Mr Tyang
JF-Expert Member
- Sep 30, 2018
- 1,728
- 6,803
Ndugu zangu Viongozi na wanachama wote wa CDM bila kupoteza Muda naomba niwape ujumbe wangu huu kwa leo;
"Ni dhahili na ukweli usiopingika kuwa idadi ya Watanzania ambao wamekuwa wakijitokeza kwenye kampeni za CDM Ni ndogo mno ukilinganisha na matarajio yaliyokuwepo, Mfano hakuna alietegemea Kama kwenye ufunguzi wa kampeni pale Mbagala kutakuwa na idadi ndogo vile ya Wananchi utafikiri kampeni za mbunge au udiwani wakati Ni ufunguzi wa kampeni za Chama Tena chini ya mgombea urais kabisa, pia hata Jana pale kawe hiyo idadi ilikuwa ndogo Sana ukilinganisha na idadi ya kawe wakati wa Lowassa ".
JE NIWAPI MNAKOSEA HADI MNAKOSA WATU? JIBU HILI HAPA;
"DSM Ni jiji lenye mishemishe nyingi na watu wake Ni wenye mishemishe nyingi, hivyo usipopanga Ratiba zako vizuri kwa kuangalia na Ratiba zingine zinazoendelea ndani ya jiji Hilo Basi tegemea kujikuta upo mwenye tu katika hiyo Ratiba yako"
Hivyo Basi kosa kubwa walilolifanya waratibu kampeni za CDM walishindwa kupanga Ratiba za kampeni kwa kuendana na Ratiba za matukio muhimu yanayoendelea DSM, na hizi ndo hesabu za Ratiba zilizowachenga;
1. Ufunguzi wa kampeni siku ya ijumaa; Ndg zangu CDM mnatambua kabisa siku ya ijumaa huwa Kuna Ibada ya ijumaa ambayo Watoto, wanawake na wanaume huenda kuswalia msikitini kwa pamoja, na Mbagala Ni sehemu iliyo na waisilam wengi hivyo haikuwa rahisi watu wasitishe shughuli Yao mhimu ya kwenda kuswali kisa kwenda kuwasikiliza wanasiasa.
2. Kuendelea kwa kampeni Jana Kawe; waratibu kampeni za CDM walishindwa kuoanisha tukio kubwa lililokuwa linatokea Jana na tukio lao. Niukweli usiopingika kuwa, Ufunguzi wa kampeni za CCM Jana ulikuwa ukifuatiliwa na Watanzania wengi Sana waliokuwepo Dodoma na ambao hawakuwepo Kupitia mitandao na vyombo vya habari Kama TV, na hii nikutana na uzito wa chama hicho pia kuwa na wanachama wazito na wenye ushawishi katika jamii pia uwepo wa wasanii Wakubwa Tanzania Kama diamond, Konde boy , Alikiba, Nandy na n.k kuliongeza idadi ya Watanzania wengi wasing'atuke kwenye tv zao.
Hivyo Basi kwa maelezo hayo Wakazi wengi wa dar es salam waliungana na Watanzania wenzao kutoka mikoa mingine kufuatilia kilichokuwa kinaendelea pale Dodoma katika viwanja vya Jamuhuri na kujikuta wamekosa muda wa kuja kawe kwenye kampeni zenu. (Ikumbukwe Kuna baadhi ya wasanii waliokuwepo Jana Wana wafuasi wengi na mashabiki wao wengi kuliko hata baadhi ya wafuasi wa vyama baadhi hapa nchini).
3. Mkutano wa leo Segerea; CDM na Leo tegemeeni kabisa mkutano wenu kukosa mvuto kwasababu ya idadi ndogo ya watu itakayokuwepo. Kwanini nasema hivi?
Leo katika uwanja wa Dodoma Kuna tukio la kuazimisha "SIKU YA TIMU YA WANANCHI (Yanga sc)" hili Ni tukio kubwa Sana na lenye mvuto wake kwa jiji la Dar na Tanzania kwa ujumla, hivyo Basi wakazi wa DSM zaidi ya elfu60 watakuwa uwanja wa Taifa kuazimisha siku hiyo na Maelfu kwa Maelfu ya Watanzania watakuwa busy kufuatilia tukio Hilo mitandaoni na kwenye runinga.
PILI; Leo huko Arusha Kuna mapambano mkali unaotarajiwa kulindima mnamo majila ya 9;30 alasiri Kati ya Simba na Namungo, Ikumbukwe hii Ni mechi mhimu Sana na yenye kuvuta attention za Watanzania wengi, hivyo watu watakuwa busy kufuatilia kinachojili katika hii mechi kuliko kuja au kufuatilia tukio la kisiasa. Mpaka hapo tunaona kabisa Simba na Yanga tu kwa leo inaenda kuteka Maelfu kwa Maelfu ya Watanzania kufuatilia Nini kinajili katika viwanja waliopo.
