbele

Ni muda sijaanzisha Mada hapa ila kuna jambao ambalo limekuwa likinitatiza kwa muda sasa ila naamini nyie mnaweza kuwa mnajua?

Hivi kwanini Lowassa anautaka Urais? akichaguliwa atalisaidiaje Taifa? Je, Pesa hizi anazotumia kuweka watu wake kwenye Chama tawala atazirudishaje?

Nimeanza kuogopa sana na kama watanzania wakikubali kuzugwa tena 2015 na kuchagua viongozi ambao wana mvuto wa sura, mvuto wa kutawala bila kuangalia rekodi yao ya nyuma taifa litaenda kubaya sana.

Taifa linaoelekea kupata Gesi na Mafuta linahitaji viongozi makini ambao wataweza kulivusha taifa, kutuondoa kwenye lindi la umasikini na kujenga utawala bora.

We shall cross the bridge when we get there. But how far is the bridge from here and now? How do we know there is a bridge ahead? How do we know we will get there?
 
Kwa kua ana vigezo vya kuiongoza nchi katika haki na kweli.Vile vile ni chaguo la Mungu kama alivyotabiriwa na Mtumishi wa mungu TB JUSHUA wa emmanuel Tv.

Nadhani tunatakiwa kufikiri kwa kina zaidi hasa tukikumbuka maneno ya mwalimu aliposema serekali corupt haiwezi kuwa huru hata siku moja na haiwezi kutenda haki. SIKU zote itakuwa ikiwatumikia wale walioiweka madarakani kwa maslahi yao na kamwe haiwezi kuwatumikia wananchi. Nikimuangalia El na wapambe wake na fedha wazotumia kupata uongozi ni zahiri wanaiwinda ikulu kwa maslahi yao binafsi na tusitegemee kwamba wataweza kuifikisha tanzania kwenye kilele cha mafanikio. Wale wanaodai kwamba sifa anazo ni sifa zipi hizo je nikuingia mkataba wa kitapeli wa richmond wa kuilipa kampuni hiyo Tshs 152 Millioni kwa siku huku watanzania wakibebeshwa mzigo wa malipo hayo na fedha hizo zikienda mifukoni kwa watu? Je hii ndiyo sifa?

Hebu tuangalie matatizo tuliyonayo na tumuombe mungu atuinulie mtu atakaye weza kutuondolea matatizo haya tusiangalie sura, Jina, dini au pesa za mtu bali tuangalie uwezo na nia ya dhati aliyonayo mtu. Hata baba wa taifa mwalimu aliwahi kusema mkitaka kuchagua kiongozi ji ulizeni kwanza ni matatizo yepi tuliyo nayo na ni nani kati ya wale watakaojitokeza kugombea uongozi anaweza kutusaidia kutatua matatizo hayo. tusishabike tu fulani anaweza au fulani ana mvuto kama tulivyofanya 2005 na baadae tukajikuta tunajuta na kulaama.
 
Back
Top Bottom