Finally; kwa maelezo hayo Ni dhahili kabisa kwa Siku tatu zote za kampeni mlizotumia Dar Naweza kusema mmepoteza pakubwa kuliko mlivyotegemea kupata, na hii imesababishwa na mpangilio mbovu wa ratiba za kampeni zenu.
Naipongeza Kamati ya kuratibu kampeni za CCM kwa kupanga Ratiba zao kwa kuoanisha na matukio mhimu mengine yanayotokea nchini. Siku ya Jana Tanzania hapakuwa na tukio kubwa la kuwafanya watu wasifuatilie uzinduzi wa kampen zao (³CCM) badala yake kampeni hiyo ndo ilikuwa tukio kubwa kwa Watanzania wengi, lakini kama CCM wangeweka siku ya ufunguzi wa kampeni zao kuwa leo Basi Ni dhahili wangepunguza idadi ya watu wengi Sana kuwafuatilia kutokana na matukio mhimu na yenye mvuto kwa Watanzania wengi yanayoendelea Leo Kama vile; Kusali, Siku ya Wananchi kwa Mkapa stadium na Fainal ya Ngao ya jamii Kati Simba sc na Namungo fc.
Mwisho; Najua tayari menejimenti inayoratibu kampeni za CDM ishachelewa kuleta ushawishi na shamlashamla za kampeni kwa jiji la Dar Basi naomba makosa mliyoyafanya ya kiratiba yasijirudie Tena huko mnakotarajia kwenda hasa kwenye majiji makubwa, Msiwaone CCM leo kuwa kimya angali Jana wamefungua kampeni wanajua leo Watanzania watakuwa busy kufuatilia Mambo ya Simba na Yanga hivyo wakiendesha mkutano hawatafuatiliwa na watu wengi. Nyie Hilo hamulioni nyie nikwenda tu matokeo yake mnaishia kuaibika kwa Kugeuza mkutano wa mgombea urais wenu kuonekana Kama mkutano wa Wagombea udiwani au mkutano wa vyama Kama SAU na CHAUMA.
#Wananchi wote Tukutane kwa Mkapa hapo baadae tuna letu Jambo pale.
#Wa Simba na Namungo Tukutane Kwenye Viunga vya Arusha tuna letu Jambo pale mtoto hatumwi dukani.
#Wakristo Tukutane Kwenye maombi ya jioni baada ya Ibada ya sasahivi tuna letu Jambo la baraka pale.
Ahsanteni muwe na J.pili njema,.
"Ni dhahili na ukweli usiopingika kuwa idadi ya Watanzania ambao wamekuwa wakijitokeza kwenye kampeni za CDM Ni ndogo mno ukilinganisha na matarajio yaliyokuwepo, Mfano hakuna alietegemea Kama kwenye ufunguzi wa kampeni pale Mbagala kutakuwa na idadi ndogo vile ya Wananchi utafikiri kampeni za mbunge au udiwani wakati Ni ufunguzi wa kampeni za Chama Tena chini ya mgombea urais kabisa, pia hata Jana pale kawe hiyo idadi ilikuwa ndogo Sana ukilinganisha na idadi ya kawe wakati wa Lowassa ".
JE NIWAPI MNAKOSEA HADI MNAKOSA WATU? JIBU HILI HAPA;
"DSM Ni jiji lenye mishemishe nyingi na watu wake Ni wenye mishemishe nyingi, hivyo usipopanga Ratiba zako vizuri kwa kuangalia na Ratiba zingine zinazoendelea ndani ya jiji Hilo Basi tegemea kujikuta upo mwenye tu katika hiyo Ratiba yako"
Hivyo Basi kosa kubwa walilolifanya waratibu kampeni za CDM walishindwa kupanga Ratiba za kampeni kwa kuendana na Ratiba za matukio muhimu yanayoendelea DSM, na hizi ndo hesabu za Ratiba zilizowachenga;
1. Ufunguzi wa kampeni siku ya ijumaa; Ndg zangu CDM mnatambua kabisa siku ya ijumaa huwa Kuna Ibada ya ijumaa ambayo Watoto, wanawake na wanaume huenda kuswalia msikitini kwa pamoja, na Mbagala Ni sehemu iliyo na waisilam wengi hivyo haikuwa rahisi watu wasitishe shughuli Yao mhimu ya kwenda kuswali kisa kwenda kuwasikiliza wanasiasa.
2. Kuendelea kwa kampeni Jana Kawe; waratibu kampeni za CDM walishindwa kuoanisha tukio kubwa lililokuwa linatokea Jana na tukio lao. Niukweli usiopingika kuwa, Ufunguzi wa kampeni za CCM Jana ulikuwa ukifuatiliwa na Watanzania wengi Sana waliokuwepo Dodoma na ambao hawakuwepo Kupitia mitandao na vyombo vya habari Kama TV, na hii nikutana na uzito wa chama hicho pia kuwa na wanachama wazito na wenye ushawishi katika jamii pia uwepo wa wasanii Wakubwa Tanzania Kama diamond, Konde boy , Alikiba, Nandy na n.k kuliongeza idadi ya Watanzania wengi wasing'atuke kwenye tv zao.
Hivyo Basi kwa maelezo hayo Wakazi wengi wa dar es salam waliungana na Watanzania wenzao kutoka mikoa mingine kufuatilia kilichokuwa kinaendelea pale Dodoma katika viwanja vya Jamuhuri na kujikuta wamekosa muda wa kuja kawe kwenye kampeni zenu. (Ikumbukwe Kuna baadhi ya wasanii waliokuwepo Jana Wana wafuasi wengi na mashabiki wao wengi kuliko hata baadhi ya wafuasi wa vyama baadhi hapa nchini).
3. Mkutano wa leo Segerea; CDM na Leo tegemeeni kabisa mkutano wenu kukosa mvuto kwasababu ya idadi ndogo ya watu itakayokuwepo. Kwanini nasema hivi?
Leo katika uwanja wa Dodoma Kuna tukio la kuazimisha "SIKU YA TIMU YA WANANCHI (Yanga sc)" hili Ni tukio kubwa Sana na lenye mvuto wake kwa jiji la Dar na Tanzania kwa ujumla, hivyo Basi wakazi wa DSM zaidi ya elfu60 watakuwa uwanja wa Taifa kuazimisha siku hiyo na Maelfu kwa Maelfu ya Watanzania watakuwa busy kufuatilia tukio Hilo mitandaoni na kwenye runinga.
PILI; Leo huko Arusha Kuna mapambano mkali unaotarajiwa kulindima mnamo majila ya 9;30 alasiri Kati ya Simba na Namungo, Ikumbukwe hii Ni mechi mhimu Sana na yenye kuvuta attention za Watanzania wengi, hivyo watu watakuwa busy kufuatilia kinachojili katika hii mechi kuliko kuja au kufuatilia tukio la kisiasa. Mpaka hapo tunaona kabisa Simba na Yanga tu kwa leo inaenda kuteka Maelfu kwa Maelfu ya Watanzania kufuatilia Nini kinajili katika viwanja waliopo.
Finally; kwa maelezo hayo Ni dhahili kabisa kwa Siku tatu zote za kampeni mlizotumia Dar Naweza kusema mmepoteza pakubwa kuliko mlivyotegemea kupata, na hii imesababishwa na mpangilio mbovu wa ratiba za kampeni zenu.
Naipongeza Kamati ya kuratibu kampeni za CCM kwa kupanga Ratiba zao kwa kuoanisha na matukio mhimu mengine yanayotokea nchini. Siku ya Jana Tanzania hapakuwa na tukio kubwa la kuwafanya watu wasifuatilie uzinduzi wa kampen zao (³CCM) badala yake kampeni hiyo ndo ilikuwa tukio kubwa kwa Watanzania wengi, lakini kama CCM wangeweka siku ya ufunguzi wa kampeni zao kuwa leo Basi Ni dhahili wangepunguza idadi ya watu wengi Sana kuwafuatilia kutokana na matukio mhimu na yenye mvuto kwa Watanzania wengi yanayoendelea Leo Kama vile; Kusali, Siku ya Wananchi kwa Mkapa stadium na Fainal ya Ngao ya jamii Kati Simba sc na Namungo fc.
Mwisho; Najua tayari menejimenti inayoratibu kampeni za CDM ishachelewa kuleta ushawishi na shamlashamla za kampeni kwa jiji la Dar Basi naomba makosa mliyoyafanya ya kiratiba yasijirudie Tena huko mnakotarajia kwenda hasa kwenye majiji makubwa, Msiwaone CCM leo kuwa kimya angali Jana wamefungua kampeni wanajua leo Watanzania watakuwa busy kufuatilia Mambo ya Simba na Yanga hivyo wakiendesha mkutano hawatafuatiliwa na watu wengi. Nyie Hilo hamulioni nyie nikwenda tu matokeo yake mnaishia kuaibika kwa Kugeuza mkutano wa mgombea urais wenu kuonekana Kama mkutano wa Wagombea udiwani au mkutano wa vyama Kama SAU na CHAUMA.
#Wananchi wote Tukutane kwa Mkapa hapo baadae tuna letu Jambo pale.
#Wa Simba na Namungo Tukutane Kwenye Viunga vya Arusha tuna letu Jambo pale mtoto hatumwi dukani.
#Wakristo Tukutane Kwenye maombi ya jioni baada ya Ibada ya sasahivi tuna letu Jambo la baraka pale.
Ahsanteni muwe na J.pili njema,.